Methali
2 Mtu mwema hupata kibali cha Yehova,
Lakini Yeye humhukumu mtu anayepanga njama za uovu.+
3 Hakuna mtu anayekuwa salama kwa kutenda uovu,+
Lakini waadilifu hawatang’olewa kamwe.
4 Mke mwema* ni taji kwa mume wake,+
Lakini mke anayetenda kwa aibu ni kama uozo katika mifupa ya mume wake.+
5 Mawazo ya waadilifu ni ya haki,
Lakini mwongozo wa waovu hudanganya.
7 Waovu wanapoangamizwa, hawako tena,
Lakini nyumba ya mwadilifu itaendelea kusimama.+
8 Mtu husifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+
Lakini mtu aliye na moyo uliopotoka atatendewa kwa dharau.+
9 Ni afadhali usiheshimiwe sana lakini uwe na mtumishi
11 Anayelima shamba lake atakuwa na chakula tele,+
Lakini anayefuatia vitu visivyo na maana hana busara.*
12 Mtu mwovu hutamani kitu kilichokamatwa na watu wengine waovu,
Lakini mzizi wa waadilifu huzaa matunda.
13 Mwovu hunaswa na mazungumzo yake ya dhambi,+
Lakini mwadilifu huokoka kutoka katika taabu.
17 Anayetoa ushahidi kwa uaminifu atasema ukweli,*
Lakini shahidi wa uwongo husema mambo ya udanganyifu.
18 Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga,
Lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.+
20 Udanganyifu umo moyoni mwa wale wanaopanga njama zinazodhuru,
22 Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova,+
Lakini wanaotenda kwa uaminifu humfurahisha.
23 Mtu mwerevu hufunika mambo anayojua,
Lakini moyo wa mjinga hububujika ujinga.+
26 Mwadilifu hutafuta malisho yake,
Lakini njia ya waovu huwapotosha.
27 Watu wavivu hawakimbizi mawindo,+
Lakini bidii ni hazina ya mtu yenye thamani.
28 Kijia cha uadilifu huongoza kwenye uzima;+
Kando ya kijia hicho hakuna kifo.