Ayubu
37 “Kwa sababu hiyo moyo wangu hupigapiga
Na kuruka kutoka mahali pake.
2 Sikiliza kwa makini mrindimo wa sauti yake
Na mngurumo unaotoka kinywani mwake.
3 Huuachilia kwa ghafla chini ya mbingu zote
Na kuituma radi yake+ mpaka kwenye miisho ya dunia.
4 Kisha sauti ya mngurumo husikika;
Hunguruma kwa sauti yenye fahari,+
Naye haizuii radi sauti yake inaposikiwa.
5 Mungu hunguruma kwa sauti yake+ kwa njia inayostaajabisha;
Hufanya mambo makuu ambayo hatuwezi kuelewa.+
7 Mungu husimamisha shughuli zote za wanadamu*
Ili kila mwanadamu anayeweza kufa ajue kazi Yake.
8 Wanyama wa mwituni huingia katika mapango yao
Na kubaki katika makao yao.
11 Naam, huyalemea mawingu kwa mvuke;
Hutawanya radi yake+ mawinguni;
12 Huzunguka-zunguka anakoyaelekeza;
13 Iwe ni adhabu*+ au kwa ajili ya nchi
Au kwa ajili ya upendo mshikamanifu, yeye husababisha yatendeke.+
14 Sikiliza hili, Ayubu;
Tulia na utafakari kwa makini kazi za Mungu zinazostaajabisha.+
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza* mawingu
Na jinsi anavyosababisha radi imweke kutoka katika mawingu yake?
16 Je, unajua jinsi mawingu yanavyoelea?+
Hizi ni kazi zinazostaajabisha za Yule ambaye ni mkamilifu katika ujuzi.+
17 Kwa nini mavazi yako yanapata joto
Wakati dunia imetulia kwa sababu ya upepo wa kusini?+
19 Tuambie tunalopaswa kumwambia;
Hatuwezi kumjibu kwa sababu tuko gizani.
20 Je, anapaswa kuambiwa kwamba ninataka kuzungumza?
Au kuna yeyote ambaye amesema jambo ambalo lazima ajulishwe?+
21 Hata hawawezi kuona nuru,*
Ingawa inang’aa angani,
Mpaka upepo unapopita na kuondoa kabisa mawingu.
22 Fahari inayong’aa kama dhahabu hutoka kaskazini;
Utukufu wa Mungu+ unaogopesha.
24 Kwa hiyo watu wanapaswa kumwogopa.+
Kwa sababu yeye hampendi yeyote anayefikiri ana hekima.”+