Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w23 Mwezi wa 11 uku. 20-25
  • Yehova Atajibia Sala Zangu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Atajibia Sala Zangu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUNAWEZA KUTAZAMIA NINI KUTOKA KWA YEHOVA?
  • MAMBO YENYE YEHOVA ANATAZAMIA KUTOKA KWETU
  • JUU YA NINI INAWEZA KUWA LAZIMA TUREKEBISHE MAMBO YENYE TUNAOMBA?
  • Namna Yehova Anajibiaka Sala Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Namna ya Kufanya Sala Zetu Zikuwe Muzuri Zaidi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
w23 Mwezi wa 11 uku. 20-25

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

Yehova Atajibia Sala Zangu?

“Mutaniita na kuja na kusali kwangu, na nitawasikiliza.” —YER. 29:12.

WIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu

KIFUPI YA HABARIa

1-2. Juu ya nini tunaweza kuwaza kama Yehova haiko najibia sala zetu?

“PATA furaha nyingi sana katika Yehova, naye atakutimizia tamaa za moyo wako.” (Zb. 37:4) Hii ni ahadi ya ajabu sana! Lakini, je, tunapaswa kutazamia kama Yehova atatupatia palepale kila kitu yenye tunamuomba? Juu ya nini tufikirie hii ulizo? Fikiria hali zenye kufuata. Dada mwenye hayaolewa anasali juu aende ku Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, lakini miaka inapita na hayaalikwa tu. Ndugu kijana anaomba Yehova amusaidie juu apone ugonjwa fulani ili aweze kutumika zaidi mu kutaniko, lakini hali yake ya afya haibadilike. Wazazi fulani wanasali juu mutoto wao aendelee kubakia katika kweli, lakini mutoto wao anaacha kumutumikia Yehova.

2 Pengine na weye ulimuomba Yehova jambo fulani, lakini hauyaipata. Ile inaweza kufanya uwaze kama Yehova anajibiaka sala za wengine hapana zako. Ao unaweza kuwaza kama pengine umefanya jambo fulani ya mubaya. Dada mwenye kuitwa Janiceb aliwaza vile. Yeye na bwana yake walisali kuhusu tamaa yao ya kutumikia ku Beteli. Anasema hivi: “Nilikuwa hakika kama hawatakawia kutuita ku Beteli.” Lakini miezi ikageuka miaka na Janice na bwana yake walikuwa tu hawayaalikwa ku Beteli. Janice anasema hivi: “Nilisikia mubaya na nilivurugika. Nilijiuliza nilifanya nini yenye ilimuhuzunisha Yehova. Nimesali sana juu ya kuenda ku Beteli. Juu ya nini Yehova hayajibia sala zangu?”

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Wakati fulani tunaweza kujiuliza kama Yehova iko nasikiliza sala zetu. Hata wanaume fulani waaminifu wa zamani walijiuliza vile. (Yob. 30:20; Zb. 22:2; Hab. 1:2) Ni nini inaweza kukuhakikishia kama Yehova atajibia sala zako? (Zb. 65:2) Ili kujibu ile ulizo, kwanza tutakuwa na lazima ya kujibia maulizo yenye kufuata: (1) Tunaweza kutazamia nini kutoka kwa Yehova? (2) Yehova anatazamia nini kutoka kwetu? (3) Juu ya nini inaweza kuwa lazima turekebishe mambo fulani yenye tunamuomba?

TUNAWEZA KUTAZAMIA NINI KUTOKA KWA YEHOVA?

4. Kulingana na Yeremia 29:12, Yehova anaahidi kufanya nini?

4 Yehova anaahidi kama atasikiliza sala zetu. (Soma Yeremia 29:12.) Mungu wetu anapenda watumishi wake waaminifu, kwa hiyo hawezi kufunga masikio wakati wanasali. (Zb. 10:17; 37:28) Lakini, ile haimaanishe kama atatupatia kila kitu yenye tunamuomba. Inaweza kuomba tungoye dunia mupya juu tupate mambo fulani yenye tunamuombaka.

5. Yehova anaangaliaka nini wakati iko nasikiliza sala zetu? Fasiria.

5 Yehova anaangaliaka namna mambo yenye tunamuomba inapatana na kusudi yake. (Isa. 55:8, 9) Kati ya mambo yenye kusudi yake itatimiza ni kujaza dunia wanaume na wanamuke wenye furaha na umoja chini ya utawala wake. Lakini Shetani anasema kama wanadamu watakuwa na maisha ya muzuri zaidi kama wanajiongoza wao wenyewe. (Mwa. 3:1-5) Ili kuonyesha kama Shetani anasema uongo, Yehova ameruhusu wanadamu wajiongoze. Lakini utawala wa wanadamu unaleta magumu mingi yenye iko natufikia leo. (Muh. 8:9) Tunaelewa kama Yehova hatatosha ile magumu yote kwa sasa. Akifanya vile watu fulani wanaweza kuwaza kama wanadamu wanajitawala muzuri na kama wanaweza kumaliza matatizo ya watu.

6. Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama siku zote Yehova anatendaka kwa upendo na kwa haki?

6 Yehova anaweza kujibia ombi za kufanana mu njia tofauti. Kwa mufano, wakati Mufalme Hezekia alikuwa mugonjwa sana alimulilia Yehova amusaidie apone. Na Yehova alijibia sala yake kwa kumuponyesha. (2 Fa. 20:1-6) Lakini wakati mutume Paulo alimulilia Yehova aondoe “mwiba katika mwili” wake, wenye inawezekana ulikuwa ugonjwa fulani, Yehova hakuondoa ile mwiba. (2 Ko. 12:7-9) Fikiria pia mufano wa mutume Yakobo na mutume Petro. Mufalme Herode alitafuta kuwaua wote wawili. Kutaniko ilisali kwa ajili ya Petro na inawezekana kwa ajili ya Yakobo pia. Hata vile, Yakobo aliuawa, lakini Petro aliokolewa kwa muujiza. (Mdo. 12:1-11) Tunaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini Yehova alimuokoa Petro lakini hapana Yakobo?’ Biblia haijibie ile ulizo.c Lakini tunaweza kuwa hakika kama Yehova “hana ukosefu wa haki hata kidogo.” (Kum. 32:4) Na tunajua kama Yehova aliwapenda wote wawili. (Ufu. 21:14) Wakati fulani tunaweza kumuomba Yehova, lakini mambo inatokea mu namna yenye hatukutazamia. Lakini juu tunajua kama Yehova ni mwenye upendo na ni mwenye haki sikuzote, tuko hakika kama kila mara anajibia sala zetu mu njia yenye kufaa.—Yob. 33:13.   

7. Tunapaswa kuepuka nini, na juu ya nini?

7 Tunajikaza kuepuka kulinganisha hali yetu na ya wengine. Kwa mufano, tunaweza kumuomba Yehova kuhusu jambo fulani, lakini hajibie vile tulimuomba. Kisha, tunapata habari kama mutu mwingine alimuomba Yehova kuhusu ileile jambo na inaonekana kama Yehova alimujibia vile alimuomba. Jambo ya vile ilifikia dada mwenye kuitwa Anna. Alimuomba Yehova asaidie bwana yake Matthew, mwenye alikuwa na ugonjwa wa kansere, apone. Wakati uleule, dada wawili wenye kukomaa walikuwa pia na ugonjwa wa kansere. Anna alisali sana kwa ajili ya Matthew na wale dada. Wale dada wawili walipona, lakini Matthew akakufa. Ku mwanzo, Anna alijiuliza ikiwa Yehova njo alisaidia wale dada wapone. Na kama ni yeye, juu ya nini hakujibia sala yake ya kuomba bwana yake naye apone? Kusema kweli, hatujue namna wale dada wawili walipona. Lakini tunajua kama Yehova anapanga kumaliza kabisa mateso yetu yote, na kama anatamani kufufua marafiki wake wenye wamekufa.—Yob. 14:15.

8. (a) Kulingana na Isaya 43:2, Yehova anatutegemeza namna gani? (b) Namna gani sala inaweza kutusaidia wakati tunapambana na magumu ya nguvu? (Ona video Sala Inatusaidia Tuvumilie.)

