Methali
21 Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova.+
Yeye huuelekeza mahali popote anapopenda.+
3 Kutenda mambo manyoofu na ya haki
Humpendeza Yehova zaidi kuliko dhabihu.+
4 Macho ya kiburi na moyo wenye majivuno
—Taa inayowaongoza waovu ni dhambi.+
5 Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio,*+
Lakini wote walio na haraka kwa hakika watakuwa maskini.+
7 Ukatili wa waovu utawafagilia mbali,+
Kwa maana wanakataa kutenda haki.
8 Njia ya mtu mwenye hatia imepinda,
Lakini matendo ya mtu safi yamenyooka.+
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa, asiye na uzoefu hupata hekima zaidi,
12 Aliye Mwadilifu huichunguza nyumba ya mwovu;
Huwapindua waovu na kuwaangamiza.+
13 Yeyote anayeziba sikio lake asisikie kilio cha mtu wa hali ya chini
Yeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+
15 Mwadilifu hushangilia kutenda haki,+
Lakini hilo ni jambo baya sana kwa watenda maovu.
16 Mtu anayetangatanga kutoka kwenye njia ya ufahamu
Atapumzika katika kundi la wale waliokufa ambao hawana uwezo.+
18 Mwovu ni fidia ya mwadilifu,
Na mwenye hila atachukuliwa badala ya mnyoofu.+
20 Hazina yenye thamani na mafuta hupatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+
21 Yeyote anayefuatia uadilifu na upendo mshikamanifu
Atapata uzima, uadilifu, na utukufu.+
22 Mtu mwenye hekima anaweza kupanda katika* jiji la watu wenye nguvu
Na kudhoofisha nguvu wanazotumaini.+
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake
Anajiepusha na taabu.+
24 Mtu mwenye kimbelembele, anayejigamba kwa kiburi, hivyo ndivyo unavyomwita
Mtu anayetenda kwa kimbelembele bila kujali.+
25 Anachotamani mtu mvivu kitamuua,
Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+
26 Anatamani kwa pupa mchana kutwa,
Lakini mwadilifu hutoa, hawanyimi wengine chochote.+
27 Dhabihu ya mwovu inachukiza.+
Sembuse anapoitoa akiwa na nia ovu!*
30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+