Zaburi
3 Wanasema: “Na tuzikate pingu zao
Na kuzitupa kamba zao!”
4 Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni atacheka;
Yehova atawadhihaki.
5 Wakati huo ataongea nao kwa hasira yake
Na kuwatisha kwa hasira yake inayowaka,
6 Akisema: “Mimi mwenyewe nimemweka mfalme wangu+
Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”
8 Niombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako
Na miisho ya dunia kuwa miliki yako.+
10 Basi sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;
Kubalini kurekebishwa,* enyi waamuzi wa dunia.
11 Mtumikieni Yehova kwa woga,
Na mshangilie mkitetemeka.
12 Mheshimuni* mwana,+ la sivyo Mungu atawaka hasira
Nanyi mtaangamia kutoka njiani,+
Kwa maana hasira Yake huwaka upesi.
Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.