8 Yehova atatutegemeza sikuzote. Juu Yehova ni Baba yetu mwenye upendo, hafurahi wakati anatuona tuko nateseka. (Isa. 63:9) Hata vile, haiko mateso yote njo Yehova anazuiaka isitupate, mateso yenye inaweza kulinganishwa na mito ao moto. (Soma Isaya 43:2.) Lakini, anatuahidi kama atatusaidia ‘kupita’ mu ile mateso. Na hataruhusu ile mateso iharibu uhusiano wetu pamoya naye. Yehova anatupatia pia roho yake takatifu yenye nguvu ili kutusaidia kuvumilia. (Lu. 11:13; Flp. 4:13) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama sikuzote tutakuwa na yote yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia na kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova.d

MAMBO YENYE YEHOVA ANATAZAMIA KUTOKA KWETU

9. Kulingana na Yakobo 1:6, 7, juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yehova atatusaidia?

9 Yehova anatazamia tumutumainie. (Ebr. 11:6) Wakati fulani tunaweza kuona kama magumu yetu ni ya nguvu sana, yenye hatuwezi kuvumilia. Tunaweza kuanza kujiuliza ikiwa Yehova atatusaidia kabisa. Lakini Biblia inatuhakikishia kama kupitia nguvu ya Mungu tunaweza “kupanda ukuta.” (Zb. 18:29) Kwa hiyo, kuliko kuwa na mashaka tunapaswa kusali kwa imani kabisa na kuwa hakika kabisa kama Yehova atajibia sala zetu.—Soma Yakobo 1:6, 7.

10. Toa mufano wenye kuonyesha namna tunaweza kutenda kulingana na sala zetu.

10 Yehova anatazamia tutende kulingana na sala zetu. Kwa mufano, ndugu anaweza kumuomba Yehova amusaidie ili wamupatie siku fulani ku kazi juu aweze kuenda ku mukusanyiko wa eneo. Yehova anaweza kujibia ile sala namna gani? Anaweza kumupatia ule ndugu uhodari wenye iko nao lazima juu aweze kuzungumuza na mukubwa wake wa kazi. Lakini ule ndugu naye anapaswa kufanya jambo fulani; anapaswa kukamata hatua ya kuomba mukubwa wake wa kazi ruhusa. Pengine itaomba afanye vile tena na tena. Anaweza hata kukamata mipango ya kutafuta mufanyakazi mwenzake mwenye anaweza kutumika pa nafasi yake wakati ataenda ku mukusanyiko. Na, kama ni lazima, anaweza hata kupendekeza wasimulipe ile wakati yenye hatatumika.

11. Juu ya nini tunapaswa kusali tena na tena kuhusu mahangaiko yetu

11 Yehova anatazamia tusali tena na tena kuhusu mahangaiko yetu. (1 Te. 5:17) Yesu alionyesha kama Mungu hatatupatia palepale mambo fulani yenye tunamuomba. (Lu. 11:9) Kwa hiyo, tusichoke! Tusali tena na tena kwa moyo wote. (Lu. 18:1-7) Wakati tunaendelea kusali kuhusu jambo fulani, tunaonyesha Yehova kama tuko kabisa na lazima ya ile jambo. Tunaonyesha pia kama tuko na imani kuwa iko na uwezo wa kutusaidia.

JUU YA NINI INAWEZA KUWA LAZIMA TUREKEBISHE MAMBO YENYE TUNAOMBA?

12. (a) Tunapaswa kujiuliza ulizo gani kuhusu mambo yenye tunamuomba Yehova, na juu ya nini? (b) Namna gani tunaweza kuhakikisha kama sala zetu zinaonyesha kuwa tunamuheshimia Yehova? (Ona kisanduku “Mambo Yenye Ninaomba, Inaonyesha Kama Ninaheshimia Yehova?”)

12 Kama hatupate mambo yenye tuliomba mu sala yetu, tunaweza kujiuliza hii maulizo tatu. Ya kwanza, ‘Jambo yenye niko naombo njo yenye inafaa kabisa?’ Mara mingi tunawazaka kama tunajua jambo yenye inatufaa kabisa. Lakini pengine mambo yenye tuko naomba haiko njo yenye itatusaidia kabisa. Kwa mufano, kama tuko nasali juu ya tatizo fulani, kunaweza kuwa njia ya muzuri zaidi ya kuishugulikia kuliko ile yenye tuko naomba. Na inawezekana mambo fulani yenye tunaomba haipatane na mapenzi ya Yehova. (Lu. 11:9) Fikiria mufano wa wazazi wenye tulizungumuzia ku mwanzo. Walimuomba Yehova ahakikishe kama mutoto wao anabakia katika kweli. Ile inaweza kuonekana kuwa ombi yenye kufaa. Lakini Yehova hakazake mutu yeyote amutumikie. Anapenda siye wote, kutia ndani watoto wetu, tuchague kumutumikia. (Kum. 10:12, 13; 30:19, 20) Kwa hiyo, wazazi walipaswa njo kumuomba Yehova awasaidie waguse moyo wa mutoto wao ili mutoto wao achochewe kumupenda na kuwa rafiki yake.—Mez. 22:6; Efe. 6:4.

