Zaburi
104 Nafsi yangu na imsifu Yehova.+
Ee Yehova Mungu wangu, wewe ni mkuu sana.+
3 Hujenga boriti za vyumba vyake vya juu katika maji yaliyo juu,*+
Akiyafanya mawingu kuwa gari lake,+
Akienda juu ya mabawa ya upepo.+
4 Huwafanya malaika wake kuwa roho,
Wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza kabisa.+
6 Uliifunika kwa vilindi vya maji kama kwa vazi.+
Maji yalisimama juu ya milima.
7 Kwa kemeo lako yalikimbia;+
Kwa sauti ya mngurumo wako yalikimbia kwa wasiwasi
8 —Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka—
Mahali ulipokusudia yawepo.
9 Uliweka mpaka ambao hayapaswi kuvuka,+
Ili yasiifunike dunia tena kamwe.
10 Wewe hupeleka chemchemi katika mabonde;*
Kati ya milima zinatiririka.
11 Zinawapa maji wanyama wote wa mwituni;
Punda mwitu hukata kiu yake.
12 Juu yake ndege wa angani hukaa;
Wanaimba katikati ya majani mengi.
13 Anainywesha milima maji kutoka katika vyumba vyake vya juu.+
Dunia hushibishwa kwa matunda ya kazi zako.+
14 Anaotesha majani kwa ajili ya ng’ombe
Na mimea kwa ajili ya matumizi ya wanadamu,+
Ili chakula kikue ardhini
15 Na divai inayofanya moyo wa mwanadamu ushangilie,+
Mafuta yanayofanya uso ung’ae,
Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+
16 Miti ya Yehova imetosheka,
Mierezi ya Lebanoni aliyopanda,
17 Ambamo ndege hutengeneza viota.
Makao ya korongo+ ni miberoshi.
19 Ameuumba mwezi ili upime nyakati zilizowekwa;
Jua linajua vizuri wakati wa kutua.+
20 Wewe unaleta giza, usiku unaingia,+
Wakati ambapo wanyama wote wa mwituni wanazunguka-zunguka.
22 Jua linapochomoza,
Wanarudi na kulala katika mapango yao.
23 Mwanadamu huenda kwenye kazi yake,
Naye hufanya kazi kwa jasho mpaka jioni.
24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana, Ee Yehova!+
Umezifanya zote kwa hekima.+
Dunia imejaa vitu ulivyoumba.
25 Kisha kuna bahari, ni kubwa sana na pana,
Imejaa viumbe walio hai wasio na idadi, wadogo kwa wakubwa.+
27 Wote wanakungojea wewe
Uwape chakula chao kwa wakati wake.+
28 Wanakusanya unachowapa.+
Unapofumbua mkono wako, wanashiba vitu vyema.+
29 Ukiuficha uso wako, wanahangaika.
Ukiiondoa roho yao, wanakufa na kurudi mavumbini.+
30 Ukiituma roho yako, wanaumbwa,+
Nawe unaifanya ardhi iwe na sura mpya.
31 Utukufu wa Yehova utadumu milele.
Yehova atashangilia kwa sababu ya kazi zake.+
32 Huitazama dunia, inatetemeka;
Huigusa milima, inafuka moshi.+
34 Mawazo yangu na yampendeze.*
Nitashangilia kwa sababu ya Yehova.
35 Watenda dhambi watatoweka duniani,
Na waovu hawatakuwapo tena.+
Nafsi yangu na imsifu Yehova. Msifuni Yah!*