Musaada kwa Ajili ya Banamuke Benye Kutendewa Mubaya
“BANAMUKE mingi sana mu dunia yote bametendewa mubaya. Na weye ulishakatendewa mubaya? Ona juu ya nini Mungu anahangaikia usalama wako, na mambo yenye atafanyia bale benye banatendea banamuke mubaya.”
Habari “Mawazo ya Mungu juu ya Usalama wa Banamuke,” yenye kuwa ku jw.org inaanza na ile maneno. Ku mwisho ya ile habari kuko lien yenye itakusaidia uchukue PDF ya ile habari, kisha unaweza kuichapisha na kuikunja na inakuwa trakte ya kurasa ine. Dada mwenye kuishi mu Amerika mwenye kuitwa Stacy anasema hivi: “Nilichapisha kopi za ile habari, kisha miye na dada moya tukazibeba fasi fulani mu eneo yetu, kwenye banamuke benye banatendewaka mubaya banakimbiliaka.”
Mwanamuke fulani mwenye alikuwa natumika kule, alitulomba tulete kopi zingine juu agabulie batu benye banaishi pale. Kwa hiyo, tulibaachia kopi zaidi ya 40 za ile habari, na karte 30 za jw.org. Wakati tulibarudilia tena, musimamizi wa ile fasi alitulomba tuonyeshe banamuke benye kuishi pale namna tunajifunzaka Biblia na batu.
Stacy na badada bengine bawili balienda fasi ingine ya vile, ya kuhangaikia banamuke benye banatendewaka mubaya. Kule baliacha kopi tano za ile trakte na bakabalomba balete zingine. Mwanamuke fulani mwenye anatumikaka ile fasi alisema hivi: “Hii habari itasaidia banamuke benye biko hapa.” Aliongeza hivi: “Tuko nayo lazima.” Wakati badada balirudia tena ile fasi, banamuke benye banaishi pale baliikala fasi moya juu babaonyeshe vile tunajifunzaka Biblia na batu, na bawili kati yabo balipenda kufika ku mukutano wa mwisho wa juma ku Jumba ya Ufalme.
Stacy anasema hivi: “Inatugusa sana kuona vile batu banafurahia hii habari. Wakati tunaichapisha na kuikunja juu ya kuitumikisha mu mahubiri, inakuwa njia ya muzuri ya kutangazia habari njema ya Ufalme banamuke benye banatendewa mubaya. Tulifurahi kuona vile batu balipenda sana ile habari, na namna Yehova alibariki mambo yenye tulijikaza kufanya juu ya kutangazia habari njema bale banamuke.”