Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 11 uku. 16-21
  • Yesu Ni Kuhani Mukubwa Mwenye Huruma

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Ni Kuhani Mukubwa Mwenye Huruma
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MWANA MUPENDWA WA MUNGU ANAKUYA KU DUNIA
  • YESU ALIJITIA FASI YA BENGINE
  • NAMNA TUNAIGA KUHANI WETU MUKUBWA LEO
  • KUHANI WETU MUKUBWA ANAWEZA KUKUSAIDIA
  • Bei ya Ukombozi Inatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Siku 40 za Mwisho za Yesu ku Dunia, Zinatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 11 uku. 16-21

HABARI YA KUJIFUNZA YA 46

WIMBO 17 “Ninataka”

Yesu Ni Kuhani Mukubwa Mwenye Huruma

“Hatuna kuhani mukubwa mwenye hawezi kusikilia uzaifu wetu huruma.”—EBR. 4:15.

WAZO KUBWA

Yesu ni Kuhani Mukubwa muzuri juu iko na huruma na anaweza kutusaidia mu njia mbalimbali leo.

1-2. (a) Juu ya nini Yehova alituma Mwana wake ku dunia? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari? (Waebrania 5:7-9)

MIAKA 2000 hivi yenye imepita, Yehova alituma Mwana wake mupendwa ku dunia. Juu ya nini? Kwanza ni juu ya kukomboa banadamu kutoka mu zambi na kifo na kumaliza magumu yenye Shetani ametuletea. (Yoh. 3:16; 1 Yo. 3:8) Pia Yehova alijua kama juu Yesu angekuwa mwanadamu ku dunia, ile ingemutayarisha ili akuwe Kuhani Mukubwa mwenye huruma, mwenye kutuelewa, na mwenye kujitia fasi yetu. Yesu alianza kutumikia kama Kuhani Mukubwa kisha ubatizo wake mu mwaka wa 29.a

2 Mu hii habari, tutazungumuzia namna kuwa mwanadamu ku dunia kulisaidia Yesu akuwe Kuhani Mukubwa mwenye huruma. Ni jambo ya maana tuelewe muzuri ile wazo juu itafanya ikuwe mwepesi kwetu kusali na kumukaribia Yehova, zaidi sana wakati tunavunjika moyo juu ya zambi zetu ao uzaifu wetu.—Soma Waebrania 5:7-9.

MWANA MUPENDWA WA MUNGU ANAKUYA KU DUNIA

3-4. Maisha ya Yesu ilibadilika namna gani wakati alikuya ku dunia?

3 Bamingi kati yetu tulishakafanya mabadiliko fulani mu maisha. Pengine tulihama na kuacha fasi kwenye tulikuwa napenda, batu ya familia, na marafiki. Haikuwake mwepesi kufanya mabadiliko. Lakini hakuna mwanadamu mwenye alishakafanya mabadiliko makubwa sana sawa Yesu. Alikuwa malaika wa kwanza na wa maana sana mbinguni. Yehova alimupenda sana na alikuwa na furaha sikuzote juu alikuwa natumika ku ‘mukono wa kuume’ wa Mungu. (Zb. 16:11; Mez. 8:30) Lakini, Wafilipi 2:7 inasema kama kwa kupenda “alijiondolea hali yake,” ni kusema aliacha cheo yake ya juu mbinguni juu aishi ku dunia na banadamu benye habakamilike.

4 Fikiria mambo yenye ilimufikia kisha kuzaliwa ku dunia. Kwanza alizaliwa mu familia maskini; tunajua vile juu bazazi yake balitoa zabihu ya hali ya chini kisha kuzaliwa kwake. (Law. 12:8; Lu. 2:24) Kisha, wakati mufalme mubaya Herode alipata habari juu ya kuzaliwa kwa Yesu, alijaribu kumuua. Kwa hiyo, familia ya Yesu ilikimbilia Misri juu ya kuokoa uzima wa Yesu, na ilibakia kule kwa wakati fulani. (Mt. 2:13, 15) Kwa kweli, maisha ya Yesu ku dunia ilikuwa tofauti kabisa na maisha yenye alikuwa nayo mbinguni!

5. Yesu aliona nini wakati alikuwa ku dunia, na namna gani kuishi ku dunia kulimusaidia akuwe Kuhani Mukubwa mwenye huruma? (Ona pia picha.)

5 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, aliona vile batu mingi balikuwa nateseka. Alielewa muzuri uchungu wenye mutu anasikiaka wakati mupendwa wake anakufa. Pengine batu benye alikuwa najua balikufa, kutia ndani baba yake Yosefu. Mu utumishi wake, alikutana na batu benye balikuwa na ugonjwa wa ukoma, bipofu, benye kupooza, na bazazi benye balifisha batoto yabo. Yesu alisikilia bale batu bote huruma. (Mt. 9:2, 6; 15:30; 20:34; Mk. 1:40, 41; Lu. 7:13) Ni kweli kama hata wakati alikuwa mbinguni alikuwa naona vile batu biko nateseka. Lakini wakati alikuwa mwanadamu ku dunia, alielewa muzuri zaidi maumivu yenye batu banasikiaka wakati biko nateseka. (Isa. 53:4) Kuwa mwanadamu ku dunia kulimusaidia aelewe namna banadamu banajisikiaka mu hali mbalimbali, na uchungu wenye magumu mbalimbali inabaleteaka. Zaidi ya ile, sawa tu banadamu bengine Yesu alichoka, alikuwa na mahangaiko, na alisikia huzuni.

Yesu anazungukwa na batu mingi benye biko namulilia abaponyeshe. Kwa huruma anakamata mikono ya mwanaume mwenye kuzeeka mwenye kuwa kilema.

Wakati Yesu aliona mateso ya batu, alibasikilia huruma na kubahangaikia (Ona fungu ya 5)


YESU ALIJITIA FASI YA BENGINE

6. Maneno ya mufano yenye nabii Isaya alitumikisha inatufundisha nini juu ya huruma ya Yesu? (Isaya 42:3)

6 Mu utumishi wake ku dunia, Yesu alionyesha sana huruma batu ya hali ya chini na benye kuonewa. Kwa kufanya vile, alitimiza unabii. Mu maandiko ya Kiebrania, wakati fulani mutu mwenye nguvu anafananishwa na bustani yenye kumwangiwa mayi ao muti mukubwa. (Zb. 92:12; Isa. 61:3; Yer. 31:12) Lakini maskini na wenye kuonewa wanafananishwa na utete wenye kupondekana na utambi wa taa wenye kutoa moshi; batu habaonake bile bitu mbili kuwa bya maana. (Soma Isaya 42:3; Mt. 12:20) Kwa kuongozwa na roho ya Mungu, nabii Isaya alitumikisha ile maneno ya mufano juu ya kutabiri namna Yesu angeonyesha upendo na huruma batu ya kawaida, benye balionekana kuwa ba bure.

7-8. Yesu alitimiza unabii wa Isaya namna gani?

7 Injili ya Matayo inaonyesha kama Yesu alitimiza hii maneno ya Isaya: “Hatavunja utete wenye kupondekana, na hatazima utambi wenye kutoa moshi.” Miujiza mingi ya Yesu ilisaidia batu benye balitendewa mubaya, benye balijiona sawa utete wenye kupondekana. Ilisaidia pia batu benye habakukuwa na tumaini mu maisha, benye balijiona sawa utambi wa taa wenye uko karibu kuzimika. Kwa mufano Yesu aliponyesha mwanaume moya mwenye alikuwa nayala ukoma. Ule mwanaume hakukuwa tena na tumaini ya kupona. Pengine aliwaza kama hatapitishaka tena wakati pamoya na batu ya familia yake na barafiki. (Lu. 5:12, 13) Tena Yesu aliponyesha mwanaume fulani mwenye alikuwa kiziwi na hakukuwa nasema muzuri. Wazia vile ule mwanaume alikuwa najisikia wakati alikuwa naona bengine biko nazungumuza lakini yeye hasikie hata kitu. (Mk. 7:32, 33) Lakini haiko ile mambo tu njo Yesu alifanya.

