Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mathayo—Yaliyomo

      • Yohana Mbatizaji ahubiri (1-12)

      • Yesu abatizwa (13-17)

Mathayo 3:1

Marejeo

  • +Yoh 1:6
  • +Mk 1:3, 4; Lu 3:3-6

Mathayo 3:2

Marejeo

  • +Mt 4:17

Mathayo 3:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Mk 1:2; Yoh 1:23
  • +Isa 40:3

Mathayo 3:4

Marejeo

  • +2Fa 1:8
  • +Mk 1:6

Mathayo 3:5

Marejeo

  • +Mk 1:5

Mathayo 3:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akawatumbukiza; akawazamisha.”

Marejeo

  • +Mk 1:9

Mathayo 3:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nyoka-vipiri.”

Marejeo

  • +Mk 12:18; Lu 7:30
  • +Mt 12:34
  • +Mt 23:33; Lu 3:7-9; 21:23

Mathayo 3:9

Marejeo

  • +Yoh 8:33, 39

Mathayo 3:10

Marejeo

  • +Mt 7:19; Lu 13:6-9

Mathayo 3:11

Marejeo

  • +Mdo 19:4
  • +Yoh 1:15, 27
  • +Mk 1:7, 8; Yoh 1:33; Mdo 2:1, 4; 1Ko 12:13
  • +Lu 3:16, 17

Mathayo 3:12

Marejeo

  • +Mal 4:1

Mathayo 3:13

Marejeo

  • +Mk 1:9

Mathayo 3:16

Marejeo

  • +Lu 3:21
  • +Isa 11:2; Mk 1:10, 11; Lu 4:18; Yoh 1:32

Mathayo 3:17

Marejeo

  • +Yoh 12:28
  • +Zb 2:7; Lu 9:35
  • +Isa 42:1; Mt 17:5; Lu 3:22

Jumla

Mt. 3:1Yoh 1:6
Mt. 3:1Mk 1:3, 4; Lu 3:3-6
Mt. 3:2Mt 4:17
Mt. 3:3Mk 1:2; Yoh 1:23
Mt. 3:3Isa 40:3
Mt. 3:42Fa 1:8
Mt. 3:4Mk 1:6
Mt. 3:5Mk 1:5
Mt. 3:6Mk 1:9
Mt. 3:7Mk 12:18; Lu 7:30
Mt. 3:7Mt 12:34
Mt. 3:7Mt 23:33; Lu 3:7-9; 21:23
Mt. 3:9Yoh 8:33, 39
Mt. 3:10Mt 7:19; Lu 13:6-9
Mt. 3:11Mdo 19:4
Mt. 3:11Yoh 1:15, 27
Mt. 3:11Mk 1:7, 8; Yoh 1:33; Mdo 2:1, 4; 1Ko 12:13
Mt. 3:11Lu 3:16, 17
Mt. 3:12Mal 4:1
Mt. 3:13Mk 1:9
Mt. 3:16Lu 3:21
Mt. 3:16Isa 11:2; Mk 1:10, 11; Lu 4:18; Yoh 1:32
Mt. 3:17Yoh 12:28
Mt. 3:17Zb 2:7; Lu 9:35
Mt. 3:17Isa 42:1; Mt 17:5; Lu 3:22
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mathayo 3:1-17

Kulingana na Mathayo

3 Siku hizo Yohana+ Mbatizaji alikuja kuhubiri+ katika nyika ya Yudea, 2 akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”+ 3 Kwa kweli, huyu ndiye anayezungumziwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.’”+ 4 Yohana alivaa mavazi yaliyofumwa kwa manyoya ya ngamia na alijifunga mshipi wa ngozi kiunoni.+ Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.+ 5 Basi watu kutoka Yerusalemu na Yudea yote na maeneo yote yaliyokuwa karibu na Yordani walikuwa wakimwendea,+ 6 naye akawabatiza* katika Mto Yordani,+ nao wakaungama dhambi zao waziwazi.

7 Alipoona Mafarisayo na Masadukayo+ wengi wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Enyi uzao wa nyoka,*+ ni nani amewaonya ili mkimbie ghadhabu inayokuja?+ 8 Basi zaeni matunda yanayoonyesha toba. 9 Msithubutu kujiambia, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia, Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwenye mawe haya. 10 Tayari shoka limewekwa kwenye mzizi wa miti. Basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.+ 11 Mimi ninawabatiza kwa maji kwa sababu mmetubu,+ lakini yule anayekuja baada yangu ana nguvu kuliko mimi, nami sistahili kuvivua viatu vyake.+ Yeye atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+ 12 Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake, naye atausafisha kabisa uwanja wake wa kupuria, na kukusanya ngano yake katika ghala, lakini atayateketeza makapi kwa moto+ usioweza kuzimwa.”

13 Ndipo Yesu akatoka Galilaya na kwenda Yordani ili abatizwe na Yohana.+ 14 Lakini Yohana akajaribu kumzuia, akisema: “Mimi ndiye ninayehitaji kubatizwa na wewe, nawe unakuja kwangu?” 15 Yesu akamjibu: “Acha iwe hivyo wakati huu, kwa maana kwa njia hiyo inafaa tufanye yote yaliyo ya uadilifu.” Ndipo Yohana akaacha kumzuia. 16 Baada ya kubatizwa, mara moja Yesu akainuka kutoka katika maji; na tazama! mbingu zikafunguliwa,+ naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikija juu yake.+ 17 Tazama! Pia, sauti ikasikika kutoka mbinguni+ ikisema: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa, ambaye nimemkubali.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki