Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Yeremia ahuzunika sana (1-3a)

      • Yehova aiadhibu Yuda (3b-16)

      • Nchi ya Yuda yaombolezewa (17-22)

      • Jigambe kuhusu kumjua Yehova (23-26)

Yeremia 9:1

Marejeo

  • +Isa 22:4; Yer 13:17

Yeremia 9:2

Marejeo

  • +Yer 5:7; 23:10

Yeremia 9:3

Marejeo

  • +Isa 59:3
  • +Yer 4:22

Yeremia 9:4

Marejeo

  • +Yer 12:6; Mik 7:2, 5
  • +Yer 6:28; Eze 22:9

Yeremia 9:5

Marejeo

  • +Zb 50:19; Mik 6:12

Yeremia 9:7

Marejeo

  • +Isa 1:25; 48:10

Yeremia 9:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yangu haipaswi.”

Marejeo

  • +Yer 5:9, 29

Yeremia 9:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wimbo wa maombolezo.”

Marejeo

  • +Yer 4:25; Sef 1:3

Yeremia 9:11

Marejeo

  • +Zb 79:1; Yer 26:18
  • +Yer 10:22
  • +Yer 4:27; 25:11; 32:43

Yeremia 9:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wameyakataa mafundisho.”

Yeremia 9:14

Marejeo

  • +Yer 7:24
  • +Amu 3:7; 1Sa 12:10; Ho. 11:2

Yeremia 9:15

Marejeo

  • +Yer 8:14; 23:15; Omb 3:15, 19

Yeremia 9:16

Marejeo

  • +Law 26:33; Kum 28:64; Zb 106:27; Zek 7:14
  • +Yer 29:17; Eze 5:2

Yeremia 9:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nyimbo za maombolezo.”

Marejeo

  • +2Nya 35:25

Yeremia 9:18

Marejeo

  • +Yer 6:26; 14:17

Yeremia 9:19

Marejeo

  • +Yer 4:31; Eze 7:16; Mik 1:8, 9
  • +Omb 4:15; Mik 2:10

Yeremia 9:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wimbo huu wa maombolezo.”

Marejeo

  • +Isa 29:2; Yer 7:29

Yeremia 9:21

Marejeo

  • +2Nya 36:17; Yer 6:11

Yeremia 9:22

Marejeo

  • +Isa 5:25; Yer 16:3, 4

Yeremia 9:23

Marejeo

  • +Isa 5:21
  • +Kum 8:12-14, 17, 18

Yeremia 9:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayejisifu na ajisifu.”

Marejeo

  • +1Ko 1:31; 2Ko 10:17
  • +Kut 34:6; Zb 89:14
  • +Zb 99:4; Ho. 6:6; Mik 6:8; 7:18

Yeremia 9:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitamfanya awajibike.”

Marejeo

  • +Amo 3:1, 2

Yeremia 9:26

Marejeo

  • +Isa 19:1; Eze 29:2
  • +Isa 1:1
  • +Yer 27:2, 3; Eze 32:29; Oba 1
  • +Yer 49:1; Eze 25:2
  • +Isa 15:1; Yer 48:1
  • +Yer 25:17, 23; 49:32
  • +Law 26:41; Yer 4:4

Jumla

Yer. 9:1Isa 22:4; Yer 13:17
Yer. 9:2Yer 5:7; 23:10
Yer. 9:3Isa 59:3
Yer. 9:3Yer 4:22
Yer. 9:4Yer 12:6; Mik 7:2, 5
Yer. 9:4Yer 6:28; Eze 22:9
Yer. 9:5Zb 50:19; Mik 6:12
Yer. 9:7Isa 1:25; 48:10
Yer. 9:9Yer 5:9, 29
Yer. 9:10Yer 4:25; Sef 1:3
Yer. 9:11Zb 79:1; Yer 26:18
Yer. 9:11Yer 10:22
Yer. 9:11Yer 4:27; 25:11; 32:43
Yer. 9:14Yer 7:24
Yer. 9:14Amu 3:7; 1Sa 12:10; Ho. 11:2
Yer. 9:15Yer 8:14; 23:15; Omb 3:15, 19
Yer. 9:16Law 26:33; Kum 28:64; Zb 106:27; Zek 7:14
Yer. 9:16Yer 29:17; Eze 5:2
Yer. 9:172Nya 35:25
Yer. 9:18Yer 6:26; 14:17
Yer. 9:19Yer 4:31; Eze 7:16; Mik 1:8, 9
Yer. 9:19Omb 4:15; Mik 2:10
Yer. 9:20Isa 29:2; Yer 7:29
Yer. 9:212Nya 36:17; Yer 6:11
Yer. 9:22Isa 5:25; Yer 16:3, 4
Yer. 9:23Isa 5:21
Yer. 9:23Kum 8:12-14, 17, 18
Yer. 9:241Ko 1:31; 2Ko 10:17
Yer. 9:24Kut 34:6; Zb 89:14
Yer. 9:24Zb 99:4; Ho. 6:6; Mik 6:8; 7:18
Yer. 9:25Amo 3:1, 2
Yer. 9:26Isa 19:1; Eze 29:2
Yer. 9:26Isa 1:1
Yer. 9:26Yer 27:2, 3; Eze 32:29; Oba 1
Yer. 9:26Yer 49:1; Eze 25:2
Yer. 9:26Isa 15:1; Yer 48:1
Yer. 9:26Yer 25:17, 23; 49:32
Yer. 9:26Law 26:41; Yer 4:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 9:1-26

Yeremia

9 Laiti kichwa changu kingekuwa maji,

Na macho yangu chemchemi ya machozi!+

Ndipo ningelia usiku na mchana

Kwa ajili ya watu wangu waliouawa.

