HABARI YA KUJIFUNZA YA 47
WIMBO 38 Atakupatia Nguvu
Uko Mutu wa Maana Sana!
“Wewe ni mutu mwenye samani sana.”—DA. 9:23.
WAZO KUBWA
Bale benye banajiona kuwa ba bure baelewe kama Yehova anabaona kuwa ba maana sana.
1-2. Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe hakika kama Yehova anatuona kuwa ba maana?
BATUMISHI bote ba Yehova ni ba maana. Lakini kuko benye banajionaka kama habiko ba maana. Pengine ni juu mutu fulani alibatendea mubaya. Na weye ulishakajiona kama hauko wa maana? Kama ni vile, nini njo inaweza kukusaidia ukuwe hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana?
2 Jambo moya yenye inaweza kukusaidia ni kusoma habari za Biblia zenye zinaonyesha namna Yehova anapenda batu batendewe. Mwana wake Yesu alitendea batu muzuri na kwa heshima. Kwa kufanya vile, alionyesha kama batu benye banajiona kuwa ba bure ni ba maana kwake na kwa Baba yake. (Yoh. 5:19; Ebr. 1:3) Mu hii habari, tutaona: (1) namna Yesu alisaidia batu bajione kuwa ba maana, na (2) namna tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatuona kuwa ba maana.—Hag. 2:7.
NAMNA YESU ALISAIDIA BATU BAJIONE KUWA BA MAANA
3. Namna gani Yesu alitendea Bagalilaya benye balikuya kwake juu abasaidie?
3 Wakati Yesu alikuwa nahubiri mu Galilaya, batu mingi balikuya kwake juu ya kumusikiliza na juu abaponyeshe. Yesu aliona kama ‘balikuwa bamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wenye hawana muchungaji.’ (Mt. 9:36) Bakubwa yabo ya dini balibaona kuwa batu ya bure sana, na hata balibaita kuwa ‘batu benye kulaaniwa.’ (Yoh. 7:47-49) Lakini Yesu alibaonyesha heshima kwa kukamata wakati ya kubafundisha na kubaponyesha. (Mt. 9:35) Na juu ya kusaidia batu mingi zaidi, Yesu alizoeza mitume wake mu kazi ya kuhubiri na alibapatia nguvu ya kuponyesha bagonjwa na balemavu.—Mt. 10:5-8.
4. Vile Yesu alitendea batu benye balionewa inatufundisha nini?
4 Juu Yesu alihangaikia basikilizaji yake na alibatendea kwa heshima, alionyesha kama batu benye mara mingi banaonwa kuwa ba bure, ni ba maana kwake na kwa Baba yake. Kama uko namutumikia Yehova lakini unawaza kama hauko wa maana, fikiria namna Yesu alihangaikia batu ba hali ya chini benye balikuya kumusikiliza. Kufanya vile kunaweza kukusaidia ujione kuwa wa maana sana kwa Yehova.
5. Fasiria hali ya mwanamuke fulani mwenye Yesu alikutana naye Galilaya.
5 Ni kweli Yesu alikuwa nafundisha bikundi ya batu, lakini alihangaikia pia mutu mumoya-mumoya. Kwa mufano, wakati wa utumishi wake mu Galilaya, alikutana na mwanamuke mwenye aliteseka sana juu alitokwa na damu kwa miaka 12. (Mk. 5:25) Kulingana na Sheria ya Musa, ile hali ilifanya ule mwanamuke asikuwe safi, na kila mutu mwenye angemugusa hangekuwa safi. Inawezekana ile ilifanya apitishe wakati mingi yeye peke, mbali na batu bengine. Zaidi ya ile, hangemuabudu Yehova pamoya na bengine ku sinagogi ao wakati wa sikukuu mbalimbali. (Law. 15:19, 25) Kwa hiyo, zaidi ya kuwa mugonjwa, inawezekana ule mwanamuke alijisikia kuwa mutu wa bure kabisa.—Mk. 5:26.
6. Mwanamuke mwenye alikuwa natokwa na damu alifanya nini juu apone?
6 Ule mwanamuke mwenye alikuwa nateseka sana alipenda Yesu amuponyeshe. Lakini hakumuomba Yesu moja kwa moja amuponyeshe. Juu ya nini? Pengine hali yake ilifanya asikie haya. Ao aliogopa kama Yesu atamukaripia juu aliingia katikati ya batu na japo kulingana na sheria hakukuwa safi. Kwa hiyo, aligusa tu nguo ya inje ya Yesu juu aliamini kabisa kama akifanya tu vile, atapona. (Mk. 5:27, 28) Na hakukosea kuamini vile, juu alipona. Wakati Yesu aliuliza nani alimugusa, ule mwanamuke alisema kama ni yeye. Yesu alitendea ule mwanamuke namna gani?
7. Yesu alitendea namna gani ule mwanamuke mwenye alikuwa nateseka sana? (Marko 5:34)
7 Yesu alitendea ule mwanamuke kwa upole na kwa heshima. Aliona namna “alikuwa na woga na alikuwa anatetemeka.” (Mk. 5:33) Kwa hiyo, alizungumuza naye kwa upole na alimutia moyo. Na hata alimuita “binti.” Kwa kumuita vile alionyesha kama anamuheshimia, na zaidi ya ile alionyesha kama anamuhangaikia na anamupenda. (Soma Marko 5:34.) Mu Biblia ni ile mara moya tu njo Yesu anaita mwanamuke “binti.” Pengine alimuita vile juu aliona namna alikuwa “anatetemeka.” Wazia namna ule mwanamuke alijisikia wakati Yesu alizungumuza naye kwa upendo. Maneno ya Yesu ya kutia moyo ilimusaidia asijihukumu juu aligusa nguo ya Yesu na juu aliingia katikati ya batu. Zaidi ya kumuponyesha, Yesu alimusaidia pia ajione kuwa wa maana sana, ajione kuwa binti mupendwa wa Baba yetu wa mbinguni.
8. Dada fulani wa Brazili alikuwa na magumu gani?
8 Leo pia, batumishi fulani ba Yehova biko na matatizo fulani ya afya yenye inafanya bavunjike moyo na bajione kuwa ba bure. Mariaa ni painia wa kawaida mu Brazili, alizaliwa bila migulu na mukono wa kushoto. Anasema hivi: “Ku masomo mara mingi balinitendea mubaya juu ya ulemavu wangu. Na banafunzi benzangu balinipanga majina yenye iliniluma sana. Na hata batu ya familia yangu balinifanya nijisikie kuwa mutu wa bure.”
9. Ni nini ilisaidia Maria ajione kuwa wa maana kwa Yehova?
9 Nini njo ilisaidia Maria? Wakati alifikia kuwa Shahidi wa Yehova, Bakristo benzake balimufariji na kumusaidia ajione vile Yehova anamuona. Anasema hivi: “Bandugu na badada bamingi sana bamenisaidia! Ninashukuru Yehova kwa moyo wote kwa kunipatia familia ya muzuri ya ndugu na dada.” Bale bandugu na dada balisaidia sana Maria aone kama Yehova anamuona kuwa wa maana.
10. Nini njo ilikuwa nahangaisha Maria Magdalene? (Ona pia picha.)
10 Tuone vile Yesu alisaidia mutu mwingine. Ule mutu ni Maria Magdalene. Maria Magdalene alikuwa na pepo wachafu saba! (Lu. 8:2) Inawezekana wale pepo wachafu walifanya akuwe na tumatabia twenye hatukukuwa twa kawaida na ile ilifanya batu basimukaribie. Na inawezekana ile hali ilifanya ateseke sana. Pengine aliogopa na aliwaza kama hakuna mwenye anamupenda ao mwenye anaweza kumusaidia. Lakini, inawezekana Yesu alifukuza pepo wachafu wenye walikuwa namusumbua, na kisha Maria Magdalene akakuwa mwanafunzi wake. Yesu alifanya nini ingine juu ya kusaidia Maria Magdalene aone kama iko wa maana kwa Mungu?
Yesu alifanya nini juu ya kuhakikishia Maria Magdalene kama alikuwa wa maana kwa Yehova? (Ona fungu ya 10-11)
11. Namna gani Yesu alisaidia Maria Magdalene aone kama ni wa maana kwa Mungu? (Ona pia picha.)
11 Yesu aliomba Maria Magdalene amusindikize yeye na banafunzi yake mu kazi ya kuhubiri.b Matokeo ilikuwa nini? Maria Madgalene alipata pendeleo ya kusikiliza Yesu tena na tena wakati Yesu alikuwa nafundisha bengine. Pia siku yenye Yesu alifufuliwa, alitokea Maria Magdalene. Alikuwa kati ya banafunzi ba kwanza-kwanza benye Yesu alizungumuza nabo ile siku. Na hata Yesu alimupatia mugao wa kujulisha mitume wake kama amefufuliwa. Kupitia ile mambo yote, Yesu alimusaidia aone kama ni wa maana kwa Yehova!—Yoh. 20:11-18.
12. Juu ya nini Lidia alijisikia sawa vile hakuna mwenye anaweza kumupenda?
12 Sawa tu Maria Magdalene, leo batu mingi banaonaka kama hakuna mwenye anaweza kubapenda. Lidia, dada moya wa mu Espanye anasema kama, mbele hata azaliwe mama yake alikuwa nafikiria kutosha mimba yake. Na hata, anakumbuka vile wakati alikuwa mutoto mama yake hakumuhangaikia na alikuwa namusema mubaya. Lidia anasema hivi: “Mu maisha nilitamani sana bengine banikubali na banipende. Lakini niliogopa kama hakuna mwenye atanipendaka juu mama yangu alinisadikisha kama nilikuwa mutu mubaya.”
13. Nini njo ilisaidia Lidia aelewe kama Yehova anamuona kuwa wa maana?
13 Wakati Lidia alianza kujifunza Biblia mambo ilibadilika. Kusali, kusoma Biblia, na maneno na matendo ya ndugu na dada bilimusaidia aelewe kama Yehova anamuona kuwa wa maana. Anasema hivi: “Mara mingi bwana yangu ananiambiaka kama ananipenda sana. Na mara kwa mara, ananikumbushaka sifa zangu za muzuri. Na bandugu na dada bengine banafanyaka vile pia.” Mu kutaniko yenu muko mutu mwenye iko na lazima ya musaada juu ya kuelewa kama Yehova anamuona kuwa wa maana? Kama kuko mutu fulani mwenye anakukuya mu akili, fanya jambo fulani juu ya kumusaidia.
MAMBO YA KUFANYA JUU TUJIONE VILE YEHOVA ANATUONA
14. Namna gani 1 Samweli 16:7 inatusaidia kujua vile Yehova anatuonaka? (Ona pia kisanduku “Juu ya Nini Yehova Anaona Batu Yake Kuwa ba Maana?”)
14 Kumbuka kama, vile ulimwengu inakuona iko tofauti na vile Yehova anakuona. (Soma 1 Samweli 16:7.) Mu ulimwengu batu banaonaka mutu kuwa wa maana kama iko wa kiyana na iko na mwili ya muzuri, kama iko na makuta mingi, ao kama alisomaka sana. (Isa. 55:8, 9) Lakini haiko ile mambo njo Yehova anaangaliaka juu ya kuamua kama mutu ni wa maana ao hapana. Njo maana, juu ujue kama uko wa maana, uangalie njo byenye Yehova anaangaliaka hapana byenye ulimwengu inaangaliaka. Jambo moya yenye inaweza kukusaidia ni kusoma habari zenye ziko mu Biblia za batu benye balikuwa najiona kama habiko ba maana, sawa vile Eliya, Naomi, na Hana. Wakati uko nasoma, ujikaze kuona mambo yenye inaonyesha kama Yehova alibapenda sana. Jambo ingine yenye unaweza kufanya, ni kuandika mambo yenye Yehova alishakufanyia yenye inaonyesha kama anakupenda sana na anakuona kuwa wa maana. Tena unaweza kutafuta mu bichapo byetu habari zenye zilitayarishwa juu ya kusaidia batu benye banajionaka kuwa ba bure.c
15. Juu ya nini Yehova alimuona Danieli kuwa “mutu mwenye samani sana”? (Danieli 9:23)
15 Ukuwe hakika kama juu uko muaminifu, uko wa maana kwa Yehova. Mufano wa Danieli unaonyesha vile. Wakati moya hivi, saa Danieli alikuwaka na miaka zaidi ya 90, ‘alichoka sana’ na alivunjika moyo. (Da. 9:20, 21) Kwa hiyo, Yehova alituma malaika Gabrieli juu amutie moyo. Malaika Gabrieli alimukumbusha Danieli kama alikuwa “mutu mwenye samani sana” na kama Yehova alisikiliza sala zake. (Soma Danieli 9:23.) Juu ya nini Yehova aliona Danieli kuwa wa maana? Juu alikuwa na sifa za muzuri, kwa mufano alipenda haki na alikuwa muaminifu. (Eze. 14:14) Kama Yehova aliandikishaka ile habari mu Biblia, ni juu ya kutufariji. (Ro. 15:4) Njo maana ukuwe hakika kama, sawa Danieli Yehova anasikilizaka sala zako na anakuona kuwa wa maana juu unapenda haki na uko namutumikia kwa uaminifu.—Mik. 6:8, maelezo ya chini; Ebr. 6:10.
16. Ni nini inaweza kukusaidia umuone Yehova kuwa Baba mwenye upendo?
16 Umuone Yehova kuwa Baba mwenye anakupenda. Kusudi ya Yehova haiko kutafuta-tafuta makosa mu weye, lakini anapenda njo kukusaidia. (Zb. 130:3; Mt. 7:11; Lu. 12:6, 7) Kufikiri sana juu ya ile, kulishasaidia batu mingi benye balikuwa najiona kuwa ba bure. Kwa mufano, Michelle, dada moya wa Espanye alijiona kuwa wa bure juu kwa miaka mingi bwana yake alikuwa namuzarau na kumutukana. Michelle anasema hivi: “Kama ninajiona wa bure, ninapimaka kuwazia vile Yehova ananibeba mu mikono yake, ananionyesha upendo, na kunilinda.” (Zb. 28:9) Lauren, wa mu Afrika ya kusini, yeye anajiambiaka hivi: “Kama Yehova alinikokota kwake kwa kamba za upendo, amenisaidia niendelee kuwa rafiki yake hii miaka yote, na hata amenitumikisha juu ya kufundisha bengine, ni kusema niko tu wa maana kwake.”—Ho. 11:4.
17. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe hakika kama Yehova anakukubali? (Zaburi 5:12) (Ona pia picha.)
17 Ukuwe hakika kama Yehova anakukubali. (Soma Zaburi 5:12.) Daudi alilinganisha kukubaliwa na Yehova na “ngao kubwa” yenye inalinda batu benye haki. Sawa vile ngao inalindaka mutu, kujua kama Yehova anatukubali na kututegemeza kunaweza kutulinda juu mawazo ya kujiona kuwa ba bure isitutawale. Sasa nini itatusaidia tukuwe hakika kama Yehova anatukubali? Sawa vile tulishaona, Biblia njo njia moya yenye Yehova anatumikishaka juu ya kutuhakikishia kama anatukubali. Lakini anatumikishaka pia bazee, barafiki yetu ba karibu, na batu bengine juu ya kutukumbusha kama tuko ba maana kwake. Sasa tunapaswa kufanya nini kama mutu anatuambia maneno yenye kutia moyo yenye inatusaidia tujione kuwa ba maana?
Kujua kama Yehova anatukubali kunaweza kutusaidia tusijione kuwa batu ya bure (Ona fungu ya 17)
18. Juu ya nini unapaswa kukubali wakati bengine banakupongeza?
18 Wakati batu benye banakujua na kukupenda banakupongeza, ukuwe tayari kukubali. Ukumbuke kama Yehova anaweza kubatumia juu ya kukusaidia ukuwe hakika kama anakukubali. Michelle, mwenye tulizungumuzia anasema hivi: “Pole kwa pole, niko najifunza kuitika kwa moyo wote maneno ya kutia moyo yenye bengine bananiambia. Haiko mwepesi, lakini ninajua kama Yehova anapenda nifanye vile.” Bazee pia bamesaidia Michelle aone kama Yehova anamukubali. Leo Michelle ni painia na anasaidiaka kazi fulani za Beteli na iko ku nyumba.
19. Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana?
19 Kwa upendo Yesu anatukumbusha kama tuko ba maana sana kwa Baba yetu wa mbinguni. (Lu. 12:24) Kwa hiyo tukuwe hakika kama Yehova anatuona kuwa ba maana. Tusisaabu ile hata siku moya! Na tufanye yetu yote juu ya kusaidia bengine baone kama Yehova anabaona kuwa ba maana!
WIMBO 139 Wazia Uko mu Dunia Mupya
a Majina fulani imebadilishwa.
b Inawezekana Maria Magdalene alikuwa kati ya banamuke benye balisafiri pamoya na Yesu. Bale banamuke balitumia bitu yabo juu ya kusaidia kutimiza mahitaji ya Yesu na mitume wake.—Mt. 27:55, 56; Lu. 8:1-3.