Yobu
33 “Lakini sasa, Yobu, tafazali sikia maneno yangu;
Sikiliza kila kitu chenye ninasema.
2 Angalia, tafazali! Ninapaswa kufungua kinywa changu;
Ulimi wangu unapaswa* kusema.
3 Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+
Na midomo yangu inasema kwa uaminifu mambo yenye ninajua.
5 Unijibu basi kama unaweza;
Toa mawazo yako mbele yangu; ukuwe tayari kujitetea.
6 Angalia! Mimi niko tu kama wewe mbele ya Mungu wa kweli;
Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+
7 Kwa hiyo woga wangu usikuogopeshe
Na mukazo wowote kutoka kwangu usikulemee.
8 Lakini ulisema katika masikio yangu,
Ndiyo, niliendelea kusikia maneno haya,
9 ‘Niko safi, sina zambi;+
Niko safi, sina kosa.+
10 Lakini Mungu anapata sababu za kunipinga;
Ananiona kuwa adui yake.+
11 Anatia miguu yangu katika mikatale;
Anachunguza njia zangu zote.’+
12 Lakini unakosea kwa kusema vile, kwa hiyo nitakujibu;
Mungu ni mukubwa kuliko mwanadamu mwenye anaweza kufa.+
13 Sababu gani unamulaumu Yeye?+
Je, ni sababu hajajibu maneno yako yote?+
14 Kwa maana Mungu anasema mara moja na mara ya pili,
Lakini hakuna mutu mwenye anasikiliza,
15 Katika ndoto, maono ya usiku,+
Wakati wanadamu wanashikwa na usingizi muzito
Wakati wanalala kwenye vitanda vyao.
16 Kisha anafungua masikio yao+
Na anaingiza* maagizo yake ndani yao,
17 Ili kumuepusha mutu asifanye zambi+
Na kulinda mwanadamu ili asikuwe na kiburi.+
19 Mutu anakaripiwa pia kupitia maumivu kwenye kitanda chake
Na kupitia maumivu yenye kuendelea ya mifupa yake,
20 Kwa hiyo nafsi yake inachukia* sana mukate,
21 Nyama ya mwili wake inakonda hata haitambuliwe,
Na mifupa yake yenye ilikuwa haionekane inatoka sasa inje.*
23 Kama kuko mujumbe* kwa ajili yake,
Muteteaji mumoja kati ya elfu moja (1 000),
Ili amuambie mwanadamu mambo yenye kunyooka,
24 Kisha Mungu anamuonyesha wema na kusema,
Nimepata bei ya ukombozi!+
26 Atamulilia Mungu,+ mwenye atamukubali,
Na ataona uso Wake na kupiga vigelegele vya shangwe,
Na Yeye atamurudishia mwanadamu mwenye anaweza kufa haki Yake.
27 Mutu huyo ataambia* watu,
‘Nimefanya zambi+ na kupotosha mambo yenye kuwa sawa,
Lakini sikupokea kile chenye nilistahili.*
29 Kwa kweli, Mungu anafanya mambo yote haya
Mara mbili, mara tatu (3), kwa ajili ya mwanadamu,
30 Ili kumutosha* katika shimo,*
Kusudi aweze kuangaziwa na mwangaza wa uzima.+
31 Kaza uangalifu, Yobu! Unisikilize!
Nyamaza, na mimi nitaendelea kusema.
32 Kama uko na jambo la kusema, unijibu.
Sema, kwa maana ninataka kukutetea.
33 Kama hauna jambo la kusema, unisikilize;
Nyamaza, na mimi nitakufundisha hekima.”