Yobu
29 Yobu akaendelea na hotuba* yake, kwa kusema:
2 “Ingekuwa muzuri kama ningekuwa kama vile nilikuwa katika ile miezi ya zamani,
Katika siku zenye Mungu alikuwa ananilinda,
3 Wakati alifanya taa yake iangaze juu ya kichwa changu,
Wakati nilitembea katika giza kwa musaada wa mwangaza wake,+
4 Wakati nilikuwa na* nguvu za ujana,
Wakati urafiki pamoja na Mungu ulikuwa wazi katika hema yangu,+
5 Wakati Mweza-Yote alikuwa angali pamoja na mimi,
Wakati watoto* wangu wote walikuwa wananizunguka pande zote,
6 Wakati miguu yangu ilinawishwa katika siagi,
Na miamba ilinimwangia mito midogo ya mafuta.+
7 Wakati nilizoea kuenda kwenye mulango mukubwa wa muji+
Na kukaa kwenye kiti changu katika kiwanja cha watu wote,+
8 Vijana wanaume walikuwa wananiona na kuenda pembeni,*
Na hata wazee walikuwa wanasimama na kubakia wima.+
9 Wakubwa walijizuia kusema;
Walikuwa wanatia mukono wao kwenye kinywa chao.
10 Sauti za watu wa maana zilinyamazishwa;
Ulimi wao ulishikamana na sehemu ya juu ya kinywa chao.
11 Kila mutu mwenye alinisikia alikuwa ananisifu,
Na wale wenye waliniona walikuwa wanashuhudia kwa ajili yangu.
12 Kwa maana nilikuwa ninaokoa maskini mwenye kulilia musaada,+
Na mutoto mwenye hana baba na mutu yeyote mwenye hakukuwa na mutu wa kumusaidia.+
14 Nilivaa haki kama nguo;
Haki yangu ilikuwa kama kanzu* na kilemba.
15 Nilikuwa macho kwa vipofu
Na miguu kwa vilema.
18 Nilizoea kusema, ‘Nitakufia ndani ya nyumba yangu mwenyewe,*+
Na siku zangu zitakuwa nyingi kama chembe za muchanga.
19 Mizizi yangu itaenea ndani ya maji,
Na umande utakaa usiku wote kwenye matawi yangu.
20 Utukufu wangu unafanywa kuwa mupya kila wakati,
Na upinde katika mukono wangu utaendelea kurusha mishale.’
21 Watu walikuwa wananisikiliza kwa hamu,
Walingojea kimya mashauri yangu.+
22 Wakati nilimaliza kusema, hawakukuwa na neno lingine la kusema;
Maneno yangu yalikuwa yanaanguka polepole* katika masikio yao.
23 Waliningojea kama vile wanangojea mvua;
Walifungua kinywa chao wazi kama vile wanangojea mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho.+