8 Mu siku za Yesu, Bayahudi mingi balikuwa naamini kama benye balikuwa nateseka balikuwa napata malipizi juu ya zambi zabo ao za bazazi yabo. (Yoh. 9:2) Ile mawazo ilifanya benye balikuwa nateseka bajione kuwa batu ya bure. Lakini juu ya kutimiza unabii wa Isaya, Yesu aliponyesha bale batu na kubasaidia bajue kama Yehova anabahangaikiaka. Ile inatufundisha nini juu ya Yesu?

9. Waebrania 4:15, 16 inaonyesha namna gani kama Kuhani wetu Mukubwa wa mbinguni anasikilia huruma banadamu benye habakamilike?

9 Soma Waebrania 4:15, 16. Tunaweza kuwa hakika kama Yesu atatusikilia huruma sikuzote. Juu tukuwe hakika, tuelewe kwanza mutu wa huruma anakuwaka namna gani. Mutu wa huruma ni mutu mwenye mateso ya bengine inamugusaka sana. Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “kusikia huruma” inamaanisha kujisikia vile mwingine iko najisikia. (Ona pia Waebrania 10:34, kwenye Paulo anatumikisha ile neno ya Kigiriki.) Sasa, vile njo Yesu alikuwaka? Ndiyo. Wakati tunasoma mu Biblia juu ya miujiza ya Yesu, tunaona kama alisikilia kabisa huruma batu benye balikuwa nateseka. Aliponyesha batu juu alibahangaikia kabisa na alipenda kubasaidia, haiko juu alilazimika kufanya vile. Kwa mufano, wakati aliponyesha ule mwanaume mwenye alikuwa na ukoma, angependa angefanya vile kwa mbali, lakini alimukaribia na akamugusa; pengine hakuna mutu mwenye alikuwa alishagusa ule mwanaume kwa miaka mingi! Na wakati aliponyesha ule mwanaume kiziwi, alimutosha fasi kwenye kulikuwa fuyo ya batu, akamupeleka fasi ya kimya juu amuponyeshe. Fikiria pia mambo yenye ilitokea wakati mwanamuke fulani aliosha migulu ya Yesu kwa machozi yake. Ule mwanamuke alikuwaka nafanya mambo ya mubaya, lakini akatubu. (Mt. 8:3; Mk. 7:33; Lu. 7:44) Wakati mufarisayo fulani alisema mubaya juu ya ule mwanamuke, Yesu alimutetea na akakemea ule Mufarisayo. Yesu hakuepuka batu benye balikuwa nateseka juu ya magonjwa ao ulemavu, lakini alibakaribia na kwa huruma alibatia moyo na kubaonyesha upendo. Kwa hiyo, tukuwe hakika kama anatusikilia na siye huruma.

NAMNA TUNAIGA KUHANI WETU MUKUBWA LEO

10. Tuko na mambo gani leo yenye iko nasaidia bipofu na biziwi? (Ona pia picha.)

10 Juu tuko banafunzi ba kweli ba Yesu, tunajikaza kumuiga kwa kuonyesha bengine upendo, kwa kujitia fasi yabo, na kwa kubaonyesha huruma. (1 Pe. 2:21; 3:8) Ni kweli kama hatuwezi kuponyesha bipofu na biziwi, lakini tunaweza kubasaidia bamujue Yehova na bamukaribie. Kwa mufano, leo bichapo byetu byenye kutegemea Biblia binapatikana mu luga za ishara zaidi ya 100 na mu luga zaidi ya 60 mu maandishi ya bipofu. Na mu luga zaidi ya 100 tuko na video zenye zinapana mafasirio juu ya mambo yenye iko naonekana mu ile video (Audiodescription). Ile mambo yote inasaidia bipofu na biziwi bamukaribie Yehova na Mwana wake.

Picha: 1. Ndugu na dada biko naimba wimbo wa Ufalme mu luga ya Ishara ku mukutano wa kutaniko. 2. Dada kipofu iko nasoma Biblia mu maandishi ya bipofu.

Bichapo byetu byenye kutegemea Biblia binapatikana mu luga zaidi ya 1000

Kushoto: Luga za ishara zaidi ya 100

Kuume: Maandishi ya bipofu mu luga zaidi ya 60

(Ona fungu ya 10)


11. Sawa Yesu, namna gani tengenezo ya Yehova inaonyesha kama inahangaikia batu ya fasi yote? (Matendo 2:5-7, 33) (Ona pia picha.)

11 Tengenezo ya Yehova inajikaza kusaidia batu ba fasi yote. Kumbuka kama kisha Yesu kufufuliwa, alimwangia banafunzi yake roho takatifu juu basaidie batu yote benye balikuya ku sikukuu ya Pentekoste basikie habari njema, kila mutu mu “luga yake mwenyewe.” (Soma Matendo 2:5-7, 33.) Kwa kufuata muongozo wa Yesu, tengenezo ya Yehova inatoa bichapo byenye kutegemea Biblia mu luga zaidi ya 1000, hata mu luga zenye zinasemwa na batu kidogo. Kwa mufano, luga fulani za Kiamerindia zinazungumuzwa na batu kidogo benye kuishi mu Amerika ya kusini na ya kaskazini. Lakini, bichapo byetu binapatikana mu luga zaidi ya 160 kati ya zile luga. Na ile inasaidia batu mingi bapate nafasi ya kusikia habari njema. Bichapo byetu binapatikana pia mu luga zaidi ya 20 za Kiromania. Maelfu ya batu benye kusema zile luga bamekubali kweli.

Picha: 1. Dada wa Amerindia anafurahi wakati anakamata Biblia mu luga yake. 2. Dada Muromania na mutoto wake banafurahia kusikiliza programe ya kiroho.

Kushoto: Luga za Kiamerindia zaidi ya 160

Kuume: Luga za Kiromania zaidi ya 20

(Ona fungu ya 11)


12. Tengenezo ya Yehova iko nafanya nini ingine leo?

12 Zaidi ya kusaidia batu basikie habari njema, tengenezo ya Yehova inatolea misaada ndugu na dada benye banapatwa na misiba ya asili. Njo maana, maelfu ya bandugu na badada banajitolea juu ya kusaidia Bakristo benzabo benye biko na lazima ya musaada. Zaidi ya ile, tengenezo ya Yehova inajenga fasi za kukusanyikia zenye kufaa juu batu bakuwe na fasi ya kukutana pamoya ili bajifunze juu ya upendo wa Mungu.

KUHANI WETU MUKUBWA ANAWEZA KUKUSAIDIA

13. Yesu anatusaidia mu njia gani mbalimbali?

13 Juu Yesu ni muchungaji wetu muzuri, anahangaikia hali ya kiroho ya kila mumoya wetu. (Yoh. 10:14; Efe. 4:7) Saa moya mambo fulani mu maisha inaweza kufanya tujisikie sawa vile utete wenye kupondekana ao utambi wa taa wenye uko karibu kuzimika. Tunaweza kuvunjika moyo juu tuko na ugonjwa wa nguvu, juu ya makosa fulani yenye tulifanya, ao juu hatupatane na Mukristo mwenzetu. Ile mambo inaweza kufanya tukazie akili huzuni yetu mupaka tunashindwa kukazia akili tumaini yetu ya wakati wenye kuya. Lakini, kumbuka kama Yesu iko naona kila kitu yenye iko napitikana na anaelewa muzuri vile uko najisikia. Juu iko na huruma, atafanya jambo fulani juu ya kukusaidia. Kwa mufano, anaweza kutumikisha roho takatifu juu ya kukutia nguvu wakati uko muzaifu. (Yoh. 16:7; Tit. 3:6) Pia anaweza kutumikisha baabudu benzako na “zawadi katika wanadamu” juu ya kukutia moyo, kukutegemeza, na kukusaidia.—Efe. 4:8.

14. Tunaweza kufanya nini wakati tunavunjika moyo?

14 Wakati unavunjika moyo, ukumbuke kama Yesu ni Kuhani wetu Mukubwa, kisha utafakari namna kujua ile kunaweza kukusaidia. Kumbuka kama Yehova alimutuma Yesu ku dunia haiko juu tu atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi, lakini pia juu aelewe muzuri magumu yenye banadamu benye habakamilike banapambana nayo. Kwa hiyo, tukuwe hakika kama wakati tunavunjika moyo juu ya zambi zetu ao uzaifu wetu, Yesu iko tayari kutusaidia “kwa wakati wenye kufaa” na anapenda kufanya vile.—Ebr. 4:15, 16.

15. Leta mufano wenye kuonyesha namna mutu mwenye amemuacha Yehova anaweza kusaidiwa juu amurudilie.

15 Tena Yesu anaongoza banafunzi yake juu batafute na basaidie bale benye balishamuacha Yehova. (Mt. 18:12, 13) Ona mufano wa Stefano.b Aliondolewa mu kutaniko kwa miaka 12, kisha siku moya aliamua kuenda ku mukutano. Anasema hivi: “Haikukuwa mwepesi, lakini nilipenda kuwa tena mu familia ya Yehova yenye upendo. Bazee benye balikutana na miye balifanya nijisikie kama ninakaribishwa. Wakati fulani, nilijiona kuwa wa bure na nilipenda tu kubiacha. Lakini bazee balinikumbusha kama Yehova na Yesu banapenda niendelee kujikaza. Wakati nilirudishwa, kutaniko yote ilinikaribisha kwa furaha miye na familia yangu. Kisha bibi yangu alianza kujifunza Biblia, na leo tuko namutumikia Yehova pamoya mu familia.” Kwa kweli, Kuhani wetu Mukubwa mwenye upendo anafurahi kuona namna benye kutubu banapata musaada wenye biko nao lazima juu barudie mu kutaniko!

16. Juu ya nini unafurahia kuwa na Kuhani Mukubwa mwenye huruma?

16 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alisaidia batu mingi wakati balikuwa na lazima ya musaada. Leo pia, tunaweza kuwa hakika kama atatusaidia wakati tuko na lazima ya musaada. Na karibuni mu dunia mupya, atasaidia banadamu benye kutii juu basihangaishwe tena na matokeo ya zambi na kutokamilika. Tunamushukuru sana Mungu wetu, Yehova, juu upendo wake na huruma yake ilimuchochea aweke Mwana wake mwenye huruma kuwa Kuhani wetu Mukubwa!

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Namna gani kuwa mwanadamu ku dunia kulisaidia Yesu akuwe Kuhani Mukubwa muzuri?

  • Namna gani Yesu alitimiza Isaya 42:3?

  • Namna gani Kuhani wetu Mukubwa anatusaidia leo?

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

a Juu ya kujua namna daraka ya Yesu ya kuwa Kuhani Mukubwa ilikamata nafasi ya kuhani mukubwa wa Bayahudi, ona habari “Furahia Pendeleo Yako ya Kumutumikia Yehova mu Hekalu Yake ya Kiroho” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 10, 2023, uku. 26, fu. 7-9.

b Majina fulani imebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine