Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Samweli

      • Daudi anafanya uzinifu na Bat-sheba (1-13)

      • Daudi anafanya mipango ili Uria auawe (14-25)

      • Daudi anamuchukua Bat-sheba ili akuwe bibi yake (26, 27)

2 Samweli 11:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, katika kipindi cha mvua ya mwisho.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 12:26
  • +1Nya 20:1

2 Samweli 11:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 12:24; 1 Fal. 1:11
  • +1Nya 3:5, 9
  • +2 Sa. 23:8, 39; 1 Fal. 15:5
  • +Mwa 10:15; Kum 20:17

2 Samweli 11:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Inawezekana ni uchafu wa siku zake za kuona mwezi.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:14, 17
  • +Law. 18:20; 20:10; Mez. 6:32; Ebr 13:4
  • +Law. 12:2; 15:19; 18:19

2 Samweli 11:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “unawe miguu yako.”

  • *

    Ao “fungu la mufalme,” ni kusema, fungu lenye mwenye kumupokea mugeni anamutumia mugeni muheshimiwa.

2 Samweli 11:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kama vile nafsi yako inaishi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 6:17; 7:2
  • +Law. 15:16; 1 Sa. 21:5

2 Samweli 11:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 51:14; Mez. 3:29

2 Samweli 11:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 12:9

2 Samweli 11:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 9:50-53
  • +Amu 6:32; 7:1

2 Samweli 11:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 11:17

2 Samweli 11:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 12:26

2 Samweli 11:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “lilikuwa mubaya katika macho ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 5:13; 12:9
  • +Mwa 39:7-9; 1 Fal. 15:5; Zab 5:6; 11:4; Ebr 13:4

Maandiko ingine

2 Sam. 11:12 Sa. 12:26
2 Sam. 11:11Nya 20:1
2 Sam. 11:32 Sa. 12:24; 1 Fal. 1:11
2 Sam. 11:31Nya 3:5, 9
2 Sam. 11:32 Sa. 23:8, 39; 1 Fal. 15:5
2 Sam. 11:3Mwa 10:15; Kum 20:17
2 Sam. 11:4Kut 20:14, 17
2 Sam. 11:4Law. 18:20; 20:10; Mez. 6:32; Ebr 13:4
2 Sam. 11:4Law. 12:2; 15:19; 18:19
2 Sam. 11:112 Sa. 6:17; 7:2
2 Sam. 11:11Law. 15:16; 1 Sa. 21:5
2 Sam. 11:15Zab 51:14; Mez. 3:29
2 Sam. 11:172 Sa. 12:9
2 Sam. 11:21Amu 9:50-53
2 Sam. 11:21Amu 6:32; 7:1
2 Sam. 11:242 Sa. 11:17
2 Sam. 11:252 Sa. 12:26
2 Sam. 11:272 Sa. 5:13; 12:9
2 Sam. 11:27Mwa 39:7-9; 1 Fal. 15:5; Zab 5:6; 11:4; Ebr 13:4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Samweli 11:1-27

Cha Pili cha Samweli

11 Kwenye mwanzo wa mwaka,* wakati wafalme wanaenda katika mapambano ya kijeshi, Daudi alituma Yoabu na watumishi wake na jeshi lote la Israeli ili waharibu Waamoni, na wakazunguka Raba kwa ajili ya vita,+ wakati huo Daudi alibakia Yerusalemu.+

2 Mangaribi moja Daudi akasimama kutoka kwenye kitanda chake na kuenda kutembea-tembea kwenye sehemu ya juu ya nyumba ya mufalme. Akiwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba akamuona mwanamuke akioga, na mwanamuke huyo alikuwa mwenye sura na umbo ya muzuri sana. 3 Daudi akamutuma mutu fulani aulize kuhusu mwanamuke huyo, na mutu huyo akaleta habari: “Je, haiko Bat-sheba+ binti ya Eliamu+ na bibi ya Uria+ Muhiti?”+ 4 Kisha Daudi akatuma wajumbe wamulete.+ Basi akakuja kwa Daudi, na Daudi akalala naye.+ (Jambo hilo lilitendeka wakati mwanamuke huyo alikuwa anajitakasa uchafu wake.*)+ Kisha, mwanamuke huyo akarudia katika nyumba yake.

