‘Muendelee Kufanya Hivi’ Tutafanya Ukumbusho Tarehe 5 Mwezi wa 4
1. Sababu gani siku ya Ukumbusho ni ya lazima sana?
1 ‘Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.’ (Luka 22:19) Yesu aliposema maneno hayo, aliwaamuru wafuasi wake wafanye Ukumbusho wa kifo chake. Kwa sababu zabihu ambayo Yesu alitoa imetutimizia mambo mengi, Ukumbusho wa kifo cha Yesu unaofanywa kila mwaka ndio siku ya lazima sana kwa Wakristo. Mwaka huu tutafanya Ukumbusho tarehe 5 mwezi wa 4. Kwa sababu tarehe hiyo inakaribia, namna gani tunaweza kumuonyesha Yehova shukurani yetu?—Kol. 3:15.
2. Namna gani tunaweza kutayarisha mioyo yetu kwa ajili ya Ukumbusho?
2 Tujitayarishe: Kwa kawaida tunajitayarisha kwa ajili ya mambo ambayo tunaona kuwa ya lazima. Tunaweza kutayarisha mioyo yetu kwa kuzungumuzia katika familia mambo yaliyotokea katika siku za mwisho za maisha ya Yesu hapa duniani, na kuchukua wakati wa kufikiri sana juu ya mambo hayo. (Ezra 7:10) Maandiko machache yanayoonyesha mambo hayo yanapatikana kwenye kalenda na katika kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku, lakini maandiko mengi zaidi yanaonyeshwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/02/2011, ukurasa wa 23-24 pamoja na sura za kitabu Mtu Mkuu Zaidi zinazozungumuzia mambo hayo.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona Ukumbusho kuwa jambo la lazima?
3 Tuhubiri Zaidi: Tunaweza pia kuonyesha kama Ukumbusho ni jambo la lazima kwetu kwa kuhubiri zaidi, kadiri tunavyoweza. (Luka 6:45) Kampanye ya duniani pote ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho itaanza Siku ya Posho, tarehe 17 mwezi wa 3. Je, unaweza kupanga wakati wako vizuri ili kupitisha wakati mwingi katika mahubiri? Kwa hiyo, labda unaweza kuwa painia musaidizi! Ikiwa unawaza kufanya hivyo, munaweza kuzungumuzia jambo hilo katika familia wakati wa Ibada yenu ya Familia ya mangaribi.
4. Tunaweza kupata faida gani kwa kuhuzuria Ukumbusho?
4 Tunapata faida nyingi kwa kuhuzuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu kila mwaka! Tunapohuzuria Ukumbusho, furaha yetu inaongezeka na tunamupenda Mungu zaidi. Tunafikiri juu ya ukarimu ambao Mungu alituonyesha kwa kutoa Mwana wake muzaliwa-pekee ili awe zabihu ya ukombozi. (Yoh. 3:16; 1 Yoh. 4:9, 10) Kwa kufikiri juu ya hayo, tunasukumwa tusiishi tena kwa ajili yetu wenyewe. (2 Kor. 5:14, 15) Tena, tunakuwa na tamaa ya kumusifu Yehova mbele ya watu wengine. (Zab. 102:19-21) Kweli kabisa, watumishi wa Yehova wenye shukurani wanangojea kwa hamu Ukumbusho utakaofanywa tarehe 5 mwezi wa 4 ili ‘kutangaza kifo cha Bwana.’—1 Kor. 11:26.