Zaburi
97 Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia na iwe na shangwe.+
Na visiwa vyake vingi vishangilie.+
4 Umeme wake wa radi huiangazia nchi;
Dunia huona na kutetemeka.+
5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Yehova,+
Mbele za Bwana wa dunia yote.
6 Mbingu hutangaza uadilifu wake,
Na mataifa yote huona utukufu wake.+
7 Wote wanaoabudu sanamu yoyote ya kuchongwa na waaibishwe,+
Wale wanaojigamba kuhusu miungu yao ya ubatili.+
Mwinamieni,* enyi miungu yote.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;
Umekwezwa juu zaidi ya miungu mingine yote.+
10 Enyi mnaompenda Yehova, chukieni maovu.+
11 Nuru imemwangazia mwadilifu+
Na shangwe walio wanyoofu moyoni.
12 Shangilieni kwa sababu ya Yehova, enyi waadilifu,
Na mlishukuru jina lake takatifu.*