PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA
Namna ya Kuwa Hakika Kama Yehova Anaweza Kukuokoa
Soma Hesabu 13:25–14:4 juu uone namna Baisraeli balionyesha kama habamutumainie Yehova.
Chunguza habari yote. Juu ya nini Baisraeli balipaswa kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kubaokoa wakati balitoka Misri? (Zb. 78:12-16, 43-53) Nini njo ilifanya baache kumutumainia Yehova? (Kum. 1:26-28) Namna gani Yoshua na Kalebu balionyesha kama banamutumainia Yehova?—Hes. 14:6-9.
Ujifunze mambo mingi zaidi. Baisraeli bangefanya nini juu batumainie Yehova zaidi? (Zb. 9:10; 22:4; 78:11) Juu ya nini inaomba tumuheshimie kwanza Yehova juu tuweze kumutumainia?—Hes. 14:11.
Unajifunza nini? Ujiulize hivi:
‘Inaweza kuwa nguvu kwangu kumutumainia kabisa Yehova mu hali gani?’
‘Ninaweza kufanya nini juu nimutumainie Yehova zaidi leo na mu siku zenye kuya?’
‘Wakati taabu kubwa itaanza ninaweza kuwa hakika na jambo gani?’—Lu. 21:25-28.