-
Mwanzo 1:29Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
29 Kisha Mungu akasema: “Tazama nimewapa kila mmea duniani pote unaozaa mbegu na kila mti unaozaa matunda yenye mbegu. Itakuwa chakula chenu.+
-
-
Zaburi 144:3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,
Mwana wa mtu anayeweza kufa ni nini hata umkazie uangalifu?+
-
-
Waebrania 2:6-8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Lakini mahali fulani shahidi mmoja alisema: “Mwanadamu ni nini hivi kwamba unamweka akilini, au mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+ 7 Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko malaika; ulimvika taji kwa utukufu na heshima, na kumweka juu ya kazi za mikono yako. 8 Ulivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Kwa kuvitiisha vitu vyote chini yake,+ Mungu hakuacha kitu chochote kisichotiishwa chini yake.+ Ingawa hivyo, bado hatuoni vitu vyote vikiwa vimetiishwa chini yake.+
-