 2 Laiti ningepata mahali ambapo wasafiri hulala nyikani!

Ndipo ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao,

Kwa maana wote ni wazinzi,+

Kundi la watu wenye hila.

 3 Wanaupinda ulimi wao kama upinde;

Uwongo, badala ya uaminifu, umeenea nchini.+

“Wanatoka uovu hadi uovu zaidi,

Nao hawanisikilizi,”+ asema Yehova.

 4 “Kila mtu, jihadhari na jirani yako,

Wala usimwamini hata ndugu yako.

Kwa maana kila ndugu ni msaliti,+

Na kila jirani ni mchongezi.+

 5 Kila mtu anamdanganya jirani yake,

Na hakuna yeyote anayesema ukweli.

Wameufundisha ulimi wao kusema uwongo.+

Wanajichosha kwa kufanya makosa.

 6 Unaishi katikati ya udanganyifu.

Katika udanganyifu wao walikataa kunijua mimi,” asema Yehova.

 7 Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Nitawayeyusha na kuwajaribu,+

Kwa maana ni nini kingine ninachoweza kumtendea binti ya watu wangu?

 8 Ulimi wao ni mshale unaoua na kusema udanganyifu.

Kwa kinywa chake mtu anazungumza na jirani yake kuhusu amani,

Lakini ndani anamvizia.”

 9 “Je, sipaswi kuwafanya wawajibike kwa sababu ya mambo haya?” asema Yehova.

“Je, sipaswi* kujilipizia kisasi dhidi ya taifa kama hili?+

10 Nitalia na kuiombolezea milima

Na kuimba wimbo wa huzuni* kwa ajili ya malisho ya nyikani,

Kwa maana yameteketezwa hivi kwamba hakuna mwanadamu anayepita humo,

Na sauti ya mifugo haisikiwi.

Ndege wa angani na wanyama wamekimbia; wametoweka.+

11 Nitalifanya Yerusalemu kuwa rundo la mawe,+ mapango ya mbwamwitu,+

Nami nitayafanya majiji ya Yuda yawe ukiwa, bila mkaaji.+

12 Ni nani mwenye hekima ya kutosha kuelewa jambo hili?

Kinywa cha Yehova kimezungumza na nani, ili atangaze jambo hilo?

Kwa nini nchi imeangamia?

Kwa nini imeteketezwa kama nyika,

Hivi kwamba hakuna mtu anayepita humo?”

13 Yehova akajibu: “Kwa sababu wameikataa sheria* yangu niliyowapa, na kwa sababu hawajaifuata na kutii sauti yangu. 14 Badala yake, walifuata kwa ukaidi mioyo yao wenyewe,+ na kuzifuata sanamu za Baali, kama baba zao walivyowafundisha kufanya.+ 15 Kwa hiyo, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Tazama, ninawafanya watu hawa wale pakanga, nami nitawafanya wanywe maji yenye sumu.+ 16 Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao na baba zao hawajayajua,+ nami nitatuma upanga uwafuate mpaka nitakapowaangamiza kabisa.’+

17 Yehova wa majeshi anasema hivi:

‘Tendeni kwa uelewaji.

Waiteni wanawake wanaoimba nyimbo za huzuni,*+

Nanyi waiteni wanawake stadi waje,

18 Ili waje haraka na kutuombolezea,

Ili macho yetu yabubujike machozi

Na kope zetu zitiririke maji.+

19 Kwa maana sauti ya maombolezo imesikika kutoka Sayuni:+

“Jinsi tulivyoangamizwa!

Jinsi aibu yetu ilivyo nyingi!

Kwa maana tumeiacha nchi, nao wamezibomoa nyumba zetu.”+

20 Enyi wanawake, sikieni neno la Yehova.

Sikio lenu na lipokee neno la kinywa chake.

Wafundisheni mabinti wenu maombolezo haya,

Na mfundishane wimbo huu wa huzuni.*+

21 Kwa maana kifo kimeingia kupitia madirisha yetu;

Kimeingia ndani ya minara yetu yenye ngome

Ili kuwaondoa watoto barabarani

Na vijana kwenye viwanja vya jiji.’+

22 Sema, ‘Yehova anasema hivi:

“Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya ardhi shambani,

Kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa na mvunaji,

Bila mtu wa kuikusanya.”’”+

23 Yehova anasema hivi:

“Mtu mwenye hekima asijigambe kwa sababu ya hekima yake;+

Mtu mwenye nguvu asijigambe kwa sababu ya nguvu zake;

Na tajiri asijigambe kwa sababu ya utajiri wake.”+

24 “Lakini yule anayejigamba na ajigambe* kwa jambo hili:

Kwamba ana ufahamu na ujuzi kunihusu,+

Kwamba mimi ni Yehova, Ninayetenda kwa upendo mshikamanifu, haki, na uadilifu duniani,+

Kwa maana ninapendezwa na mambo hayo,”+ asema Yehova.

25 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamwadhibu* kila mtu aliyetahiriwa lakini bado hajatahiriwa,+ 26 yaani, Misri+ na Yuda+ na Edomu+ na Waamoni+ na Moabu+ na wale wote wanaonyoa nywele pembeni mwa vichwa vyao ambao wanakaa nyikani;+ kwa maana mataifa yote hayajatahiriwa, na watu wote wa nyumba ya Israeli hawajatahiriwa moyoni.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki