Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 12 uku. 14-19
  • Uige Unyenyekevu wa Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uige Unyenyekevu wa Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NI MWEPESI KUMUKARIBIA YEHOVA
  • YEHOVA IKO NA USAWAZIKO
  • YEHOVA NI MUVUMILIVU
  • YEHOVA ANAONA BATU YA HALI YA CHINI
  • Iga Namna ya Kufikiri ya Yehova na Yesu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Kutoa Kutakuletea Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 12 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 50

WIMBO 48 Tutembee na Yehova Kila Siku

Uige Unyenyekevu wa Yehova

“Mukuwe waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.”—EFE. 5:1.

WAZO KUBWA

Kujifunza ni mu njia gani tunaweza iga unyenyekevu wa Yehova.

1. Juu ya nini unyenyekevu wa Yehova ni wa ajabu sana?

LEO mu dunia, batu benye biko na mamlaka habakuwake na unyenyekevu. Yehova yeye ni Mweza-Yote lakini ni munyenyekevu. (Zb. 113:​5-8) Yehova njo munyenyekevu kupita batu yote, hana kiburi hata kidogo. Tutaona ni mu njia gani ine Yehova anaonyesha sifa ya unyenyekevu. Tutaona pia namna Yesu anaiga unyenyekevu wa Baba yake. Kuchunguza ile mambo kutatusaidia tumukaribie Yehova zaidi na tuige hata zaidi sifa yake ya unyenyekevu.

NI MWEPESI KUMUKARIBIA YEHOVA

2. Zaburi 62:8 inaonyesha nini juu ya Yehova? (Ona pia picha ku.)

2 Haikuwake mwepesi kukaribia batu benye kiburi. Juu ya kiburi banatendaka mu njia yenye inafanya batu basijisikie huru kubakaribia ao baepuke tu kabisa kubakaribia. Lakini Yehova haiko vile! Juu Baba yetu wa mbinguni ni munyenyekevu, anatuomba tumukaribie na tumuambie mambo yenye iko natuhangaisha yenye iko mu moyo wetu. (Soma Zaburi 62:8.) Sawa tu vile baba mwenye upendo anakuwaka tayari kusikiliza mahangaiko ya batoto yake, Yehova anakuwaka tayari kusikiliza sala za batumishi yake. Na hata, mu Biblia muko sala za mingi zenye Yehova aliandikisha zenye zinaonyesha kama anapenda tumukaribie. (Yos. 10:​12-14; 1 Sa. 1:​10-18) Lakini tutafanya nini ikiwa wakati fulani tunajisikia sawa vile hatustahili kumukaribia Yehova?

Baba iko nasikiliza kwa uvumilivu mutoto wake mudogo wakati iko namufasiria vile alivunja bila kupenda kitu ya kutilia maua saa alikuwa nacheza.

Baba anamuiga Yehova, anasikiliza kwa unyenyekevu mutoto wake mwenye alivunja kitu ya kutilia maua wakati alikuwa nacheza (Ona fungu ya 2)


3. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anapenda tusali kwake kwa ukawaida?

3 Tunaweza kumukaribia Yehova katika sala hata kama tunawaza kama hatustahili upendo wake. Juu ya nini tunasema vile? Mu mufano wa Yesu wa mwana mupotevu, ule mwana alitubu lakini aliona kama hastahili kurudia kwa baba yake. Baba yake alitenda namna gani wakati aliona anarudia? Yesu alisema kama, wakati tu baba yake alimuona, “akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.” (Lu. 15:​17-20) Yesu alionyesha kama Yehova iko sawa ule baba mwenye upendo. Wakati batu benye balishavunjika moyo juu zamiri yabo iko nabahukumu ao juu ya mahangaiko banasali kwake, anabasikiliza kwa uangalifu. (Omb. 3:​19, 20) Juu iko na huruma, anabahakikishia kama anabapenda na anabafariji, sawa tu vile ule baba mwenye alikaribishaka mutoto wake. (Isa. 57:15) Anafanya vile namna gani? Mara mingi anafanya vile kupitia bazee, batu ya familia benye kuwa Mashahidi, na bandugu na badada bengine. (Yak. 5:​14, 15) Yehova anatutolea ile musaada juu anapenda tumukaribie.

4. Juu ya nini ilikuwa mwepesi kwa batu kumukaribia Yesu?

4 Yesu anamuiga Baba yake. Yesu ni munyenyekevu sawa Baba yake. Njo maana wakati alikuwa ku dunia batu balijisikia huru kumukaribia na kumuuliza maulizo. (Mk. 4:​10, 11) Na wakati alibauliza mawazo yabo, balimuambia kabisa vile balijisikia. (Mt. 16:​13-16) Na wakati balifanya makosa habakuogopa juu balijua kama Yesu alikuwa mwenye fazili, mwenye rehema, na muvumilivu. (Mt. 17:​24-27) Juu Yesu alimuiga Baba yake muzuri sana, banafunzi yake balifikia kumujua Yehova muzuri zaidi. (Yoh. 14:9) Balijifunza kama Yehova ni munyenyekevu na anapenda batu bamukaribie, haiko sawa viongozi wa dini wa mu ile wakati wenye hawakukuwa na huruma, walikuwa na kiburi, na hawakupenda batu babakaribie.

5. Namna gani unyenyekevu unaweza kufanya ikuwe mwepesi kwa bengine kutukaribia?

5 Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Kama tunakomalisha sifa ya unyenyekevu, itakuwa mwepesi kwa bengine kutukaribia. Kama mutu haiko munyenyekevu atasikilia bengine wivu, atakuwa na kiburi, na itakuwa nguvu kwake kusamehe; ile itafanya batu basimukaribie. Lakini kama mutu ni munyenyekevu atakuwa mwenye fazili, muvumilivu, na atakuwa tayari kusamehe; ile itafanya bengine bajisikie huru kumukaribia. (Kol. 3:​12-14) Bazee banapaswa kujikaza sana juu ikuwe mwepesi kwa bengine kubakaribia. Na juu babakaribie, itaomba bapitishe wakati pamoya nabo. Ni kusema, bazee banapaswa kujikaza kuhuzuria mikutano ku Jumba ya Ufalme pamoya na bengine, kuliko kufuata mikutano kupitia videokonferanse kama haiko lazima kufanya vile. Na wakati inawezekana, banajikaza kuhubiri nyumba kwa nyumba pamoya na ndugu na dada. Ile itafanya ndugu na dada babajue muzuri na batajisikia huru kuzungumuza nabo wakati biko na lazima ya musaada.

YEHOVA IKO NA USAWAZIKO

6-7. Leta mufano wenye kuonyesha namna Yehova anakuwaka tayari kubadilisha mawazo yake wakati batumishi yake banamulilia.

6 Batu mingi benye kiburi habakuwake na usawaziko na ile inafanyaka ikuwe nguvu kwabo kubadilisha mawazo yabo. Lakini juu Yehova ni munyenyekevu, anakuwaka na usawaziko na anakuwaka tayari kubadilisha mawazo yake hata kama yeye njo iko juu zaidi kupita batu yote. Ona namna alitendea Miriamu dada ya Musa. Miriamu na Haruni balikuwa nasema mubaya juu ya Musa, mwenye Yehova alikuwa natumikisha juu ya kuongoza batu yake. Kwa kufanya vile, ni Yehova njo balikuwa nakosea heshima. Kwa hiyo Yehova alimukasirikia Miriamu na akamupiga kwa ugonjwa wa ukoma. Lakini wakati Haruni alimulilia Musa amusaidie Miriamu, na Musa naye akamulilia Yehova amuponyeshe, Yehova hakushikilia maamuzi yake. Juu ni munyenyekevu, alimuponyesha Miriamu.—Hes. 12:​1-15.

7 Tena Yehova alionyesha unyenyekevu wakati alimusikiliza Mufalme Hezekia. Yehova alikuwa ametuma nabii Isaya aambie Mufalme Hezekia kama atakufa. Lakini Hezekia alimulilia Yehova amuponyeshe. Yehova alifanya nini? Yehova alimuonyesha rehema na akamuongezea miaka ingine 15 ya kuishi. (2 Fa. 20:​1, 5, 6) Kwa kweli, unyenyekevu unamuchochea Yehova aonyeshe huruma na akuwe tayari kubadilisha mawazo.

8. Ni mifano gani inaonyesha kama Yesu iko na usawaziko? (Marko 3:​1-6)

8 Yesu anaiga Baba yake. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alijikaza kufanyia batu mambo ya muzuri wakati iliwezekana. Kwa mufano, aliponyesha batu siku ya Sabato hata kama baadui yake habakufurahia ile. (Soma Marko 3:​1-6.) Yesu anaendelea kuonyesha usawaziko mu namna iko naongoza kutaniko ya Kikristo leo. Kwa mufano, wakati mutu fulani mu kutaniko anafanya zambi nzito, Yesu anamuvumilia na anamupatia nafasi ya kubadilika.—Ufu. 2:​2-5.

9. Namna gani tunaweza kuonyesha usawaziko? (Ona pia picha.)

9 Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Yehova anakuwaka na usawaziko mu namna yake ya kuwaza na kutenda. Tunapaswa kujikaza kumuiga. (Yak. 3:17) Kwa mufano, muzazi hapaswe kuachilia mutoto afanye byote byenye anapenda, lakini pia anapaswa kuonyesha usawaziko kwa kuepuka kumuomba afanye byenye binapita uwezo wake. Ni vile Yakobo alifanya, sawa vile habari yenye kuwa mu Mwanzo 33:​12-14 inaonyesha. Bazazi banyenyekevu na benye kuwa na usawaziko banapaswa pia kujikaza kuepuka kulinganisha batoto. Bazee Bakristo nabo banapaswa kuwa na usawaziko. Wakati bazee ba mingi mu baraza banakubaliana na uamuzi fulani wenye haupinge kanuni za Biblia, muzee mwenye iko na usawaziko anapaswa kuwa tayari kuitika hata kama yeye iko na mawazo tofauti. (1 Ti. 3:​2, 3) Na siye bote tunapaswa kujikaza kuelewa mawazo ya bengine hata kama tuko na mawazo tofauti. (Ro. 14:1) Kwa kweli, kila mutu mu kutaniko anapaswa kujikaza juu ‘usawaziko wake ujulikane kwa watu wote.’—Flp. 4:5.

Picha: Baba iko nahubiri nyumba kwa nyumba na batoto yake badogo. 1. Anafurahi wakati mutoto wake mwanaume fulani anatolea mutu broshua “Furahia Maisha Milele!” 2. Kisha, anafurahia wakati mutoto wake mwanamuke fulani karte ya jw.org.

Baba anaonyesha usawaziko juu ya mambo yenye anatazamia batoto yake bafanye mu mahubiri (Ona fungu ya 9)


YEHOVA NI MUVUMILIVU

10. Leta mifano yenye kuonyesha namna Yehova alionyesha uvumilivu.

10 Pengine na weye ulishaona kama batu ya kiburi habapendake kungoya. Kiburi inafanya basikuwe na uvumilivu. Lakini Yehova yeye haiko vile, yeye njo iko na uvumilivu kupita batu yote! Kwa mufano, mu siku za Noa Yehova alisema kama atangoya miaka 120 mbele aharibu batu babaya. (Mwa. 6:3) Kwa hiyo Noa alikuwa na wakati wa kukomalisha batoto na wa kujenga safina kwa musaada wa batu ya familia yake. Mufano ingine ni ya namna Yehova alionyesha Abrahamu uvumilivu wakati alizungumuza naye kupitia malaika. Malaika wa Yehova alimusikiliza Abrahamu kwa uvumilivu wakati alikuwa nauliza maulizo juu ya uharibifu wa Sodoma na Gomora. Mutu wa kiburi angeweza kuambia hivi Abrahamu: ‘Weye uko nani juu uniulize miye maulizo!’ Lakini juu Yehova ni munyenyekevu, alimuvumilia Abrahamu.—Mwa. 18:​20-33.

11. Sawa vile 2 Petro 3:9 inasema, juu ya nini Yehova anaonyesha uvumilivu leo?

11 Kwa unyenyekevu, Yehova iko naonyesha uvumilivu leo. Iko nangoya wakati wenye alishapanga kuharibu ulimwengu ufike. Juu ya nini iko naonyesha uvumilivu? “Kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (Soma 2 Petro 3:9.) Yehova iko tu napoteza wakati bure? Hapana! Mamilioni ya batu bameitika kweli na bamekuwa barafiki yake. Na tunatumainia kama batu bengine ba mingi zaidi batafanya vile. Lakini uvumilivu wa Yehova uko na mipaka. Yehova anapenda batu, lakini hataendelea kubavumilia na kubaacha bafanye byenye banapenda milele. Ataharibu batu babaya.—Hab. 2:3.

12. Namna gani Yesu anaiga uvumilivu wa Yehova?

12 Yesu anaiga Baba yake. Kwa miaka mingi, Yesu ameiga uvumilivu wa Yehova. Amejionea vile Shetani anasemea bongo Yehova na banadamu baaminifu. (Mwa. 3:​4, 5; Yob. 1:11; Ufu. 12:10) Yesu ameona pia vile banadamu bameteseka sana. Wazia vile anangoya kwa hamu “ili avunje kazi za Ibilisi”! (1 Yo. 3:8) Sasa, nini inasaidia Yesu aendelee kungoya ruhusa ya Yehova juu aharibu kabisa-kabisa kazi zote za Shetani? Jambo moya yenye inamusaidia ni hii: Yesu Kristo ni munyenyekevu njo maana anaacha Yehova aamue wakati wa kuleta mwisho.—Mdo. 1:7.

13. Namna gani Yesu alivumilia mitume wake, na juu ya nini alifanya vile?

13 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alivumilia mitume wake. Kwa mufano, balibishana tena na tena juu ya kujua nani njo mukubwa zaidi kati yabo. Lakini Yesu hakutingiza kichwa na kusema: ‘Haba batu habatabadilikaka!’ Aliendelea tu kubavumilia. (Lu. 9:46; 22:​24-27) Alikuwa hakika kama kisha wakati batabadilika. Na weye ulishakafanya kosa ileile tena na tena? Kama ni vile, pengine uko mwenye shukrani sana juu Mufalme wetu ni munyenyekevu na muvumilivu.

14. Namna gani unaweza kukomalisha sifa ya uvumilivu?

14 Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Ni kwa kujikaza kuwa na “akili ya Kristo,” juu ile inafanya ikuwe mwepesi zaidi kwetu kuwaza na kutenda sawa Yehova. (1 Ko. 2:16) Sasa tutafanya nini juu tuelewe muzuri akili ya Kristo? Tunapaswa kusoma Bitabu bya Injili. Kisha tunapaswa kukamata wakati ya kufikiri juu ya mambo yenye tunasoma na kuona namna inatusaidia kujua mawazo ya Yesu juu ya jambo fulani. Tena, tunapaswa kumuomba Yehova atusaidie juu tuige unyenyekevu na uvumilivu wa Yesu. Na wakati tunajikaza kuwa na akili ya Kristo, tutaiga zaidi Mungu wetu kwa kuvumilia bengine, na hata kujivumilia siye peke.—Mt. 18:​26-30, 35.

YEHOVA ANAONA BATU YA HALI YA CHINI

15. Leta mifano yenye kuonyesha kama Yehova anaona banyenyekevu kuwa ba maana. (Zaburi 138:6)

15 Soma Zaburi 138:6. Waza kidogo: Mwenye mamlaka zaidi mu ulimwengu anaona batu banyenyekevu. Ile ni pendeleo kubwa sana! Ona mifano fulani ya batu ba hali ya chini benye Yehova alitendea mu njia ya pekee. Bamoya kati yabo habajulikane sana, lakini Yehova aliandikisha habari yabo mu Biblia. Kwa mufano, Yehova aliongoza Musa aandike kuhusu Debora, mwenye alikuwa mutumishi muaminifu mu familia ya Yakobo na Isaka kwa miaka karibu 125! Hata kama hatujue mambo mingi juu ya ule mwanamuke muaminifu, Yehova alihakikisha kama jina yake inaandikwa mu Biblia juu ya kuonyesha kama alipendwa sana. (Mwa. 24:59; 35:​8, na maelezo ya chini) Miaka mingi kisha pale, Yehova alichagua Daudi, mwenye alikuwa muchungaji juu akuwe Mufalme wa taifa ya Israeli. (2 Sa. 22:​1, 36) Wakati kidogo kisha Yesu kuzaliwa, Mungu alituma bamalaika ku kikundi ya bachungaji juu ya kubajulisha kama Yesu, mwenye angekuwa Masiya, amezaliwa Betlehemu. Kwa kufanya vile, alibapatia pendeleo ya kuwa ba kwanza kujua ile habari. (Lu. 2:​8-11) Na wakati Yosefu na Maria balibeba Yesu ku hekalu, Yehova alipatia Simeoni na Ana pendeleo ya kuona Mwana wake. (Lu. 2:​25-30, 36-38) Kwa kweli, “ijapokuwa Yehova iko juu, yeye anaona wanyenyekevu”!

16. Namna gani Yesu aliiga namna ya Baba yake ya kutendea bengine?

16 Yesu anaiga Baba yake. Sawa Baba yake, Yesu alitendea kwa heshima batu ya hali ya chini. Alifundisha batu benye habakusoma sana na batu ba kawaida kweli kuhusu Ufalme wa Mungu. (Mdo. 4:13; Mt. 11:25) Tena, Yesu aliponyesha bagonjwa na alifanya vile mu njia yenye ilionyesha kama alibapenda na kubaheshimia. (Lu. 5:13) Busiku ya mwisho mbele bamuue, alifanya kazi ya mutumishi kwa kunawisha mitume wake migulu. (Yoh. 13:5) Na mbele apande mbinguni, aliheshimisha banafunzi yake banyenyekevu ba ile wakati na benye bangefuata kwa kubapatia kazi ya maana zaidi kupita zote: Kazi ya kusaidia batu bapate uzima wa milele.—Mt. 28:​19, 20.

17. Namna gani tunaweza kuonyesha bengine upendo na heshima? (Ona pia picha.)

17 Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Tunaonyesha batu upendo na heshima kwa kubahubiria habari njema, ikuwe balikomalia wapi, biko na rangi gani ya ngozi, ao balisoma masomo gani. Hata tukuwe na uwezo gani ao mapendeleo gani, tunaonyesha bandugu na badada yetu upendo na heshima kwa kubaona kuwa ba maana zaidi kutupita. (Flp. 2:3) Yehova anafurahi wakati tuko banyenyekevu na tuko ba kwanza kuonyeshana heshima mu zile njia na mu njia zingine.—Ro. 12:10; Sef. 3:12.

Badada bawili biko najifunza Biblia pamoya na mwanamuke moya mu gereza.

Tunaiga unyenyekevu wa Yehova wakati tunahubiria habari njema batu ba kila namna (Ona fungu ya 17)a


18. Juu ya nini unapenda kuiga unyenyekevu wa Yehova?

18 Wakati tunajikaza kuiga unyenyekevu wa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, inakuwa mwepesi zaidi kwa bengine kutukaribia, tunakuwa na usawaziko zaidi, tunakuwa bavumilivu zaidi, na tunaonyesha bengine upendo na heshima. Na ukumbuke kama wakati tunajikaza kuiga Mungu wetu munyenyekevu, atatuona kuwa ba maana zaidi!—Isa. 43:4.

NAMNA GANI UNYENYEKEVU UNAWEZA KUFANYA . . .

  • ikuwe mwepesi kwa bengine kukukaribia?

  • ukuwe na usawaziko?

  • ukuwe muvumilivu?

Wimbo 159 Mumupatie Yehova Utukufu

a MAFASIRIO YA PICHA: Badada fulani banaiga unyenyekevu wa Yehova kwa kuhubiria banamuke benye biko mu gereza.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine