Methali
3 Mwanangu, usisahau mafundisho* yangu,
Na moyo wako ushike amri zangu,
2 Kwa sababu zitakuongezea siku nyingi
Na miaka ya uhai na amani.+
3 Usiruhusu upendo mshikamanifu na uaminifu* zikuache.+
Zifunge shingoni mwako;
Ziandike kwenye kibao cha moyo wako;+
4 Ndipo utakapopata kibali na ufahamu mzuri
Machoni pa Mungu na wanadamu.+
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.+
Mwogope Yehova na ujiepushe na uovu.
8 Hilo litaponya mwili wako*
Na kuiburudisha mifupa yako.
9 Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani,+
Kwa mavuno ya kwanza ya* mazao* yako yote;+
10 Ndipo maghala yako yatakapojazwa kabisa,+
Na mitungi yako itafurika* divai mpya.
11 Mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova,+
Wala usichukie karipio lake,+
12 Kwa maana Yehova huwakaripia wale anaowapenda,+
Kama baba anavyomkaripia mwana anayempenda.+
13 Mwenye furaha ni mtu anayepata hekima+
Na mtu anayepata utambuzi;
14 Kupata hekima ni bora kuliko kupata fedha,
Na kuipata kama faida ni bora kuliko kupata dhahabu.+
15 Ni yenye thamani kuliko marijani;*
Hakuna chochote unachotamani kinachoweza kulinganishwa nayo.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kulia;
Na katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na utukufu.
17 Njia zake zinapendeza,
Na vijia vyake vyote vina amani.+
18 Ni mti wa uzima kwa wale wanaoishika,
Na wale wanaoishika kwa nguvu wataitwa wenye furaha.+
19 Yehova aliuweka msingi wa dunia kwa hekima.+
Aliziimarisha kabisa mbingu kwa utambuzi.+
20 Kwa ujuzi wake vilindi vya maji vilitenganishwa
Na anga zenye mawingu zilidondosha umande.+
21 Mwanangu, zisiondoke machoni pako.*
Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri;
22 Zitakupa uzima
Na kuwa pambo shingoni mwako;
23 Ndipo utakapotembea kwa usalama katika njia yako,
28 Usimwambie jirani yako, “Nenda; rudi baadaye! Nitakupa kesho,”
Ikiwa unaweza kumpa kitu hicho sasa.
29 Usipange kumdhuru jirani yako+
Anayejihisi akiwa salama mkiwa pamoja.
31 Usimwonee wivu mtu mkatili+
Wala kuchagua yoyote kati ya njia zake,
32 Kwa maana Yehova humchukia mtu mwenye hila,+
Lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.+
35 Wenye hekima watarithi heshima,
Lakini wapumbavu hutukuza aibu.+