Yobu
30 “Sasa wananichekelea+
—Wanaume wenye miaka kidogo kuliko mimi,
Wenye baba zao ningekataa
Kuwaweka pamoja na imbwa wenye kulinda kundi langu.
2 Uwezo wa mikono yao ulikuwa na faida gani kwangu?
Nguvu zao zimekwisha.
3 Wamechoka sana kwa sababu ya uhitaji na njaa;
Wanatafuna udongo wenye kukauka
Wenye ulikuwa tayari umeharibiwa na kuachwa ukiwa.
4 Wanakusanya mumea wa chumvi kutoka katika miti midogo-midogo;
Chakula chao ni muzizi wa miti ya miretemu.
5 Wanafukuzwa watoke katikati ya watu;+
Watu wanawalalamikia kama vile wangemufanyia mwizi.
6 Wanaishi kwenye miteremuko ya mabonde,
Katika mashimo ya udongo na ya miamba.
7 Wanalia katika miti midogo-midogo
Na wanajikusanya kati ya mimea yenye kuwasha.
8 Kama wana wa wenye hawana akili na wenye hawana jina,
Wamefukuzwa* watoke katika inchi.
11 Kwa sababu Mungu ameniondolea nguvu zangu* na kuninyenyekeza,
Hawajizuie kufanya jambo lolote mbele yangu.*
12 Kwenye mukono wangu wa kuume wanasimama kama kikundi cha watu wenye kasirani;
Wananifukuza
Na wanatia vizuizi vya uharibifu katika njia yangu.
14 Wanakuja kama vile watu wenye kupita katika tundu kubwa la ukuta;
Wanakuja kwa wingi katikati ya uharibifu.
15 Woga mukubwa umenilemea;
Heshima yangu imepeperushwa mbali kama upepo,
Na wokovu wangu umepotea kama wingu.
18 Nguvu nyingi zinaharibu nguo yangu;*
Inanibana kama shingo ya nguo yangu.
19 Mungu ameniangusha chini ndani ya matope;
Nimefanywa kuwa mavumbi na majivu.
20 Ninakulilia unisaidie, lakini haunijibu;+
Ninasimama, lakini wewe unaniangalia tu.
21 Umenitendea bila huruma;+
Kwa nguvu zote za mukono wako, unanishambulia.
22 Unaniinua na kunipeperusha kwa upepo;
Kisha unanitupa huku na huku katika zoruba.*
23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha mupaka kwenye kifo,
Nyumba kwenye kila mutu mwenye uzima ataenda.
24 Lakini hakuna mwenye angepiga mutu mwenye kuvunjika moyo*+
Wakati analilia musaada akiwa katika taabu.
25 Je, sikutoa machozi kwa ajili ya wale wenye walikuwa katika magumu?
Je, sikuhuzunika* kwa ajili ya maskini?+
26 Hata kama nilitumainia mema, mabaya yalikuja;
Nilitazamia mwangaza, lakini giza likakuja.
27 Tumbo langu lilinguruma bila kuacha;
Siku za mateso zilinishambulia.
28 Ninatembea-tembea kwa huzuni;+ hakuna mwangaza wa jua.
Katika mukusanyiko wa watu, ninasimama na kulilia musaada.
29 Nimekuwa ndugu ya mbweha
Na rafiki ya mabinti wa mbuni.+
31 Kinubi changu kinatumiwa tu kwa ajili ya maombolezo,
Na filimbi* yangu kwa ajili ya sauti ya kilio.