Zaburi
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mtindo wa Mahalathi,* uimbwe kwa zamu. Maskili* ya Hemani+ Mwezra.
88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+
Wakati wa mchana ninalia kwa sauti,
Na usiku ninakuja mbele zako.+
4 Tayari nimehesabiwa miongoni mwa wale wanaoshuka shimoni;*+
Nimekuwa mtu asiye na uwezo wowote,*+
5 Aliyeachwa kati ya watu waliokufa
Kama waliouawa wanaolala kaburini,
Ambao huwakumbuki tena
Na ambao wametengwa mbali na utunzaji* wako.
6 Umeniweka katika shimo lenye kina kirefu sana,
Sehemu zenye giza, shimo kubwa.*
7 Ghadhabu yako inanilemea sana,+
Nawe unanilemea kwa mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)
8 Umewafukuza rafiki zangu mbali sana nami;+
Umenifanya niwe kitu kinachowachukiza.
Nimenaswa na siwezi kutoroka.
9 Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+
Ee Yehova, ninakulilia mchana kutwa;+
Ninakunyooshea mikono yangu.
10 Je, utawatendea maajabu waliokufa?
Je, wale waliokufa ambao hawana uwezo wanaweza kuinuka na kukusifu?+ (Sela)
11 Je, upendo wako mshikamanifu utatangazwa kaburini,
Na uaminifu wako mahali pa maangamizi?*
12 Je, maajabu yako yatajulikana gizani
Au uadilifu wako katika nchi ya waliosahauliwa?+
14 Kwa nini, Ee Yehova, unanikataa?*+
Kwa nini unanificha uso wako?+
15 Tangu nilipokuwa kijana,
Nimeteseka nami niko karibu kuangamia;+
Nimekufa ganzi kwa sababu ya mambo yanayotisha unayoruhusu yanipate.
16 Hasira yako inayowaka inanilemea;+
Vitisho vyako vinaniangamiza.
17 Vinanizunguka mchana kutwa kama maji;
Vinanizingira ili kunibana pande zote.*
18 Umewafukuza rafiki zangu na wenzangu mbali sana nami;+
Giza limekuwa mwenzangu.