Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 10
Bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe.—Efe. 5:28.
Yehova anatazamia kwamba bwana amupende bibi yake na ahangaikie mahitaji yake ya kiroho, ya kimwili, na akuwe rafiki muzuri kwake. Kuwa na uwezo wa kufikiri, kuheshimia wanamuke, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia kuwa bwana muzuri. Kisha kuoa, munaweza kuwa na watoto. Mufano wa Yehova unaweza kukufundisha nini kuhusu kuwa baba muzuri? (Efe. 6:4) Yehova aliambia waziwazi Yesu, mwana wake, kama anamupenda na anamukubali. (Mt. 3:17) Kama unakuwa baba, uhakikishie watoto wako kwa ukawaida kama unawapenda. Ukuwe na zoea ya kuwapongeza juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Baba wenye wanamuiga Yehova wanasaidia watoto wao wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya ile daraka kwa kupenda na kuhangaikia watu wa familia yako na wa mu kutaniko, na kwa kujifunza kuwaonyesha kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana.—Yoh. 15:9. w23.12 28-29 fu. 17-18
Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 10
[Yehova] ndiye anafanya nyakati zako kuwa imara.—Isa. 33:6.
Siye watumishi waaminifu wa Yehova tunapambana na magumu yenye watu wote wanapataka. Tunaweza pia kupambana na upinzani ao mateso kutoka kwa wale wenye wanachukia watu wa Mungu. Hata kama Yehova hazuie ile magumu isitupate, anatuahidi kama atatusaidia. (Isa. 41:10) Kwa musaada wake tunaweza kuendelea kuwa na furaha, kukamata maamuzi ya muzuri, na kuendelea kuwa washikamanifu, hata mu hali za nguvu sana. Yehova anaahidi kutupatia jambo yenye Biblia inaita “amani ya Mungu.” (Flp. 4:6, 7) Ile amani ni utulivu wa akili na wa moyo wenye mutu anakuwaka nao kwa sababu ya uhusiano muzuri wenye iko nao pamoja naye. Ile amani “inapita uelewaji wote”; inapita jambo yoyote yenye tunaweza kuwazia. Ulishakasikia utulivu wa ajabu kisha kusali kwa Yehova? Ile yenye ulisikiaka njo “amani ya Mungu.” w24.01 20 fu. 2; 21 fu. 4
Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 10
Acha nimusifu Yehova; Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.—Zb. 103:1.
Watu waaminifu wanamupenda Mungu, na ile inawachochea wasifu jina yake kwa moyo wote. Mufalme Daudi alielewa kama kusifu jina ya Mungu ni kumusifu Mungu mwenyewe. Jina ya Mungu, Yehova, inamaanisha mambo mingi, inatukumbusha sifa zake za muzuri, na matendo yake ya ajabu. Daudi aliona jina ya Baba yake kuwa takatifu na aliisifu. Alipenda kufanya vile kwa “kila kitu chenye kuwa ndani” yake, ni kusema, kwa moyo wote. Kuhusu kumusifu Yehova, Walawi njo walikuwa ku mustari wa mbele. Kwa unyenyekevu, walikubali kama maneno yao haingeweza kusifu jina ya Yehova kwa ukamili vile inastahili. (Ne. 9:5) Bila shaka, ile sifa yenye kutoka ku moyo na yenye kufanywa kwa unyenyekevu, ilifurahisha moyo wa Yehova. w24.02 9 fu. 6