Yoshua
2 Kisha Yoshua mwana wa Nuni akatuma kwa uficho wanaume wawili wapelelezi kutoka Shitimu.+ Akawaambia: “Muende mupeleleze inchi, zaidi sana muji wa Yeriko.” Basi wakaenda na kufika kwenye nyumba ya mwanamuke mumoja kahaba jina lake Rahabu,+ na wakakaa pale. 2 Mufalme wa Yeriko akaambiwa: “Angalia! Wanaume Waisraeli wameingia humu leo usiku ili kupeleleza inchi.” 3 Basi mufalme wa Yeriko akatuma ujumbe kwa Rahabu: “Uwatoshe inje wanaume wenye walikuja na wenye wako katika nyumba yako, kwa maana wamekuja ili kupeleleza inchi yote.”
4 Lakini mwanamuke huyo alichukua wanaume hao wawili na kuwaficha. Kisha akasema: “Ni kweli, wanaume hao walikuja kwangu, lakini sikujua walitoka wapi. 5 Na wakati giza liliingia, wakati mulango mukubwa wa muji ulikuwa karibu kufungwa, wanaume hao waliondoka. Sijue walienda wapi, lakini kama munawafuatilia haraka, mutawakuta.” 6 (Lakini alikuwa amewapandisha kwenye sehemu ya juu ya nyumba na kuwaficha kati ya majani ya kitani yenye kutandikwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba.) 7 Basi wanaume hao wakawafuatilia kuelekea Yordani kwenye nafasi za kuvukia,+ na wakati tu walitoka, mulango mukubwa wa muji ukafungwa.
8 Mbele ya wanaume hao kulala, Rahabu akaenda kuwaona kwenye sehemu ya juu ya nyumba. 9 Akawaambia: “Ninajua kwamba Yehova atawapatia inchi hii+ na tumeogopa kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa inchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tulisikia namna Yehova alikausha maji ya Bahari Nyekundu mbele yenu wakati mulitoka Misri+ na mambo yenye mulitendea wale wafalme wawili wa Waamori, Sihoni+ na Ogu,+ wenye muliharibu kabisa ngambo ingine ya* Yordani. 11 Wakati tulisikia kuhusu mambo hayo, mioyo yetu ilizimia kwa sababu ya woga,* na hakuna mwenye alikuwa na uhodari wowote kwa sababu yenu, kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na chini duniani.+ 12 Sasa, tafazali, muniapie kwa Yehova kwamba, kwa sababu nimewatendea ninyi kwa upendo mushikamanifu, ninyi pia mutatendea nyumba ya baba yangu kwa upendo mushikamanifu; na munipatie alama yenye kuaminika.* 13 Munapaswa kulinda uzima wa baba yangu na mama yangu, ndugu zangu na dada zangu, na watu wao wote, na munapaswa kutuokoa ili tusikufe.”*+
14 Kwa hiyo wanaume hao wakamuambia: “Tutatoa uzima wetu kwa ajili ya uzima wenu!* Kama hamutaambia watu kazi yenye walitutuma kufanya, basi tutawatendea kwa upendo mushikamanifu na kwa uaminifu wakati Yehova atatupatia inchi hii.” 15 Basi akawashusha kwa kamba kupitia dirisha, kwa maana nyumba yake ilikuwa kwenye upande mumoja wa ukuta wa muji. Kwa kweli, alikuwa anaishi kwenye ukuta.+ 16 Kisha akawaambia: “Muende kwenye eneo lenye milima mujifiche kule siku tatu (3), ili wale wenye kuwafuatilia wasiwapate. Halafu, wakati wale wenye kuwafuatilia watakuwa wamerudia, munaweza kuendelea na safari yenu.”
17 Wanaume hao wakamuambia: “Hatutakuwa na hatia kuhusiana na kiapo hiki chenye umetufanya tuape+ 18 ikiwa wakati tutakuja katika inchi hii, utafunga kamba hii ya uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa kwenye dirisha lenye kupitia hilo unatushusha. Unapaswa kukusanya baba yako, mama yako, ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako katika nyumba hii.+ 19 Kisha kama mutu anatoka katika nyumba yako na kuenda inje, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, na hatutakuwa na hatia. Lakini kama jambo fulani la mubaya linamupata mutu mwenye atabakia pamoja na wewe katika nyumba, damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu. 20 Lakini kama unaambia watu kazi yenye walitutuma kufanya,+ hatutakuwa na hatia kuhusiana na kiapo hiki chenye umetufanya tuape.” 21 Akasema: “Ikuwe kama vile munasema.”
Kwa hiyo akawaacha waende, na wakaenda. Kisha, akafunga ile kamba ya rangi nyekundu yenye kungaa kwenye dirisha. 22 Basi wakaenda na kufika katika eneo lenye milima na wakakaa kule siku tatu (3), mupaka wakati wale wenye walikuwa wanawafuatilia walirudia. Walikuwa wamewatafuta katika kila barabara lakini hawakuwaona. 23 Wanaume hao wawili wakatoka kwenye eneo lenye milima na kuvuka muto na kufika kwa Yoshua mwana wa Nuni. Wakamuelezea mambo yote yenye yaliwapata. 24 Tena wakamuambia Yoshua: “Yehova ametupatia inchi yote.+ Na hata, wakaaji wote wa inchi wamevunjika moyo kwa sababu yetu.”+