Kumbukumbu la Torati
10 “Wakati huo Yehova aliniambia, ‘Ujichongee mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza,+ na upande kuja kwangu kwenye mulima; unapaswa kujitengenezea pia sanduku la mbao. 2 Na nitaandika kwenye mabamba hayo maneno yenye yalikuwa kwenye yale mabamba ya kwanza, yenye ulivunja-vunja, na utatia mabamba hayo ndani ya sanduku hilo.’ 3 Kwa hiyo nikatengeneza sanduku la mbao za mugunga* na kuchonga mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza na kupanda kwenye mulima nikiwa na mabamba hayo mbili katika mukono wangu.+ 4 Kisha akaandika kwenye mabamba hayo maneno yenye alikuwa ameandika mbele,+ zile Amri Kumi (10),*+ zenye Yehova alikuwa amewaambia ninyi kwenye mulima kutoka katika moto+ siku ya mukusanyiko;*+ na Yehova akanipatia mabamba hayo. 5 Kisha nikageuka na kushuka kutoka kwenye mulima+ na kutia mabamba hayo katika sanduku lenye nilikuwa nimetengeneza, yangali ndani, kama vile Yehova alikuwa ameniamuru.
6 “Kisha Waisraeli wakaondoka Beeroti Bene-yaakani na kuenda Mosera. Haruni akakufa na kuzikwa kule,+ na Eleazari mwana wake akaanza kutumika akiwa kuhani pa nafasi yake.+ 7 Kutoka kule wakaelekea Gudgoda, na kutoka Gudgoda wakaelekea Yotbata,+ inchi yenye kutiririka mito midogo ya maji.*
8 “Wakati huo Yehova alitia pembeni kabila la Lawi+ ili libebe sanduku la agano la Yehova,+ kusudi lisimame mbele ya Yehova ili kumutolea utumishi, na kubariki katika jina lake,+ kama vile wanafanya mupaka leo. 9 Ndiyo maana Lawi hakupewa fungu wala uriti pamoja na ndugu zake. Yehova ndiye uriti wake, kama vile Yehova Mungu wako alikuwa amemuambia.+ 10 Mimi mwenyewe nilikaa kwenye mulima kama vile nilifanya mara ya kwanza, siku makumi ine (40), muchana na usiku,+ na Yehova alinisikiliza wakati huo pia.+ Yehova hakutaka kukuharibu. 11 Kisha Yehova akaniambia, ‘Tangulia mbele ya watu, na utayarishe kuondoka, ili waingie na kuriti inchi yenye nimeapia mababu zao kwamba nitawapatia.’+
12 “Sasa, Ee Israeli, Yehova Mungu wako anataka ufanye nini?+ Mambo haya tu: kumuogopa Yehova Mungu wako,+ kutembea katika njia zake zote,+ kumupenda, kumutumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote,+ 13 na kushika amri na sheria za Yehova zenye ninakuamuru leo kwa faida yako mwenyewe.+ 14 Angalia, mbingu, hata mbingu za mbingu* ni za Yehova Mungu wako, na dunia na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake.+ 15 Lakini ni mababu zako tu ndio Yehova alikaribia na kuwaonyesha upendo wake, na amewachagua ninyi, uzao wao,+ katikati ya vikundi vyote vya watu, kama vile muko leo. 16 Munapaswa sasa kusafisha* mioyo yenu+ na kuacha kuwa kichwa-nguvu vile.*+ 17 Kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu wa miungu+ na Bwana wa mabwana, Mungu mukubwa, mwenye nguvu, na mwenye kuogopesha sana, mwenye hamutendee mutu yeyote kwa upendeleo+ na hakubali rushwa.* 18 Anatenda haki kwa ajili ya mutoto mwenye hana baba* na mujane+ na anamupenda mukaaji mugeni,+ anamupatia chakula na nguo. 19 Ninyi pia munapaswa kumupenda mukaaji mugeni, kwa maana mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+
20 “Unapaswa kumuogopa Yehova Mungu wako, unapaswa kumutumikia yeye,+ unapaswa kushikamana naye, na unapaswa kuapa kwa jina lake. 21 Ni Yeye unapaswa kusifu.+ Yeye ni Mungu wako, mwenye amekufanyia mambo haya makubwa na yenye kuogopesha sana yenye macho yako mwenyewe yameona.+ 22 Mababu zako walishuka Misri+ na watu* makumi saba (70), na sasa Yehova Mungu wako amefanya mukuwe wengi kama nyota za mbinguni.+