Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nehemia 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Nehemia—Yaliyomo

      • Watu waungama dhambi zao (1-38)

        • Yehova, Mungu anayesamehe (17)

Nehemia 9:1

Marejeo

  • +Yos 7:6; Yon 3:5, 6

Nehemia 9:2

Marejeo

  • +Ezr 9:1, 2; Ne 13:3
  • +Law 26:40; Ezr 9:6; Zb 106:6; Da 9:8

Nehemia 9:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa saa tatu.”

Marejeo

  • +Ne 8:3, 8

Nehemia 9:4

Marejeo

  • +Ne 8:7
  • +Ne 8:4

Nehemia 9:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “milele hata milele.”

Marejeo

  • +Yer 33:10, 11

Nehemia 9:6

Marejeo

  • +Kum 6:4

Nehemia 9:7

Marejeo

  • +Mwa 12:1, 2
  • +Mwa 11:31
  • +Mwa 17:5

Nehemia 9:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu yake.”

Marejeo

  • +Mwa 22:10-12
  • +Mwa 15:18

Nehemia 9:9

Marejeo

  • +Kut 2:23-25; 3:7

Nehemia 9:10

Marejeo

  • +Kut 7:3; Kum 6:22
  • +Kut 5:2
  • +Kut 9:16

Nehemia 9:11

Marejeo

  • +Kut 14:21, 22
  • +Kut 15:1, 5, 10

Nehemia 9:12

Marejeo

  • +Kut 13:21; 14:19, 20

Nehemia 9:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sheria zinazotegemeka.”

Marejeo

  • +Kut 19:11
  • +Kum 4:10, 36
  • +Kum 4:8

Nehemia 9:14

Marejeo

  • +Kut 16:29; 20:8-11; Kum 5:12-14

Nehemia 9:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “uliinua mkono wako.”

Marejeo

  • +Kut 16:4
  • +Kut 17:6

Nehemia 9:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “na kufanya shingo yao kuwa ngumu.”

Marejeo

  • +Hes 14:44
  • +Kum 9:6

Nehemia 9:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakafanya shingo yao kuwa ngumu.”

  • *

    Au “Mungu mwenye matendo ya kusamehe.”

  • *

    Au “neema.”

  • *

    Au “fadhili nyingi zenye upendo.”

Marejeo

  • +Hes 14:11, 41
  • +Hes 14:1, 4
  • +Kut 34:6; Hes 14:18
  • +Kum 4:31

Nehemia 9:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Marejeo

  • +Kut 32:1, 4

Nehemia 9:19

Marejeo

  • +Hes 14:19, 20
  • +Kut 40:38; Hes 9:15

Nehemia 9:20

Marejeo

  • +Hes 11:17, 25
  • +Kut 16:14, 15
  • +Hes 20:8

Nehemia 9:21

Marejeo

  • +Kut 16:35; Hes 14:33; Kum 2:7
  • +Kum 29:5

Nehemia 9:22

Marejeo

  • +Yos 11:23
  • +Hes 21:23, 24; Kum 2:31
  • +Hes 21:26
  • +Hes 21:33, 35

Nehemia 9:23

Marejeo

  • +Mwa 15:1, 5
  • +Mwa 12:7; 26:3

Nehemia 9:24

Marejeo

  • +Hes 14:29-31; Yos 21:43
  • +Yos 18:1

Nehemia 9:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “iliyonona.”

Marejeo

  • +Kum 3:4, 5
  • +Kum 8:7-9
  • +Yos 24:13

Nehemia 9:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuitupa Sheria yako nyuma yao.”

Marejeo

  • +Kum 31:20; 32:15; Amu 2:12
  • +2Fa 21:11; Zb 106:38

Nehemia 9:27

Marejeo

  • +Amu 2:14
  • +Kum 31:17
  • +Amu 2:18; 3:9, 15; 1Sa 12:11; 2Fa 13:4, 5

Nehemia 9:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “waliwaponda.”

Marejeo

  • +Amu 2:19
  • +Amu 4:1, 2; 6:1
  • +Amu 6:6
  • +Zb 106:43-45

Nehemia 9:29

Marejeo

  • +2Fa 17:13, 14; 2Nya 24:19
  • +Law 18:5

Nehemia 9:30

Marejeo

  • +Ro 10:21
  • +2Nya 36:15, 16; Isa 42:24; Yer 40:2, 3

Nehemia 9:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “neema.”

Marejeo

  • +Eze 14:22
  • +Kut 34:6; Kum 4:31

Nehemia 9:32

Marejeo

  • +Kum 7:9; Da 9:4
  • +2Fa 24:12, 14
  • +Yer 34:18-20
  • +Omb 4:13, 14
  • +2Fa 17:6

Nehemia 9:33

Marejeo

  • +Da 9:5

Nehemia 9:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “maonyo uliyowapa.”

Nehemia 9:35

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “iliyonona.”

Marejeo

  • +Kum 28:47; 32:15

Nehemia 9:36

Marejeo

  • +Kum 28:48; Ezr 9:9

Nehemia 9:37

Marejeo

  • +Kum 28:15, 33; Ne 5:4

Nehemia 9:38

Marejeo

  • +2Fa 23:3; 2Nya 15:12; Ezr 10:3
  • +Ne 10:28, 29

Jumla

Neh. 9:1Yos 7:6; Yon 3:5, 6
Neh. 9:2Ezr 9:1, 2; Ne 13:3
Neh. 9:2Law 26:40; Ezr 9:6; Zb 106:6; Da 9:8
Neh. 9:3Ne 8:3, 8
Neh. 9:4Ne 8:7
Neh. 9:4Ne 8:4
Neh. 9:5Yer 33:10, 11
Neh. 9:6Kum 6:4
Neh. 9:7Mwa 12:1, 2
Neh. 9:7Mwa 11:31
Neh. 9:7Mwa 17:5
Neh. 9:8Mwa 22:10-12
Neh. 9:8Mwa 15:18
Neh. 9:9Kut 2:23-25; 3:7
Neh. 9:10Kut 7:3; Kum 6:22
Neh. 9:10Kut 5:2
Neh. 9:10Kut 9:16
Neh. 9:11Kut 14:21, 22
Neh. 9:11Kut 15:1, 5, 10
Neh. 9:12Kut 13:21; 14:19, 20
Neh. 9:13Kut 19:11
Neh. 9:13Kum 4:10, 36
Neh. 9:13Kum 4:8
Neh. 9:14Kut 16:29; 20:8-11; Kum 5:12-14
Neh. 9:15Kut 16:4
Neh. 9:15Kut 17:6
Neh. 9:16Hes 14:44
Neh. 9:16Kum 9:6
Neh. 9:17Hes 14:11, 41
Neh. 9:17Hes 14:1, 4
Neh. 9:17Kut 34:6; Hes 14:18
Neh. 9:17Kum 4:31
Neh. 9:18Kut 32:1, 4
Neh. 9:19Hes 14:19, 20
Neh. 9:19Kut 40:38; Hes 9:15
Neh. 9:20Hes 11:17, 25
Neh. 9:20Kut 16:14, 15
Neh. 9:20Hes 20:8
Neh. 9:21Kut 16:35; Hes 14:33; Kum 2:7
Neh. 9:21Kum 29:5
Neh. 9:22Yos 11:23
Neh. 9:22Hes 21:23, 24; Kum 2:31
Neh. 9:22Hes 21:26
Neh. 9:22Hes 21:33, 35
Neh. 9:23Mwa 15:1, 5
Neh. 9:23Mwa 12:7; 26:3
Neh. 9:24Hes 14:29-31; Yos 21:43
Neh. 9:24Yos 18:1
Neh. 9:25Kum 3:4, 5
Neh. 9:25Kum 8:7-9
Neh. 9:25Yos 24:13
Neh. 9:26Kum 31:20; 32:15; Amu 2:12
Neh. 9:262Fa 21:11; Zb 106:38
Neh. 9:27Amu 2:14
Neh. 9:27Kum 31:17
Neh. 9:27Amu 2:18; 3:9, 15; 1Sa 12:11; 2Fa 13:4, 5
Neh. 9:28Amu 2:19
Neh. 9:28Amu 4:1, 2; 6:1
Neh. 9:28Amu 6:6
Neh. 9:28Zb 106:43-45
Neh. 9:292Fa 17:13, 14; 2Nya 24:19
Neh. 9:29Law 18:5
Neh. 9:30Ro 10:21
Neh. 9:302Nya 36:15, 16; Isa 42:24; Yer 40:2, 3
Neh. 9:31Eze 14:22
Neh. 9:31Kut 34:6; Kum 4:31
Neh. 9:32Kum 7:9; Da 9:4
Neh. 9:322Fa 24:12, 14
Neh. 9:32Yer 34:18-20
Neh. 9:32Omb 4:13, 14
Neh. 9:322Fa 17:6
Neh. 9:33Da 9:5
Neh. 9:35Kum 28:47; 32:15
Neh. 9:36Kum 28:48; Ezr 9:9
Neh. 9:37Kum 28:15, 33; Ne 5:4
Neh. 9:382Fa 23:3; 2Nya 15:12; Ezr 10:3
Neh. 9:38Ne 10:28, 29
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Nehemia 9:1-38

Nehemia

9 Siku ya 24 ya mwezi huo, Waisraeli wakakusanyika; walikuwa wamefunga wakiwa wamevaa nguo za magunia na kujirushia mavumbi.+ 2 Kisha wazao wa Waisraeli wakajitenga na wageni wote,+ wakasimama na kuungama dhambi zao wenyewe na makosa ya baba zao.+ 3 Kisha wakasimama mahali walipokuwa na kusoma kwa sauti kitabu cha Sheria+ ya Yehova Mungu wao kwa robo siku;* na kwa robo nyingine ya siku walikuwa wakiungama na kumwinamia Yehova Mungu wao.

4 Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia,+ Bani, na Kenani wakasimama kwenye jukwaa+ la Walawi na kumlilia Yehova Mungu wao kwa sauti kubwa. 5 Nao Walawi, yaani, Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabneya, Sherebia, Hodia, Shebania, na Pethahia wakasema: “Simameni, msifuni Yehova Mungu wenu kwa umilele wote.*+ Na walisifu jina lako tukufu, ambalo limekwezwa juu kuliko baraka zote na sifa zote.

6 “Wewe peke yako ndiye Yehova;+ uliumba mbingu, naam, mbingu za mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vilivyo juu yake, bahari na vyote vilivyomo. Nawe unavihifadhi vyote hai, na jeshi la mbinguni linakuinamia wewe. 7 Wewe ndiye Yehova Mungu wa kweli, uliyemchagua Abramu,+ ukamtoa katika jiji la Uru+ la Wakaldayo na ukampa jina Abrahamu.+ 8 Nawe ukaona moyo wake ukiwa mwaminifu mbele zako;+ basi ukafanya agano naye ili umpe nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi, na Wagirgashi, ili kuupa uzao wake* nchi hiyo;+ nawe ukatimiza ahadi zako, kwa maana wewe ni mwadilifu.

9 “Basi ukaona mateso ya mababu zetu huko Misri,+ nawe ukasikia kilio chao kwenye Bahari Nyekundu. 10 Kisha ukafanya ishara na miujiza dhidi ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua waliwatendea kwa kimbelembele.+ Ukajijengea jina ambalo limedumu hadi leo hii.+ 11 Nawe ukaitenganisha bahari mbele yao, wakavuka bahari juu ya nchi kavu,+ na wale waliowafuatia ukawatupa ndani ya maji mengi kama vile jiwe linavyotupwa ndani ya bahari iliyochafuka.+ 12 Uliwaongoza mchana kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto, ili kuwaangazia njia waliyopaswa kupitia.+ 13 Nawe ukashuka kwenye Mlima Sinai+ ukazungumza nao kutoka mbinguni+ na kuwapa hukumu za uadilifu, sheria za kweli,* masharti bora na amri bora.+ 14 Ukawajulisha Sabato yako takatifu+ na kuwapa amri, masharti, na sheria kupitia Musa mtumishi wako. 15 Walipokuwa na njaa uliwapa mkate kutoka mbinguni,+ walipokuwa na kiu ukawapa maji kutoka kwenye mwamba,+ na ukawaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa* kwamba utawapatia.

16 “Lakini mababu zetu, wakatenda kwa kimbelembele+ na kuwa wakaidi,*+ nao hawakusikiliza amri zako. 17 Walikataa kusikiliza+ wala hawakukumbuka matendo yako ya ajabu uliyofanya miongoni mwao, lakini wakawa wakaidi,* nao wakachagua kiongozi ili warudi Misri ambako walikuwa watumwa.+ Lakini wewe ni Mungu uliye tayari kusamehe,* mwenye huruma* na rehema, usiye mwepesi wa hasira, una upendo mwingi mshikamanifu,*+ nawe hukuwaacha.+ 18 Hata walipojitengenezea sanamu ya ndama wa chuma* na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wenu aliyewaongoza kutoka Misri,’+ nao wakatenda matendo makubwa ya ukosefu wa heshima, 19 hata wakati huo, kwa rehema zako nyingi, hukuwaacha nyikani.+ Nguzo ya wingu iliyowaongoza njiani mchana haikuondoka juu yao, wala nguzo ya moto iliyowaangazia njia usiku.+ 20 Nawe ukawapa roho yako njema ili iwape ufahamu,+ hukuwanyima mana vinywani mwao,+ na walipohisi kiu ukawapa maji.+ 21 Kwa miaka 40 uliwapa chakula nyikani.+ Hawakukosa chochote. Mavazi yao hayakuchakaa,+ wala miguu yao haikuvimba.

22 “Uliwapa falme na mataifa, ukawagawia kipande kwa kipande,+ nao wakamiliki nchi ya Sihoni,+ yaani, nchi ya mfalme wa Heshboni,+ na pia nchi ya Ogu+ mfalme wa Bashani. 23 Nawe ukawafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ Kisha ukawaleta katika nchi ambayo ulikuwa umewaahidi mababu zao kwamba wanapaswa kuingia na kuimiliki.+ 24 Basi wana wao wakaingia na kuimiliki nchi hiyo,+ nawe ukawatiisha Wakanaani walioishi katika nchi hiyo,+ ukawatia mikononi mwao, wao pamoja na wafalme wao na wakaaji wa nchi, ili wawatendee wapendavyo. 25 Wakateka majiji yenye ngome+ na ardhi yenye rutuba,*+ wakamiliki nyumba zilizojaa vitu vyema vya kila aina, visima ambavyo tayari vilikuwa vimechimbwa, mashamba ya mizabibu, mizeituni,+ na miti ya matunda kwa wingi. Hivyo wakala na kushiba na kunenepa, nao wakaufurahia wema wako mwingi.

26 “Hata hivyo, hawakutii, bali walikuasi+ na kuigeuzia mgongo Sheria yako.* Wakawaua manabii wako waliowaonya wakurudie, nao wakatenda matendo makubwa ya ukosefu wa heshima.+ 27 Kwa sababu hiyo uliwatia mikononi mwa maadui wao,+ walioendelea kuwatesa.+ Lakini walipokuwa wakiteseka walikulilia, nawe uliwasikia ukiwa mbinguni; na kwa sababu ya rehema zako nyingi, uliwapa waokozi waliowaokoa kutoka mikononi mwa maadui wao.+

28 “Lakini mara tu walipopata utulivu, walitenda tena yaliyo maovu mbele zako,+ nawe ulikuwa ukiwaacha mikononi mwa maadui wao, ambao waliwakandamiza.*+ Kisha walirudi na kukuomba msaada,+ nawe uliwasikiliza ukiwa mbinguni na kuwaokoa tena na tena kwa sababu ya rehema zako nyingi.+ 29 Ingawa uliwaonya ili wairudie Sheria yako, walitenda kwa kimbelembele na kukataa kusikiliza amri zako;+ nao wakatenda dhambi kwa kutofuata masharti yako, ambayo mtu akiyafuata ataishi.+ Lakini walikugeuzia mgongo na kufanya shingo zao ziwe ngumu, nao wakakataa kukusikiliza. 30 Uliwaonyesha subira+ kwa miaka mingi na ukaendelea kuwaonya kwa roho yako kupitia manabii wako, lakini walikataa kusikiliza. Mwishowe ukawatia mikononi mwa mataifa ya nchi hizo.+ 31 Na kwa sababu ya rehema zako nyingi, hukuwaangamiza+ wala kuwaacha, kwa maana wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema.+

32 “Na sasa, Ee Mungu wetu, Mungu mkuu, mwenye nguvu, mwenye kuogopesha, unayeshika agano lako na kutenda kwa upendo mshikamanifu,+ usiyaone kuwa madogo mateso yote yaliyotupata sisi, wafalme wetu, wakuu wetu,+ makuhani wetu,+ manabii wetu,+ mababu zetu, na watu wako wote tangu siku za wafalme wa Ashuru+ mpaka leo hii. 33 Umekuwa mwadilifu katika mambo yote yaliyotupata, kwa maana umetenda kwa uaminifu; lakini ni sisi tuliotenda uovu.+ 34 Wafalme wetu, wakuu wetu, makuhani wetu, na mababu zetu hawajashika Sheria yako wala kusikiliza amri zako wala vikumbusho ulivyowapa* ili kuwaonya. 35 Hata walipokuwa kwenye ufalme wao wakifurahia wema mwingi uliowapa na katika nchi kubwa na yenye rutuba* uliyowapa, hawakukutumikia+ wala kuacha mazoea yao maovu. 36 Basi leo hii sisi ni watumwa+—naam, watumwa katika nchi ambayo uliwapa mababu zetu ili wale matunda yake na vitu vyake vyema. 37 Mazao yake mengi ni ya wafalme uliowafanya watutawale kwa sababu ya dhambi zetu.+ Wanatutawala wapendavyo na kuitendea mifugo yetu wapendavyo, tunateseka sana.

38 “Basi kwa sababu ya hayo yote, tunafanya mapatano thabiti+ kwa maandishi, nayo yamethibitishwa kwa muhuri wa wakuu wetu, Walawi wetu, na makuhani wetu.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki