Ezekieli
13 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii juu ya manabii wa Israeli,+ na uambie wale wenye kutunga unabii wao wenyewe,*+ ‘Musikie neno la Yehova. 3 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Ole wao manabii wajinga, wenye kufuata roho yao wenyewe, wakati hawakuona kitu chochote!+ 4 Ee Israeli, manabii wako wamekuwa kama mbweha kati ya mabomoko. 5 Hamutaenda mahali kwenye kubomoka katika kuta za majiwe ili kuzijenga upya kwa ajili ya nyumba ya Israeli,+ ili Israeli aendelee kusimama katika vita katika siku ya Yehova.”+ 6 “Wameona maono ya uongo na kutabiri uongo, wale wenye kusema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati Yehova mwenyewe hakuwatuma, na wamengojea neno lao litimie.+ 7 Je, haiko maono ya uongo ndiyo mumeona na uongo ndio mumetabiri wakati munasema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati sikusema jambo lolote?”’
8 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “‘Kwa sababu mumesema uongo na maono yenu ni ya uongo, mimi niko juu yenu,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”+ 9 Mukono wangu uko juu ya manabii wenye maono yao ni ya uongo na wenye kutabiri uongo.+ Hawatakuwa kati ya watu wenye ninaambia siri zangu; wala hawataandikwa katika kitabu cha kuandikishia cha nyumba ya Israeli; wala hawatarudia katika inchi ya Israeli; na mutalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.+ 10 Hayo yote ni kwa sababu wamepotosha watu wangu kwa kusema, “Kuko amani!” wakati hakuna amani.+ Wakati ukuta zaifu wa kutenganisha unajengwa, wanaupiga lipu kwa chokaa.’*+
11 “Ambia wale wenye kupiga lipu kwa chokaa kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa yenye kufurika itakuja, mvua ya majiwe itaanguka,* na zoruba kali zenye upepo mukali zitaubomoa.+ 12 Na wakati ukuta utaanguka mutaulizwa, ‘Chokaa yenye mulipakaa iko wapi?’+
13 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Nitafanya zoruba kali zenye upepo mukali zilipuke katika kasirani yangu kali, na mvua kubwa yenye kufurika katika hasira yangu, na mvua ya majiwe katika kasirani yangu kali yenye kuharibu. 14 Nitabomoa ukuta wenye mumepiga lipu kwa chokaa na nitauangusha chini, na musingi wake utafunuliwa. Wakati muji utaanguka, mutaangamia ndani yake; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
15 “‘Wakati nitamwanga kasirani yangu kali yote juu ya ukuta huo na juu ya wale wenye kuupiga lipu kwa chokaa, nitawaambia: “Ukuta hauko tena, na wale wenye kuupiga lipu hawako tena.+ 16 Manabii wa Israeli hawako tena, wale wenye kutolea Yerusalemu unabii na kuona maono ya amani kwa ajili yake, wakati hakuna amani,”’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
17 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, elekeza uso wako juu ya mabinti wa watu wako wenye kutunga unabii wao wenyewe, na utoe unabii juu yao. 18 Uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Ole wao wanamuke wenye kushona pamoja tepe kwa ajili ya mikono yote* na kutengeneza vitambaa kwa ajili ya vichwa vya kila ukubwa ili kuwinda uzima wa* watu! Je, munawinda uzima wa* watu wangu na kujaribu kulinda uzima wenu?* 19 Je, mutanichafua kati ya watu wangu kwa ajili ya mikono ya shayiri na kwa ajili ya vipande vya mukate,+ mukiua wale wenye hawastahili* kufa na kulinda wale wenye hawastahili* kuishi, mukifanya vile kwa kudanganya watu wangu, wenye kusikiliza uongo wenu?”’+
20 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, nitakamata hatua juu ya tepe zenu, Enyi wanamuke, zenye munatumia kuwinda watu* kama vile wao ni ndege, na nitaziondoa kwenye mikono yenu na kufungua watu wenye munawinda kama ndege. 21 Nitapasua vitambaa vyenu vya kufunika kichwa na kukomboa watu wangu katika mukono wenu, nao hawatakuwa tena kitu cha ninyi kukamata katika kuwinda; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 22 Kwa sababu mumemuvunja moyo mwenye haki kwa uongo wenu+ wakati mimi mwenyewe sikukuwa nimemuletea taabu,* na mumetia nguvu mikono ya muovu,+ ili asiache njia yake ya mubaya na kuendelea kuishi.+ 23 Kwa hiyo, ninyi wanamuke hamutaona tena maono ya uongo na kufanya uaguzi;+ na mimi nitakomboa watu wangu katika mukono wenu, na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”