5 Mwanamuke huyo akapata mimba, na akatuma ujumbe kwa Daudi: “Niko na mimba.” 6 Basi Daudi akatuma ujumbe kwa Yoabu: “Unitumie Uria Muhiti.” Kwa hiyo Yoabu akamutuma Uria kwa Daudi. 7 Wakati Uria alifika kwa Daudi, Daudi akamuuliza habari kuhusu Yoabu, habari kuhusu maaskari, na habari kuhusu vita. 8 Kisha Daudi akamuambia Uria: “Shuka uende kwenye nyumba yako na upumuzike.”* Wakati Uria alitoka katika nyumba ya mufalme, zawadi ya fazili ya mufalme* ilitumwa nyuma yake. 9 Lakini, Uria alilala kwenye muingilio wa nyumba ya mufalme pamoja na watumishi wengine wote wa bwana wake, na hakushuka kuenda kwenye nyumba yake. 10 Kwa hiyo Daudi akaambiwa: “Uria hakushuka kuenda kwenye nyumba yake.” Basi Daudi akamuambia Uria: “Umetoka katika safari, haiko vile? Sababu gani haukushuka kuenda kwenye nyumba yako?” 11 Uria akamujibu Daudi: “Sanduku+ na Israeli na Yuda wanakaa katika makao ya muda, na bwana wangu Yoabu na watumishi wa bwana wangu wanapiga kambi katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba. Basi namna gani ninaweza kuenda katika nyumba yangu ili kula na kunywa na kulala na bibi yangu?+ Kama vile hakika unaishi na uko muzima,* sitafanya jambo hilo!”

12 Basi Daudi akamuambia Uria: “Bakia hapa leo pia, na kesho nitakuruhusu uende.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku hiyo na siku yenye ilifuata. 13 Kisha Daudi akamuitisha ili akule na kunywa pamoja naye, na akamulewesha. Lakini mangaribi, Uria alienda kulala kwenye kitanda chake pamoja na watumishi wa bwana wake, na hakushuka kuenda kwenye nyumba yake. 14 Asubui Daudi akamuandikia Yoabu barua na akaituma kwa mukono wa Uria. 15 Aliandika katika barua hiyo: “Mumutie Uria kwenye mustari wa mbele mahali kwenye vita iko nguvu sana. Kisha mumuache na kurudia nyuma yake, ili apigwe na kufa.”+

16 Yoabu alikuwa amechunguza muji kwa uangalifu, na alimutia Uria mahali kwenye alijua kulikuwa wapiganaji-vita wenye nguvu. 17 Wakati watu wa muji walitoka inje na kupigana na Yoabu, wamoja kati ya watumishi wa Daudi wakauawa, na Uria Muhiti alikuwa kati ya wale wenye walikufa.+ 18 Sasa Yoabu akamupelekea Daudi habari zote za vita. 19 Akamupatia mujumbe maagizo haya: “Wakati utamaliza kumuambia mufalme habari zote za vita, 20 mufalme anaweza kukasirika na kukuambia, ‘Sababu gani mulienda karibu sana na muji ili kupigana? Je, hamukujua kwamba watapiga mishale kutoka sehemu ya juu ya ukuta? 21 Ni nani alimupiga na kumuua Abimeleki+ mwana wa Yerubesheti?+ Je, haikukuwa mwanamuke mwenye alimuangushia jiwe la juu la kusagia kutoka kwenye sehemu ya juu ya ukuta, na kumuua kule Tebesi? Sababu gani mulienda karibu sana na ukuta?’ Kisha utasema, ‘Pia mutumishi wako Uria Muhiti alikufa.’”

22 Basi mujumbe huyo akaenda na kumuambia Daudi kila jambo lenye Yoabu alikuwa amemutuma aseme. 23 Mujumbe huyo akamuambia Daudi: “Watu wao walitupita nguvu, na walitoka ili kutushambulia katika eneo la mashamba; lakini tuliwarudisha nyuma mupaka kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa muji. 24 Na wapiga-mishale walikuwa wanatupia watumishi wako mishale kutoka kwenye sehemu ya juu ya ukuta, na wamoja kati ya watumishi wa mufalme wakakufa; mutumishi wako Uria Muhiti akakufa pia.”+ 25 Basi Daudi akamuambia mujumbe huyo: “Ambia Yoabu hivi: ‘Jambo hili lisikuhangaishe, kwa maana upanga unameza huyu na pia ule. Mufanye mashambulizi yakuwe nguvu zaidi juu ya muji na muushinde.’+ Na umutie moyo.”

26 Wakati bibi ya Uria alisikia kwamba Uria bwana yake amekufa, akaanza kumuombolezea bwana yake. 27 Wakati tu kipindi cha kuomboleza kilimalizika, Daudi akamuitisha na kumuleta katika nyumba yake, na akakuwa bibi yake+ na akamuzalia mwana. Lakini jambo lenye Daudi alikuwa amefanya lilimuchukiza sana* Yehova.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine