Siku ya Yenga, 27 Mwezi wa 7
Uweze kutia moyo . . . na kukaripia.—Tit. 1:9.
Ili kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho, uko na lazima ya kujifunza ufundi fulani wa maana. Ile itakusaidia kutimiza migao yako mu kutaniko, kupata kazi ya kukutegemeza weye na familia yako, na kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na wengine. Kwa mufano, ujifunze kusoma na kuandika muzuri. Biblia inasema kama mutu mwenye furaha na mwenye anapata matokeo ya muzuri anapitisha wakati kila siku na iko anasoma na kufikiri sana juu ya Neno ya Mungu. (Zb. 1:1-3) Kwa kusoma Biblia kila siku, atafikia kujua namna ya Yehova ya kuona mambo, na ile inaweza kumusaidia kufikiri muzuri. (Mez. 1:3, 4) Ndugu na dada wako na lazima ya wanaume wenye uzoefu wa kuwapatie maagizo na mashauri yenye kutegemea Biblia. Kujua kusoma na kuandika muzuri kunaweza kukusaidia utayarishe hotuba na maelezo yenye kujenga. Ile inaweza pia kukusaidia kuandika maelezo fulani ya maana wakati uko unajifunza Biblia, ile mambo yenye uliandika inaweza kukusaidia kujenga imani yako na kutia wengine moyo. w23.12 26-27 fu. 9-11
Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 7
Ule mwenye kuwa katika umoja na ninyi ni mukubwa kuliko ule mwenye kuwa katika umoja na ulimwengu.—1 Yo. 4:4.
Wakati unaogopa, utafakari juu ya mambo yenye Yehova atafanya wakati wenye kuya wakati Shetani hatakuwa tena. Onyesho fulani ku mukusanyiko wa eneo wa 2014, ulionyesha baba fulani mwenye alikuwa nazungumuza na familia yake juu ya namna 2 Timoteo 3:1-5 inaweza kusomwa ikiwa ilikuwa inatabiri namna mambo itakuwa mu Paradiso: “Mu ulimwengu mupya mutakuwa nyakati za furaha. Kwa maana watu watakuwa wenye kupendana, wenye kupenda mambo ya kiroho, wenye kiasi, wanyenyekevu, wenye kumusifu Mungu, wenye kutii wazazi, wenye shukrani, washikamanifu, wenye kupenda sana watu wa familia yao, wenye kupenda makubaliano, wenye kusema mambo ya muzuri juu ya wengine, wenye kujizuia, wapole, wenye kupenda wema, wenye kutumainika, wenye kuwa tayari kusikia, wenye kujishusha, wenye kumupenda Mungu kuliko kupenda raha, wenye wanachochewa na ushikamanifu kwa Mungu; na weye ushikamane na watu wa namna ile.” Unazungumuzaka na watu wa familia yako ao waamini wenzako juu ya namna maisha itakuwa mu ulimwengu mupya? w24.01 6 fu. 13-14
Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 7
Nimekukubali.—Lu. 3:22.
Inatia moyo sana kujua kama Yehova anakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema: “Yehova anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Lakini, wakati fulani kuko Wakristo wenye wanaweza kuvunjika moyo na kujiuliza hivi: ‘Yehova ananikubali na miye?’ Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wa zamani walijiuliza pia vile wakati fulani. (1 Sa. 1:6-10; Yob. 29:2, 4; Zb. 51:11) Biblia inaonyesha wazi kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kukubaliwa na Yehova. Namna gani? Tunapaswa kukubali Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Kwa kufanya vile tunaonyesha waziwazi kama tumetubu zambi zetu na tumemuahidi Mungu kama tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi sana wakati tunafanya ile mambo ili kuwa marafiki wake wa karibu. Wakati tunaendelea kufanya yetu yote ili kuheshimia naziri yetu ya kujitoa kwake, Yehova anatukubali na kutuona kuwa marafiki wake.—Zb. 25:14. w24.03 26 fu. 1-2