Kumbukumbu la Torati
30 “Wakati maneno haya yote yatakuja juu yako, baraka na laana yenye nimeweka mbele yako,+ na uyakumbuke*+ katika mataifa yote kwenye Yehova Mungu wako amekusambaza,+ 2 na urudie kwa Yehova Mungu wako+ na kusikiliza sauti yake kulingana na mambo yote yenye ninakuamuru leo, wewe na wana wako, kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote,+ 3 basi Yehova Mungu wako atarudisha watu wako wenye walikamatwa mateka+ na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka katika vikundi vyote vya watu kwenye Yehova Mungu wako amekusambaza.+ 4 Hata kama watu wako wanasambazwa mupaka mwisho wa mbingu, Yehova Mungu wako atakukusanya na kukurudisha kutoka kule.+ 5 Yehova Mungu wako atakurudisha katika inchi yenye baba zako waliriti, na utairiti; na atakufanya ufanikiwe na kukufanya uongezeke kuliko baba zako.+ 6 Yehova Mungu wako atasafisha* moyo wako na moyo wa uzao wako,+ na hivyo utamupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote na ili uishi.+ 7 Kisha Yehova Mungu wako ataleta laana hizi zote juu ya maadui wako, wenye walikuchukia na kukutesa.+
8 “Halafu utarudia na kusikiliza sauti ya Yehova na kushika amri zake zote zenye ninakuamuru leo. 9 Yehova Mungu wako atakufanya upate matokeo ya muzuri sana katika kazi yote ya mikono yako,+ atafanya ukuwe na watoto wengi na mifugo mingi na mazao mengi ya udongo wako, kwa maana Yehova atafurahia tena kukufanya upate matokeo ya muzuri, kama vile alifurahia mababu zako.+ 10 Kwa maana wakati huo utasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako na kushika amri zake na sheria zenye kuandikwa katika kitabu hiki cha Sheria, na utarudia kwa Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote.+
11 “Sasa amri hii yenye ninakuamuru leo haiko nguvu sana kwako, wala haiko kwenye hauwezi kufika.*+ 12 Haiko mbinguni, ili useme, ‘Ni nani mwenye atapanda mupaka mbinguni na atuletee amri hiyo, ili tuisikie na kuishika?’+ 13 Wala haiko ngambo ingine ya bahari, ili useme, ‘Ni nani atavuka ngambo ingine ya bahari ili atuletee amri hiyo, ili tuisikie na kuishika?’ 14 Kwa maana lile neno liko karibu sana na wewe, katika kinywa chako mwenyewe na katika moyo wako mwenyewe,+ ili ulitende.+
15 “Angalia, ninaweka mbele yako leo uzima na mema, na kifo na mabaya.+ 16 Kama utasikiliza amri za Yehova Mungu wako zenye ninakuamuru leo, kwa kumupenda Yehova Mungu wako,+ kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na kanuni zake na maamuzi yake ya hukumu, basi utaishi+ na kuongezeka, na Yehova Mungu wako atakubariki katika inchi yenye unaenda kuriti.+
17 “Lakini kama moyo wako unageuka+ na hausikilize na unashawishiwa na unainamia miungu mingine na kuitumikia,+ 18 ninawaambia leo kwamba hakika mutaangamia.+ Hamutaishi wakati murefu katika inchi yenye unavuka Yordani ili kuiriti. 19 Ninachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi juu yako leo kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yako, baraka na laana;+ na unapaswa kuchagua uzima ili uendelee kuishi,+ wewe na wazao wako,+ 20 kwa kumupenda Yehova Mungu wako,+ kwa kusikiliza sauti yake, na kushikamana naye,+ kwa maana yeye ni uzima wako na kwa uwezo wake utafanya wakati murefu katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zako Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+