Isaya
Yakaribie; kisha yaseme.+
Tukuje pamoja kwa ajili ya hukumu.
2 Ni nani amemuinua mutu kutoka mahali jua linatokea,*+
Akimuita afuate miguu Yake* ili atimize haki,
Ili atie mataifa katika mukono wake
Na kumufanya atiishe wafalme?+
Mwenye anawafanya wakuwe mavumbi mbele ya upanga wake,
Kama majani ya kukauka yenye kupeperushwa na upepo mbele ya upinde wake?
3 Anawafuatilia, akipita bila kuzuiwa
Kwenye njia zenye miguu yake haijapitia.
4 Ni nani ametenda na kufanya jambo hili,
Akiita vizazi tangu mwanzo?
5 Visiwa vimeona jambo hilo na kuogopa.
Miisho ya dunia ilianza kutetemeka.
Wanakaribia na kuja mbele.
6 Kila mumoja anamusaidia mwenzake
Na kumuambia ndugu yake: “Ukuwe na nguvu.”
7 Kwa hiyo fundi anamutia nguvu fundi wa metali;+
Ule mwenye kulainisha kwa nyundo* ya chuma
Anamutia nguvu ule mwenye kupiga nyundo* kwenye fuawe,*
Anasema kuhusu kazi ya kuunganisha vyuma: “Iko muzuri.”
Kisha inapigiliwa misumari ili isianguke.
8 “Lakini wewe, Ee Israeli, uko mutumishi wangu,+
Wewe, Ee Yakobo, mwenye nimechagua,+
Uzao wa* Abrahamu rafiki yangu,+
9 Wewe, mwenye nilitosha kwenye miisho ya dunia,+
Na wewe, mwenye niliita kutoka sehemu zake za mbali zaidi.
10 Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.+
Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.+
Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia,+
Nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.’
11 Angalia! Wale wote wenye kuwaka kasirani juu yako watapatishwa haya na kufezeheshwa.+
Wale wenye kupigana na wewe watafanywa kuwa bure na wataharibiwa.+
12 Utatafuta watu wenye kupambana na wewe, lakini hautawapata;
Watu wenye kupigana na wewe watakuwa kama kitu chenye hakiko, kama kitu bure kabisa.+
13 Kwa maana mimi, Yehova Mungu wako, ninashika mukono wako wa kuume,
Ni mimi mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’+
14 Usiogope, wewe munyoo* Yakobo,+
Ninyi watu wa Israeli, nitawasaidia,” ni vile Yehova, Mukombozi wako,+ Mutakatifu wa Israeli, anasema.
15 “Angalia! Nimekufanya kuwa kifaa cha kupiga-piga nafaka,+
Kifaa kipya cha kupiga-piga nafaka chenye meno yenye makali pande mbili.
Utakanyanga milima na kuiponda
Na kufanya vilima kuwa kama maganda ya mbegu.
17 “Wenye uhitaji na maskini wanatafuta maji, lakini hakuna.
Ulimi wao umekauka kwa sababu ya kiu.+
Mimi, Yehova, nitawajibu.+
Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.+
Nitageuza jangwa kuwa kiziwa cha maji chenye matete
Na inchi yenye haina maji kuwa chemchemi za maji.+
19 Nitapanda muti wa mwerezi katika jangwa,
Muti wa mugunga* na muti wa muhadasi na muti wa musonobari.+
Nitapanda muti wa muberoshi katika jangwa tambarare,
Pamoja na muti wa mutizari na muti wa muvinje,+
20 Ili watu wote waone na kujua
Na kukaza uangalifu na kuelewa
Kwamba mukono wa Yehova umefanya vile,
Na Mutakatifu wa Israeli ameumba jambo hilo.”+
21 “Mulete kesi yenu ya hukumu,” ni vile Yehova anasema.
“Mujitetee,” ni vile Mufalme wa Yakobo anasema.
22 “Mulete ushuhuda na mutuambie mambo yenye yatatokea.
Ao mututangazie mambo yenye kuja.+
Ndiyo, mufanye jambo fulani, la muzuri ao la mubaya,
Ili tushangae wakati tutaliona.+
Kila mutu mwenye anawachagua ninyi ni chukizo.+
25 Nimemuinua mutu fulani kutoka kaskazini, na atakuja,+
Mutu mumoja kutoka mahali jua linatokea*+ mwenye ataitia jina langu.
Atakanyanga-kanyanga watawala* kama vile wao ni udongo,+
Kama vile mufinyanzi* anakanyanga-kanyanga udongo mubichi.
26 Ni nani alisema kuhusu jambo hili tangu mwanzo, ili tujue,
Ao kuanzia nyakati za zamani, ili tuseme, ‘Yeye anasema kweli’?+
Kwa kweli, hakuna mwenye alilitangaza!
Hakuna mwenye alilisema!
Hakuna mwenye alisikia jambo lolote kutoka kwenu.”+
27 Nilikuwa wa kwanza kumuambia Sayuni: “Angalia! Wako hapa!”+
Na kwa Yerusalemu nitatuma mutu mwenye kubeba habari njema.+
28 Lakini niliendelea kuangalia, na hapakukuwa mutu;
Hapakukuwa mutu yeyote kati yao mwenye alitoa shauri.
Na niliendelea kuwaomba watoe jibu.
29 Angalia! Wote ni udanganyifu.*
Kazi zao ni bure.
Sanamu zao za metali* ni upepo na kitu cha kuwazia-wazia tu.+