Zaburi
Sala ya Daudi.
17 Sikia sihi yangu ya kuomba haki, Ee Yehova;
Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada;
Sikiliza sala yangu ninayosema bila udanganyifu.+
2 Nawe ufanye uamuzi wa haki kwa niaba yangu;+
Macho yako na yaone yaliyo sawa.
3 Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+
Umenisafisha;+
Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,
Na kinywa changu hakijatenda dhambi.
4 Kuhusiana na shughuli za wanadamu,
Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za mnyang’anyi.+
5 Acha hatua zangu zibaki kwenye njia zako
Ili miguu yangu isijikwae.+
6 Ninakuita wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu.
Nitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+
7 Onyesha upendo wako mshikamanifu kwa njia yenye kustaajabisha,+
Ee Mwokozi wa wale wanaokimbilia mkono wako wa kuume
Kutoka kwa wale wanaokuasi.
9 Nilinde kutokana na waovu wanaonishambulia,
Kutokana na maadui wangu* wanaoweza kufa ambao wananizingira.+
10 Wamekufa ganzi;*
Kwa kinywa chao wanaongea kwa kiburi;
11 Sasa wanatuzingira;+
Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.*
12 Yeye ni kama simba anayetamani kurarua windo lake vipandevipande,
Kama mwanasimba anayenyemelea mafichoni.
13 Inuka, Ee Yehova, ukabiliane naye+ na kumwangusha chini;
Niokoe* kutoka kwa mwovu kwa kutumia upanga wako;
14 Niokoe kwa mkono wako, Ee Yehova,
Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* ambao fungu lao liko katika maisha haya,+
Wale ambao unawajaza kwa vitu vizuri unavyoandaa+
Na ambao huwaachia urithi wana wao wengi.