Mambo Yenye Ninaomba, Inaonyesha Kama Ninaheshimia Yehova?

Yehova ni Baba mwenye upendo mwenye anapenda kujibia maombi yetu. Lakini ni Muumbaji wetu pia na anastahili kuonyeshwa heshima. (Ufu. 4:11) Namna gani unaweza kuonyesha heshima Baba yako wa mbinguni wakati uko namuomba mambo fulani?

  • Uhakikishe kama mambo yenye unaomba inapatana na mapenzi ya Mungu na uko na nia ya muzuri. (1 Yo. 5:14) Sala zetu hazipaswe kuwa za uchoyo ni kusema, za kuomba tu mambo yenye tuko nayo lazima na mambo yenye tunapenda. Yakobo alionya Wakristo wa kwanza-kwanza kama hawangepata jibu ya sala zao ikiwa walisali “kwa kusudi la mubaya” ni kusema, kwa kujifikiria wao wenyewe.—Yak. 4:3.

  • Tusikuwe tunamulazimisha Yehova atupatie mambo yote yenye tunapenda. (Mt. 4:7) Ukuwe hakika kama Yehova anajua njia ya muzuri zaidi ya kujibia sala zako. Na wakati fulani, jibu yake inaweza kuwa tofauti na mambo yenye unatazamia.—Efe. 3:20.

  • Ukumbuke kumushukuru juu ya mambo yenye anakupatia kila siku. Wazia furaha yenye anasikia wakati unamushukuru sana juu ya musaada wenye amekutolea.—Kol. 3:15; 1 Te. 5:17, 18.

13. Kulingana na Waebrania 4:16, ni wakati gani njo Yehova atatusaidia? Fasiria.

13 Ulizo ya pili ya kujiuliza ni, ‘Huu njo wakati wa Yehova wa kujibia ombi yangu?’ Tunaweza kuona kama ni lazima sala zetu zijibiwe palepale. Lakini, Yehova njo anajua wakati wenye kufaa zaidi wa kutusaidia. (Soma Waebrania 4:16.) Wakati hatupate palepale kitu yenye tuko naomba tunaweza kuwaza kama jibu ya Yehova ni ‘Hapana.’ Lakini jibu inaweza kuwa ni ‘Hapana kwa sasa.’ Fikiria tena mufano wa ule ndugu kijana mwenye alisali ili apone. Yehova angemuponyesha kwa muujiza, Shetani angeweza kusema kama ule ndugu anaendelea kumutumikia Yehova juu tu alimuponyesha. (Yob. 1:9-11; 2:4) Zaidi ya ile, Yehova alishaweka wakati wenye ataponyesha magonjwa yote. (Isa. 33:24; Ufu. 21:3, 4) Mbele ile wakati ifike, hatuwezi kutazamia kama tutaponyeshwa kwa muujiza. Kwa hiyo, ule ndugu anaweza kumuomba Yehova amupatie nguvu na amupatie amani ya akili ili avumilie ugonjwa wake na aendelee kumutumikia kwa uaminifu.—Zb. 29:11.

14. Mufano wa Janice unakufundisha nini?

14 Kumbuka mufano wa Janice mwenye alisali kuhusu kutumikia ku Beteli. Ni kisha miaka tano njo alielewa namna Yehova alikuwa amejibia sala yake. Anasema hivi: “Yehova alitumia ile wakati ili kunifundisha na kunisaidia nikuwe Mukristo muzuri zaidi. Nilikuwa na lazima ya kumutumainia zaidi. Nilipaswa kufanya maendeleo mu namna yangu ya kufanya funzo ya kipekee. Nilipaswa kujifunza kuwa na furaha ya kweli, yenye haitegemee hali yenye niko ndani.” Janice na bwana yake walifikia kualikwa ili wafanye kazi ya muzunguko. Wakati Janice anakumbuka ile mambo, anasema hivi: “Yehova alijibia sala zangu, hata kama haikukuwa mu namna yenye nilitazamia. Ilinikamata wakati ili kuona kama alijibia sala yangu mu njia ya muzuri sana, lakini niko mwenye shukrani sana juu nilijionea upendo na wema wake.”

