Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 16
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Paulo anamuchagua Timoteo (1-5)

      • Maono juu ya mwanaume Mumakedonia (6-10)

      • Lidia anakuwa muamini kule Filipi (11-15)

      • Paulo na Sila wanafungwa katika gereza (16-24)

      • Mulinzi wa gereza na nyumba yake yote wanabatizwa (25-34)

      • Paulo anataka wamuombe musamaha (35-40)

Matendo 16:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 14:5-7; 2 Tim. 3:11
  • +Mdo 19:22; Rom. 16:21; 1 Kor. 4:17; 1 Tes. 3:2; 1 Tim. 1:2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/11/2015, uku. 9

    Kutoa Ushahidi, uku. 122

Matendo 16:2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/11/2015, uku. 14

    15/12/2009, uku. 11

    15/5/2009, uku. 14

    Kutoa Ushahidi, uku. 122

Matendo 16:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Kor. 9:20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/11/2015, uku. 14

    15/5/2008, uku. 32

    1/12/2003, uku. 20-21

    Kutoa Ushahidi, uku. 122

Matendo 16:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 15:28, 29

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 123

Matendo 16:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 123

Matendo 16:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 18:23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 9-10

    15/5/2008, uku. 32

    Kutoa Ushahidi, uku. 125

Matendo 16:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Pe. 1:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 9-10

    15/5/2008, uku. 32

    Kutoa Ushahidi, uku. 125-126

Matendo 16:8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 9-10

    Kutoa Ushahidi, uku. 125-126

Matendo 16:9

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 9-10

    Kutoa Ushahidi, uku. 126

Matendo 16:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 12, 126

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/11/2007, uku. 18-19

Matendo 16:11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 124

Matendo 16:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Flp 1:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,”

    uku. 223-224

Matendo 16:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ufu 1:11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 132

Matendo 16:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 16:33; 18:8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 132

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/3/2007, uku. 32

    Mwalimu, uku. 95

Matendo 16:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 19:31; 20:6

Matendo 16:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mk 1:23, 24; Lu 4:41

Matendo 16:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 17:18; Mk 1:25, 26, 34; Lu 9:1; 10:17

Matendo 16:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 19:24, 25
  • +Mt 10:18

Matendo 16:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 17:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, uku. 1971

Matendo 16:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Tes. 2:2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 129

Matendo 16:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Lu 21:12

Matendo 16:24

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 129

    Huduma ya Ufalme,

    2/2000, uku. 4-5

Matendo 16:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Efe 5:19; Kol 3:16

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/8/2012, uku. 29

    Kutoa Ushahidi, uku. 130

Matendo 16:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 5:18-20; 12:7

Matendo 16:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 12:18, 19

Matendo 16:28

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/4/2002, uku. 26

Matendo 16:30

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 130

Matendo 16:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoh 3:16; 6:47

Matendo 16:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 130

Matendo 16:33

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 8:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 130

Matendo 16:37

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bila kutusambisha.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:25; 23:27

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/3/2015, uku. 12

Matendo 16:38

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 22:27-29

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 131

Matendo 16:40

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 1:3, 4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 132

Maandiko ingine

Mdo. 16:1Mdo 14:5-7; 2 Tim. 3:11
Mdo. 16:1Mdo 19:22; Rom. 16:21; 1 Kor. 4:17; 1 Tes. 3:2; 1 Tim. 1:2
Mdo. 16:31 Kor. 9:20
Mdo. 16:4Mdo 15:28, 29
Mdo. 16:6Mdo 18:23
Mdo. 16:71 Pe. 1:1
Mdo. 16:12Flp 1:1
Mdo. 16:14Ufu 1:11
Mdo. 16:15Mdo 16:33; 18:8
Mdo. 16:16Law. 19:31; 20:6
Mdo. 16:17Mk 1:23, 24; Lu 4:41
Mdo. 16:18Mt 17:18; Mk 1:25, 26, 34; Lu 9:1; 10:17
Mdo. 16:19Mdo 19:24, 25
Mdo. 16:19Mt 10:18
Mdo. 16:20Mdo 17:6
Mdo. 16:221 Tes. 2:2
Mdo. 16:23Lu 21:12
Mdo. 16:25Efe 5:19; Kol 3:16
Mdo. 16:26Mdo 5:18-20; 12:7
Mdo. 16:27Mdo 12:18, 19
Mdo. 16:31Yoh 3:16; 6:47
Mdo. 16:33Mdo 8:12
Mdo. 16:37Mdo 22:25; 23:27
Mdo. 16:38Mdo 22:27-29
Mdo. 16:402 Kor. 1:3, 4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 16:1-40

Matendo ya Mitume

16 Basi akafika Derbe na pia Listra.+ Na mwanafunzi mumoja mwenye kuitwa Timoteo+ alikuwa kule, alikuwa mwana wa mwanamuke Muyahudi mwenye alikuwa muamini, lakini baba yake alikuwa Mugiriki, 2 na ndugu kule Listra na Ikoniamu walikuwa wanatoa ushahidi muzuri juu yake. 3 Paulo alitamani Timoteo aende pamoja naye, basi akamuchukua na akamutahiri kwa sababu ya Wayahudi wenye walikuwa katika sehemu hizo,+ kwa maana wote walijua kwamba baba yake alikuwa Mugiriki. 4 Wakati walikuwa wanapita katika miji, walikuwa wanawapatia maagizo yenye yalikuwa yameamuliwa na mitume na wazee wenye walikuwa Yerusalemu+ ili wayashike. 5 Kisha, kwa kweli, makutaniko yakaendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.

6 Zaidi ya hayo, wakapitia Frigia na inchi ya Galatia,+ kwa sababu roho takatifu iliwakataza kusema lile neno katika jimbo la Asia. 7 Tena, wakati walishuka na kufika Misia wakajaribu kuingia Bitinia,+ lakini roho ya Yesu haikuwaruhusu. 8 Basi wakapita Misia na kushuka mupaka Troa. 9 Na usiku Paulo akaona maono⁠—⁠mwanaume mumoja Mumakedonia alikuwa amesimama pale akimuomba: “Vuka uingie Makedonia na utusaidie.” 10 Kisha tu yeye kuona maono hayo, tukajaribu kuingia Makedonia, kwa kuwa tulifikia uamuzi wa kwamba Mungu alikuwa ametuita tuwatangazie habari njema.

11 Basi tukasafiri katika bahari kutoka Troa na tukaenda moja kwa moja mupaka Samotrake, lakini siku yenye ilifuata tukaenda Neapoli; 12 na kutoka kule tukaenda Filipi,+ koloni, lenye ni muji mukubwa wa wilaya ya Makedonia. Tukakaa katika muji huo kwa siku fulani. 13 Siku ya Sabato tukaenda inje ya mulango mukubwa karibu na muto, kwenye tuliwaza kulikuwa mahali pa sala, tukakaa na kuanza kuzungumuza na wanamuke wenye walikuwa wamekusanyika. 14 Na mwanamuke fulani mwenye aliitwa Lidia, muuzishaji wa nguo za rangi ya zambarau, wa muji wa Tiatira+ na muabudu wa Mungu, alikuwa anasikiliza, na Yehova* akafungua wazi moyo wake asikilize kwa uangalifu mambo yenye Paulo alikuwa anasema. 15 Sasa wakati yeye na watu wa nyumba yake walibatizwa,+ akatuomba: “Kama mumeniona kuwa muaminifu kwa Yehova,* mukuje na mukae katika nyumba yangu.” Na akatulazimisha kuenda.

