Isaya
55 Mukuje, ninyi wote wenye kiu,+ mukuje kwenye maji!+
Ninyi wenye hamuna feza, mukuje, mununue na mukule!
Ndiyo, mukuje, mununue divai na maziwa+ bila feza na bila garama.+
2 Sababu gani munaendelea kulipa feza kwa ajili ya kitu chenye hakiko mukate,
Na sababu gani mutumie mapato yenu* kwa ajili ya kitu chenye hakishibishe?
Munisikilize kwa uangalifu, na mukule mambo ya muzuri,+
Na mutapata* furaha nyingi katika vitu vyenye kujenga mwili kabisa.*+
3 Mutege sikio na mukuje kwangu.+
Musikilize, na mutaendelea* kuishi,
Na bila kusita nitafanya agano la milele pamoja na ninyi+
Kulingana na maonyesho ya upendo mushikamanifu kwa Daudi, yenye ni ya uaminifu.*+
5 Angalia! Utaita taifa lenye haujue,
Na watu wa taifa wenye hawakukujua watakukimbilia
Kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ Mutakatifu wa Israeli,
Kwa sababu atakutukuza.+
6 Mumutafute Yehova wakati anaweza kupatikana.+
Mumuite wakati angali karibu.+
Na mutu mubaya mawazo yake;
Na amurudilie Yehova, mwenye atamuonyesha rehema,+
8 “Kwa maana mawazo yangu hayako mawazo yenu,+
Na njia zenu haziko njia zangu,” ni vile Yehova anasema.
9 “Kwa maana kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia,
Ni vile njia zangu ziko juu kuliko njia zenu,
Na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.+
10 Kwa maana kama vile mvua na teluji* inamwangika kutoka mbinguni
Na hairudie kule mupaka ilowanishe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,
Na kupatia mbegu mupandaji na kupatia mukate mwenye kula,
11 Ni vile neno langu lenye kutoka katika kinywa changu litakuwa.*+
Halitarudia kwangu bila matokeo,+
Lakini hakika litatimiza jambo lolote lenye kunipendeza,*+
Na hakika litafanikiwa katika mambo yenye nimelituma kufanya.
Milima na vilima vitachangamuka mbele yenu kwa vigelegele vya shangwe,+
Na miti yote ya pori itapiga mikono.+