Picha: 1. Dada wawili kila mumoja iko najaza kipekee fomu ya Masomo ya Waeneza Injili. Kila mumuja anasali mbele ya kutuma fomu yake. 2. Kwenye Jumba ya Ufalme, moja kati ya wale dada anaonyesha kwa furaha marafiki wake, kutia ndani ule dada mwengine mwenye naye alijaza fumu, barua ya kumualika ku masomo. 3. Dada mwenye akualika kumasoma anasali kwa Yehova na kisha anandika barua. Baadaye anahubiri mu inchi ya kigeni na anatumika mu kazi fulani ya ujenzi.

Ikiwa unaona kuwa Yehova hayajibia sala yako, sali juu ya mambo ingine (Ona fungu ya 15)f

15. Juu ya nini wakati fulani ni muzuri tusali juu ya mambo kwa ujumla? (Ona pia picha.)

15 Ulizo ya tatu ya kujiuliza ni, ‘Nisali juu ya jambo ingine?’ Hata kama ni muzuri kusali juu ya jambo moja yenye tuko nayo lazima, inaweza kuwa muzuri zaidi kusali kwa ujumla bila kutaya jambo moya tu ili tuweze kutambua mapenzi ya Yehova ni nini kwa ajili yetu. Fikiria mufano wa ule dada wenye alikuwa anasali juu aende ku Masomo ya Waeneza Injili wa Ufalme. Anapenda kusoma ile masomo juu aweze kutumikia fasi kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri. Kwa hiyo, wakati iko naendelea kusali ili aalikwe ku ile masomo, anaweza pia kumuomba Yehova amusaidie kutambua nafasi zingine za kupanua utumishi wake. (Mdo. 16:9, 10) Kisha anaweza kutenda kulingana na sala zake kwa kuuliza mwangalizi wa muzunguko kama kuko kutaniko ya karibu yenye kuwa na lazima ya mapainia zaidi. Ao anaweza kuandikia biro ya tawi ili ajue fasi kwenye kuko lazima ya wahubiri zaidi.e

16. Tunaweza kuwa hakika juu ya jambo gani?

16 Vile tumeona, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atajibia sala zetu mu njia ya upendo na yenye kufaa. (Zb. 4:3; Isa. 30:18) Wakati fulani inawezekana tusipate jibu yenye tulitazamia. Lakini Yehova hawezi kuzarau sala zetu hata siku moya. Anatupenda sana, na hawezi kutuacha hata kidogo. (Zb. 9:10) Kwa hiyo, endelea ‘kumutegemea [Yehova] nyakati zote,’ kwa kumumwangia moyo wako katika sala.—Zb. 62:8.

KUHUSU SALA ZETU, . . .

  • tunaweza kutazamia nini kutoka kwa Yehova?

  • Yehova anatazamia nini kutoka kwetu?

  • juu ya nini inaweza kuwa lazima turekebishe mambo fulani yenye tunamuomba Yehova

WIMBO 43 Sala ya Shukrani

a Hii habari itafasiria juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama kila siku Yehova atajibia sala zetu kwa upendo na mu njia yenye kufaa zaidi.

b Majina fulani yamebadilishwa.

c Soma habari “Unatumainia Njia ya Yehova ya Kufanya Mambo?” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2022, fu. 3-6.

d Ili kupata habari zaidi juu ya namna Yehova anatusaidia tuvumilie magumu ya nguvu, angalia ku jw.org video Sala Inatusaidia Tuvumilie.

e Juu ya kujua maagizo kuhusu kutumikia mu eneo ya tawi ingine, soma kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova, sura ya 10, fu. 6-9.

f MAFASIRIO YA PICHA : Dada wawili wanasali mbele ya kujaza fomu ya kuenda ku Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Kisha mumoja wao anaalikwa, na mwingine hapana. Kuliko kuvunjika moyo, dada mwenye hakualikwa anasali kwa Yehova juu amusaidie atambua nafasi zingine za kupanua utumishi wake. Kisha anaandikia biro ya tawi barua ili kuwajulisha kama iko tayari kutumikia fasi kwenye kuko uhitaji.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine