HABARI YA KUJIFUNZA YA 26
Muendelee Kuwa Tayari kwa Ajili ya Siku ya Yehova
“Siku ya Yehova inakuja sawasawa kabisa na vile mwizi anakuja usiku.”—1 TE. 5:2.
WIMBO 143 Uendelee Kufanya Kazi, Kukesha, na Kungojea
KIFUPI YA HABARIa
1. Tunapaswa kufanya nini ili tuokoke siku ya Yehova?
WAKATI Biblia inasema kuhusu “siku ya Yehova,” inazungumuzia wakati wenye Yehova ataharibu maadui wake na kuokoa watu wake. Zamani, wakati fulani Yehova alihukumu mataifa fulani. (Isa. 13:1, 6; Eze. 13:5; Sef. 1:8) “Siku ya Yehova” itaanza na uharibifu wa Babiloni Mukubwa na itaishia ku vita ya Armagedoni. Juu ya kuokoka ile “siku,” tunapaswa kujitayarisha kuanzia sasa. Kwa kweli, Yesu alifundisha kama tunapaswa ‘kuendelea kuwa tayari’ kwa ajili ya “taabu kubwa.” Alisema ile maneno ili kuonyesha kama tunapaswa kufanya vile bila kuacha.—Mt. 24:21; Lu. 12:40.
2. Juu ya nini maneno yenye kuwa mu 1 Watesalonike inaweza kutusaidia?
2 Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandikia Watesalonike barua yake ya kwanza. Mu ile barua, alizungumuzia mifano mingi ili kusaidia Wakristo waendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova ya hukumu. Mutume Paulo alijua kama siku ya Yehova haingekuya ile wakati. (2 Te. 2:1-3) Lakini, aliambia ndugu zake wajitayarishe kwa ajili ya ile siku sawa vile tu ingekuya kesho. Na siye pia tunapaswa kutumikisha ile shauri. Sasa tuzungumuzie namna anafasiria mambo yenye kufuata: (1) Namna siku ya Yehova itakuya, (2) nani njo hawataokoka, na (3) mambo yenye tunaweza kufanya ili kujitayarisha juu tuokoke.
SIKU YA YEHOVA ITAKUYA NAMNA GANI?
Wakati mutume Paulo aliandika 1 Watesalonike, alitumia mifano yenye inaweza kutusaidia (Ona fungu ya 3)
3. Ni mu maana gani siku ya Yehova itakuya sawa vile mwizi usiku? (Ona pia picha.)
3 “Vile mwizi anakuja usiku.” (1 Te. 5:2) Huu ni mufano wa kwanza kati ya mifano tatu yenye mutume Paulo anatumia ili kufasiria namna siku ya Yehova itakuya. Mara mingi wezi wanaibaka haraka na wanafanyaka vile usiku saa yenye watu hawawatazamie. Vilevile, siku ya Yehova itakuya kwa kushitukia na itashangaza watu wengi sana. Hata wamoja kati ya Wakristo wa kweli wanaweza kushangaa juu ya namna mambo itatokea haraka. Lakini siye, hatutaharibiwa sawa vile waovu.
4. Ni mu maana gani siku ya Yehova itakuwa sawa vile maumivu ya kuzala?
4 “Kama vile maumivu ya kuzaa ya mwanamuke mwenye mimba.” (1 Te. 5:3) Mama mwenye kuwa na mimba hajuake kabisa wakati wenye atazala. Lakini, anakuwaka hakika kama atazala tu. Na wakati saa yake ya kuzala inafika, pengine anaweza kuzala kwa kushitukia, kwa maumivi, na hawezi kuiponyoka. Vilevile, hatujue siku na saa yenye siku ya Yehova itaanza. Lakini, tuko hakika kama itakuya na kama Mungu atahukumu waovu kwa kushitukia na hawataponyoka.
5. Ni mu maana gani taabu kubwa itakuwa sawa vile asubui sana?
5 Sawa vile asubui sana. Mu mufano wa tatu wenye Paulo alizungumuzia, anataya tena wezi wenye wako naiba usiku. Lakini mara hiyo, analinganisha siku ya Yehova na asubui sana. (1 Te. 5:4) Wezi wenye wanakuyaka kuiba usiku wanaweza kusahau kama saa iko napita. Kwa hiyo, mwangaza wa asubui unaweza kufanya waonekane na wakamatwe. Vilevile, taabu kubwa inaweza kuonyesha wazi wale wenye kuwa sawa vile wezi, ni kusema, wale wenye wanabakia mu giza kwa kuendelea kufanya mambo yenye haimufurahishe Mungu. Tofauti nao, tunaweza kuwa tayari kwa kuachana na mambo yenye haimufurahishe Yehova na kwa kuendelea kufuatilia “kila namna ya wema, na haki, na kweli.” (Efe. 5:8-12) Sasa Paulo anazungumuzia mifano mbili yenye iko na uhusiano ili kuzungumuzia wale wenye hawataokoka.
NANI NJO HAWATAOKOKA SIKU YA YEHOVA?
6. Ni mu maana gani watu wengi sana wanalala? (1 Watesalonike 5:6, 7)
6 “Wale wenye wanalala.” (Soma 1 Watesalonike 5:6, 7.) Paulo alilinganisha wale wenye hawataokoka siku ya Yehova na watu wenye wanalala. Hawajue mambo yenye iko nafanyika pembeni yao ao kama wakati iko napita. Kwa hiyo, hawawezi kujua wakati jambo fulani ya maana inatokea na hawawezi kufanya kitu. Watu wengi sana leo wanalala mu maana ya kiroho. (Ro. 11:8) Hawaamini mambo yenye kuonyesha kama tuko naishi mu “siku za mwisho” na yenye kuonyesha kama taabu kubwa itakuya hivi karibuni. Mambo makubwa yenye kufanyika mu dunia leo inaweza kufanya watu fulani walamuke mu usingizi wa kiroho na waanze kupenda kusikia habari njema ya Ufalme yenye tuko nahubiri. Hata vile, wengi wako narudia kulala kuliko kuwa macho. Hata watu fulani wenye wanaamini kama siku ya hukumu itakuya, wanawazaka kama ingali mbali. (2 Pe. 3:3, 4) Kwa hiyo, ni jambo ya maana sana kwetu kuwa macho kila siku.
7. Ni mu maana gani wale wenye Mungu ataharibu wako sawa vile walevi?
7 “Wale wenye wanalewa.” Mutume Paulo alilinganisha wale wenye Mungu ataharibu na walevi. Kwa kawaida, wakati mutu analewa hatendake haraka kama kunatokea jambo fulani pembeni yake, na hakamatake maamuzi ya muzuri. Vilevile, waovu hawatendake kulingana na mashauri ya Mungu. Wanachagua njia yenye itawapeleka ku uharibifu. Lakini, Wakristo wanaombwa kulinda akili zao, ni kusema, kuwa na akili timamu. (1 Te. 5:6) Mutu fulani mwenye kuwa na elimu ya Biblia anafasiria kama mutu mwenye kuwa na akili timamu anakuwaka mwenye “kutulia na haogopake sana, tena anakuwaka nafikiri ili kukamata uamuzi wa muzuri.” Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa wenye kutulia? Juu tusijiingize mu mambo ya politike ao mu mambo ya maisha. Kadiri siku ya Yehova iko nakaribia ni vile mukazo wa kuunga mukono mu ile mambo uko naongezeka. Njo maana, hatupaswe kuhangaika sana juu ya mambo yenye tutafanya. Roho takatifu ya Mungu inaweza kutusaidia ili tukuwe wenye kutulia, tusiogope, na tukamate maamuzi ya muzuri.—Lu. 12:11, 12.
TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUJITAYARISHA KWA AJILI YA SIKU YA YEHOVA?
Leo watu hawako macho, lakini, siye tunaendelea kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova kwa kuvala bamba ya kifua ya imani, upendo, na kofia ya tumaini (Ona fungu ya 8, 12)
8. 1 Watesalonike 5:8 inazungumuzia sifa gani zenye zinaweza kutusaidia tukuwe macho na tulinde akili zetu? (Ona pia picha.)
8 “Kuvaa bamba la kifua . . . na . . . kofia ya chuma.” Paulo anatulinganisha na maaskari wenye kuwa macho na wenye kuvala muzuri kwa ajili ya vita. (Soma 1 Watesalonike 5:8.) Askari anapaswa kuwa tayari kupigana kila wakati kama vita inaanza. Ni vile pia kwetu. Tunaendelea kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova kwa kuvala bamba ya kifua ya imani, upendo, na kofia ya chuma ya tumaini. Zile sifa zinaweza kutusaidia sana.
9. Imani inatulindaka namna gani?
9 Bamba ya kifua ilikuwa nalinda moyo wa askari. Imani na upendo inalindaka moyo wetu wa mufano. Njo sifa zenye zitatusaidia tuendelee kumutumikia Mungu na kumufuata Yesu. Juu tuko na imani, tuko hakika kama Yehova atatupatia zawabu kama tunaendelea kumutafuta kwa moyo wote. (Ebr. 11:6) Imani itatusaidia tuendelee kuwa washikamanifu kwa Kiongozi wetu, Yesu, hata kama inaomba tuvumilie magumu. Tunaweza kufanya imani yetu ikuwe nguvu ili tuweze kuvumilia kwa kujifunza mambo fulani kupitia mifano ya watu wa leo wenye waliendelea kuwa washikamanifu ijapokuwa mateso ao magumu ya kupata makuta. Na tunaweza kuepuka hatari ya kupenda sana makuta na vitu vya kimwili kama tunaiga wale wenye walifanya maisha yao ikuwe mwepesi ili kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza.b
10. Namna gani kupenda Mungu na jirani kunatusaidia kuvumilia mu kazi ya mahubiri?
10 Upendo ni wa maana pia ili tukuwe macho na kulinda akili zetu. (Mt. 22:37-39) Kumupenda Mungu kunatusaidia tuhubiri kwa uvumilivu hata kama ile inaweza kufanya tupate magumu. (2 Ti. 1:7, 8) Tunaendelea kuhubiri mu maeneo yetu kwa kutumia telefone na hata barua juu tunapenda pia wale wenye hawamutumikie Yehova. Tunatumainia kama siku moya majirani wetu watabadilika na kuanza kufanya mambo ya muzuri.—Eze. 18:27, 28.
11. Kupenda ndugu na dada zetu kunatusaidia namna gani? (1 Watesalonike 5:11)
11 Tunapenda pia ndugu na dada zetu. Tunaonyesha ule upendo kwa “kutiana moyo na kujengana.” (Soma 1 Watesalonike 5:11.) Sawa vile maaskari wenye hawaachanake mu vita, siye pia tunatianaka moyo. Kusema kweli, askari anaweza kuumiza askari mwenzake wakati wa vita, lakini hawezi kufanya vile kwa kupenda. Na siye hatuwezi kukwaza ndugu na dada zetu kwa kupenda ao kurudisha ubaya kwa ubaya. (1 Te. 5:13, 15) Tunaonyesha pia kama tuko na upendo kwa kuheshimia ndugu wenye wanasimamia kutaniko. (1 Te. 5:12) Wakati mutume Paulo aliandika barua yake ya kwanza kwa Watesalonike, ile kutaniko ilikuwa haiyafanya hata mwaka moya. Inawezekana wanaume wenye walikuwa naisimamia hawakukuwa na uzoefu na pengine walifanya makosa fulani. Hata vile, ndugu na dada walipaswa tu kuwaheshimia. Kadiri taabu kubwa iko nakaribia, tutakuwa na lazima zaidi ya muongozo wa wazee wa kutaniko yetu kuliko vile tunakuwaka nao lazima leo. Inaweza kuwa nguvu kupata muongozo kutoka kwa ndugu wa makao makubwa ao wa biro ya tawi, njo maana ni jambo ya maana sana kupenda na kuheshimia wazee wetu kuanzia sasa. Hata kutokee nini, tunapaswa kulinda akili zetu, hapana kukaza akili juu ya uzaifu wao, lakini kukumbuka kama Yehova iko naongoza wale wanaume waaminifu kupitia Kristo.
12. Tumaini yetu inalindaka mawazo yetu namna gani?
12 Tumaini ya wokovu inalindaka mawazo yetu sawa vile tu kofia ya chuma ilikuwaka nalinda kichwa ya askari. Kama tuko na tumaini ya nguvu, tutaona kama mambo yenye ulimwengu unaweza kutupatia haina maana. (Flp. 3:8) Tumaini yenye tuko nayo inatusaidia tuendelee kutulia na tusiogope. Na njo vile ilikuwa kuhusu Wallace na Laurinda, wenye wako natumika ku Beteli mu Afrika. Mu majuma tatu, mama yake na Laurinda na baba yake na Wallace walikufa. Juu ya ugonjwa wa korona, Laurinda na Wallace walishindwa kurudia kwao ili wakuwe pamoya na familia zao. Wallace alisema hivi: “Juu niko na tumaini ya ufufuo, niko nafikiria namna watakuwa mu siku zao za kwanza mu dunia mupya, hapana namna walikuwaka mu siku za mwisho za maisha yao mu hii dunia. Ile tumaini inanitulizaka wakati niko napambana na huzuni ya kufiwa.”
13. Tunapaswa kufanya nini ili tupate roho takatifu?
13 “Musizimishe moto wa roho.” (1 Te. 5:19) Paulo alilinganisha roho takatifu na moto wenye kuwa ndani yetu. Mutu mwenye kuwa na roho ya Mungu, anakuwaka na bidii, anapendaka kufanya mambo ya muzuri, na anafurahiaka kufanya kazi ya Yehova. (Ro. 12:11) Tunapaswa kufanya nini ili tupate roho takatifu? Tunapaswa kumuomba Mungu atupatie ile roho, kujifunza Neno yake, na kujiunga na tengenezo yake yenye kuongozwa na roho. Kufanya vile kutatusaidia tuonyeshe “tunda la roho.”—Gal. 5:22, 23.
Ujiulize hivi, ‘Matendo yangu inaonyesha kama napenda kuendelea kupata roho ya Mungu?’ (Ona fungu ya 14)
14. Tunapaswa kuepuka kufanya nini ili Mungu aendelee kutupatia roho yake takatifu? (Ona pia picha.)
14 Wakati Mungu anatupatia roho takatifu, tunapaswa kuwa waangalifu juu ‘tusizimishe moto wa roho.’ Mungu anapatiaka tu roho takatifu wale wenye wanaendelea kuwa na mawazo na mwenendo muzuri. Hataendelea kupatia roho yake takatifu mutu mwenye iko na mawazo ya mubaya na mwenye iko na mwenendo mubaya. (1 Te. 4:7, 8) Juu Mungu aendelee kutupatia roho takatifu, tunapaswa pia kuepuka ‘kuzarau maneno ya unabii.’ (1 Te. 5:20) Mu hii andiko, neno “unabii” maana yake ujumbe mbalimbali wenye Yehova anatupatia kupitia roho yake takatifu, kutia ndani mambo yenye inahusu siku yake na namna tunaweza kutenda kwa uharaka leo. Tusiwaze kama siku ya Yehova ao Armagedoni itakuyaka wakati tutakuwa tulishakufa. Kuliko kuwaza vile, tunaonyesha kama tunatazamia kuwa itakuya hivi karibuni ao tunaichunga kabisa mu akili yetu kwa kuendelea kuwa na “vitendo vya ushikamanifu kwa Mungu” kila siku na kwa kuendelea kuwa na mwenendo muzuri.—2 Pe. 3:11, 12.
“MUCHUNGUZE MAMBO YOTE”
15. Tunapaswa kufanya nini ili tusipotoshwe na habari yoyote ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu? (1 Watesalonike 5:21)
15 Hivi karibuni, watu wenye kumupinga Mungu watatangaza mu maana fulani hivi: “Amani na usalama!” (1 Te. 5:3) Habari ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu itayala mu dunia na itapotosha watu wengi sana. (Ufu. 16:13, 14) Halafu siye? Hatutapotoshwa kama ‘tunachunguza [ao ‘kujaribu’] mambo yote.’ (Soma 1 Watesalonike 5:21; ona maelezo ya funzo.) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “muchunguze” ilikuwa natumiwa ili kuonyesha namna watu walikuwa napima metali sawa vile zahabu na feza ili kujua kama zilikuwa za kweli. Kwa hiyo, siye pia tunapaswa kujaribu ao kuchunguza maneno yenye tunasikia ao mambo yenye tunasoma ili kuona kama ni ya kweli ao hapana. Ilikuwa jambo ya maana kwa Watesalonike kufanya vile, na itaendelea kuwa ya maana zaidi sana kwetu kadiri taabu kubwa iko nakaribia. Kuliko kuamini kila jambo yenye watu wanasema, tunatumia uwezo wetu wa kufikiri ili kulinganisha mambo yenye tunasoma ao yenye tunasikia na mambo yenye Biblia na tengenezo ya Yehova inasema. Kama tunafanya vile, hatutapotoshwa na habari yoyote ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu.—Mez. 14:15; 1 Ti. 4:1.
16. Tuko na tumaini gani na tunaazimia kufanya nini?
16 Tunajua kama watumishi wa Mungu wataokoka taabu kubwa. Lakini, hakuna mwenye anajua mambo ya kesho. (Yak. 4:14) Hata vile, ikuwe tutakuwa tungali wazima wakati wa taabu kubwa ao kama tutakufa mbele ianze, tutapata zawabu ya uzima wa milele kama tunaendelea kuwa waaminifu. Watiwa-mafuta watakuwa pamoya na Kristo mbinguni. Kondoo wengine watakuwa mu paradiso hapa ku dunia. Tuendelee basi kukaza akili yetu juu ya tumaini yetu ya muzuri na tuendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova!
WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe
a Mu 1 Watesalonike sura ya 5, muko mifano mbalimbali yenye inatufundisha mambo fulani kuhusu siku ya Yehova yenye itakuya. Ile “siku” ni nini, na itakuya namna gani? Nani njo wataokoka? Nani njo hawataokoka? Tunaweza kufanya nini ili kuwa tayari kwa ajili ya ile siku? Tutazungumuzia maneno ya mutume Paulo na tutajibia ile maulizo.
b Ona sehemu “Walijitoa kwa Kujipendea.”