Zaburi
Ya Daudi. Muziki.
24 Dunia na vyote vyenye kuwa ndani yake ni vya Yehova,+
Inchi yenye kuzaa na wale wenye kukaa juu yake.
2 Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+
Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.
3 Ni nani anaweza kupanda mulima wa Yehova,+
Na ni nani anaweza kusimama mahali pake patakatifu?
4 Mutu yeyote mwenye mikono yenye haina kosa na mwenye moyo safi,+
Mwenye hajaapa kiapo cha uongo kwa uzima Wangu,*
Wala kuapa kwa udanganyifu.+
6 Hiki ni kizazi cha wale wenye kumutafuta,
Cha wale wenye kutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
7 Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+
Mufunguke,* ninyi miingilio ya zamani,
Ili Mufalme mwenye utukufu aingie!+
8 Mufalme huyu mwenye utukufu ni nani?
9 Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+
Mufunguke, ninyi miingilio ya zamani,
Ili Mufalme mwenye utukufu aingie!
10 Yeye ni nani, huyo Mufalme mwenye utukufu?
Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.+ (Sela)