16 Sasa ikatokea kwamba wakati tulikuwa tunaenda mahali pale pa sala, tulikutana na mutumishi mumoja mwanamuke mwenye alikuwa na roho, pepo muchafu wa uaguzi.+ Aliletea mabwana wake faida nyingi kwa kutabiri matukio. 17 Ule mutumishi mwanamuke alikuwa anamufuata Paulo na sisi na alikuwa anasema maneno haya kwa sauti kubwa: “Watu hawa ni watumwa wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi+ na wanawatangazia ninyi njia ya wokovu.” 18 Akaendelea kufanya vile kwa siku nyingi. Mwishowe jambo hilo likamuchokesha Paulo, akageuka na kumuambia huyo roho: “Ninakuagiza katika jina la Yesu Kristo utoke ndani yake.” Na akatoka saa ileile.+

19 Basi, wakati mabwana wake waliona kama tumaini lao la kupata faida lilikuwa limeondolewa,+ wakamukamata Paulo na Sila na wakawakokota mupaka katika soko kwa watawala.+ 20 Wakawapeleka mupaka kwa waamuzi wa raia, na kusema: “Watu hawa wanasumbua sana muji wetu.+ Wao ni Wayahudi, 21 na wanatangaza desturi zenye haturuhusiwe kukubali ao kufuata, kwa kuwa sisi ni Waroma.” 22 Na watu wengi wakasimama pamoja ili kuwapinga, na wale waamuzi wa raia wakapasua nguo zao, kisha wakatoa amri wapigwe fimbo.+ 23 Kisha kuwapiga sana, wakawatupa katika gereza na wakaagiza mulinzi wa gereza awalinde muzuri.+ 24 Kwa sababu alipewa agizo hilo, akawatupa katika chumba cha ndani zaidi cha gereza na kufunga miguu yao katika mikatale.

25 Lakini karibu katikati ya usiku, Paulo na Sila walikuwa wanasali na kumusifu Mungu kwa wimbo,+ na wafungwa walikuwa wanawasikiliza. 26 Tetemeko kubwa la inchi likatokea kwa kushitukia na misingi ya gereza ikatikiswa. Zaidi ya hayo, milango yote ikafunguka mara moja, na vifungo vya wote vikafunguka.+ 27 Wakati mulinzi wa gereza aliamuka na kuona kwamba milango ya gereza ilikuwa imefunguka, akachomoa upanga wake na alikuwa karibu kujiua, kwa sababu aliwaza wafungwa walikuwa wamekimbia.+ 28 Lakini Paulo akasema kwa sauti kubwa: “Usijiumize, kwa maana sisi wote tuko hapa!” 29 Kwa hiyo, akaomba walete mwangaza na akaingia ndani mbio, na alikuwa anatetemeka, akaanguka chini mbele ya Paulo na Sila. 30 Na akawaleta inje na kusema: “Mabwana wangu, nifanye nini ili niokolewe?” 31 Wakajibu: “Amini Bwana Yesu na utaokolewa, wewe na nyumba yako.”+ 32 Kisha wakamuambia neno la Yehova* yeye pamoja na wote wenye walikuwa katika nyumba yake. 33 Na akaenda pamoja nao saa hiyo ya usiku na akasafisha vidonda vyao. Kisha yeye na nyumba yake yote wakabatizwa bila kukawia.+ 34 Akawaleta katika nyumba yake na akaweka chakula kwenye meza mbele yao, na akafurahi sana pamoja na nyumba yake yote kwa kuwa sasa alikuwa amemuamini Mungu.

35 Wakati ilikuwa muchana, waamuzi wa raia wakatuma wakubwa wa polisi wakisema: “Fungua wale watu.” 36 Mulinzi wa gereza akamuambia Paulo maneno yao: “Waamuzi wa raia wametuma watu kwamba ninyi wawili mufunguliwe. Basi mutoke sasa na muende kwa amani.” 37 Lakini Paulo akawaambia: “Walitupiga fimbo mbele ya watu wote, bila kutuhukumu,* ijapokuwa sisi ni Waroma,+ na wakatutupa katika gereza. Je, sasa wanataka kututosha kwa uficho? Hapana, haiwezekane! Acha wakuje watutoshe wao wenyewe.” 38 Wale wakubwa wa polisi wakaelezea waamuzi wa raia maneno hayo. Na hawa wakaogopa wakati walisikia kwamba watu hao walikuwa Waroma.+ 39 Basi wakakuja na kuwabembeleza na kisha kuwapeleka inje, wakawaomba watoke katika muji huo. 40 Lakini wakatoka katika gereza na wakaenda kwenye nyumba ya Lidia, na wakati waliona ndugu, wakawatia moyo+ na wakaondoka.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine