Zaburi
3 Kwa maana atakuokoa usinaswe na mtego wa mwindaji wa ndege,
Kutoka kwa ugonjwa wa kuambukiza unaoangamiza.
4 Kwa manyoya yake atakufunika,
Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+
Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*
5 Hutaogopa vitisho vya usiku,+
Wala mshale unaoruka mchana,+
6 Wala ugonjwa wa kuambukiza unaonyemelea gizani,
Wala maangamizi yanayoharibu wakati wa adhuhuri.
8 Utayaona tu kwa macho yako
Unaposhuhudia adhabu* ya waovu.
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”
Umemfanya Aliye Juu Zaidi kuwa makao* yako;+
10 Hutapatwa na msiba,+
Na hakuna pigo litakalokaribia hema lako.
13 Utamkanyaga mwanasimba na swila;
Utamkanyagia chini simba mwenye manyoya marefu shingoni na nyoka mkubwa.+
14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamwokoa.+
Nitamlinda kwa sababu analijua* jina langu.+
15 Ataniita, nami nitamjibu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamwokoa na kumtukuza.