Zaburi
Miktamu* ya Daudi.
16 Unilinde, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemuambia Yehova: “Wewe ni Yehova, Chanzo changu cha wema.
3 Na watakatifu wenye kuwa katika dunia,
Watukufu, ndio wananipendeza sana.”+
4 Wale wenye kufuatilia miungu mingine wanaongeza huzuni zao.+
Sitamwanga hata kidogo matoleo yao ya vinywaji ya damu,
Wala midomo yangu haitataja majina yao.+
5 Yehova ni fungu langu, fungu lenye niligawiwa,+ na kikombe changu.+
Unalinda uriti wangu.
6 Nafasi zenye kupendeza zimepimwa kwa ajili yangu.
Ndiyo, nimetosheka na uriti wangu.+
7 Nitamusifu Yehova, mwenye amenipa shauri.+
Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa yananirekebisha.*+
8 Ninamuweka Yehova mbele yangu kila wakati.+
Kwa sababu iko* kwenye mukono wangu wa kuume, sitatikiswa* hata kidogo.+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote iko na* shangwe.
Na ninakaa* kwa usalama.
10 Kwa maana hautaniacha* katika Kaburi.*+
Hautaruhusu mushikamanifu wako aone shimo.*+
11 Unanijulisha njia ya uzima.+