Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 10
Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.—Flp. 3:16.
Kama haufikie muradi wenye haupatane na uwezo wako, usiwaze kama Yehova ataona kuwa unashindwa. (2 Ko. 8:12) Ujifunze mambo fulani kupitia kizuizi yenye unakutana nayo.Usisahau miradi yenye ulishakafikia. Biblia inasema kama “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu.” (Ebr. 6:10) Na weye usisahau miradi yenye ulishakafikia, sawa vile kukomalisha urafiki wako pamoya na Yehova, kuambia wengine juu yake, ao kubatizwa. Sawa vile tu ulijikazaka kufikia miradi yako ya kiroho zamani, unaweza pia kujikaza kufikia miradi yako ya sasa.Kwa musaada wa Yehova, unaweza kuwa na furaha ya kufikia muradi wako Kila mara ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia, na ile itafanya ukuwe na furaha wakati uko najikaza kufikia miradi yako. (2 Ko. 4:7) Kama hauvunjike moyo, utapata baraka mingi hata zaidi.—Gal. 6:9. w23.05 31 fu. 16-18
Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 10
Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mumenipenda na mumeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.—Yoh. 16:27.
Yehova anapenda kuonyesha kama anakubali wale wenye anapenda. Maandiko inazungumuzia mara mbili zenye Yehova aliambia Yesu kama alikuwa Mwana wake mupendwa mwenye alikubali. (Mt. 3:17; 17:5) Unapenda kumusikia Yehova anasema kama anakukubali? Hatuwezi kusikia sauti ya Yehova, lakini anazungumuza na siye kupitia Neno yake. Tunaweza “kumusikia” Yehova anasema kuwa anatukubali wakati tunasoma maneno ya Yesu yenye kuwa mu Injili. Yesu alionyesha kwa ukamili utu wa Baba yake. Wakati tunasoma namna Yesu aliambia wafuasi wake waaminifu kama anawakubali hata kama hawakukuwa wakamilifu, tunaweza kuwazia kama ni Yehova njo iko natuambia ile maneno. (Yoh. 15:9, 15) Kama tunapata magumu, ile magumu haimaanishe kama Yehova hatukubali tena. Lakini inatupatia nafasi ya kuonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda na kumutumainia.—Yak. 1:12. w24.03 28 fu. 10-11
Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 11
Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa.—Mt. 21:16.
Kama uko muzazi, usaidie watoto wako watayarishe maelezo yenye kufaa kulingana na miaka yao. Wakati fulani, mambo mazito sawa vile magumu ya ndoa ao namna ya kuwa na mwenendo safi inazungumuziwaka wakati ya funzo. Hata vile, kunaweza kuwa fungu moya ao mbili kwenye mutoto anaweza kutoa maelezo. Tena, usaidie watoto wako waelewe juu ya nini kiongozi hatawataya kila mara wakati wananyangula mikono. Kufanya vile, kunaweza kuwasaidia wasikasirike wakati kiongozi anataya wengine. (1 Ti. 6:18) Siye wote tunaweza kutayarisha maelezo yenye itamutukuza Yehova na yenye itajenga Wakristo wenzetu. (Mez. 25:11) Kama tunazungumuzia jambo yenye inatuhusu, tunapaswa kuepuka kusema mambo mingi juu yetu. ( Mez. 27:2; 2 Ko. 10:18) Kuliko kufanya vile, tutakaza akili juu ya Yehova, Neno yake, na watu wake.—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 fu. 17-18