Kwa Waroma
4 Kama ni vile, tutasema Abrahamu, babu yetu kulingana na mwili alipata faida gani? 2 Kwa mufano, kama Abrahamu angetangazwa kuwa mwenye haki kwa sababu ya matendo, angekuwa na sababu ya kujisifu, lakini hapana mbele ya Mungu. 3 Kwa maana andiko linasema nini? “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova,* na hilo likahesabiwa kwake kuwa haki.”+ 4 Sasa kwa mutu mwenye anafanya kazi, malipo yake hayahesabiwe kuwa fazili zenye hazistahiliwe lakini kama vile deni. 5 Kwa upande mwingine, mutu mwenye hafanye kazi lakini anaweka imani katika Ule mwenye anatangaza mutu mwenye hamuogope Mungu kuwa mwenye haki, imani yake inahesabiwa kuwa haki.+ 6 Kama vile Daudi pia anasema juu ya furaha ya mutu mwenye Mungu anahesabia kuwa mwenye haki bila matendo: 7 “Wenye furaha ni wale wenye matendo yao ya kuvunja sheria yamesamehewa na wenye zambi zao zimefunikwa;* 8 mwenye furaha ni mutu mwenye Yehova* hatahesabia zambi yake hata kidogo.”+
9 Basi, je, furaha hiyo inakuja tu kwa watu wenye kutahiriwa ao pia kwa watu wenye hawatahiriwe?+ Kwa maana tunasema: “Imani ya Abrahamu ilihesabiwa kwake kuwa haki.”+ 10 Basi, ni katika hali gani ilihesabiwa kuwa haki? Wakati alikuwa ametahiriwa ao mbele ya kutahiriwa? Hakukuwa bado mwenye kutahiriwa lakini alikuwa hajatahiriwa. 11 Na alipokea alama+—ni kusema, kutahiriwa—kuwa muhuri* wa haki kupitia imani yenye alikuwa nayo wakati alikuwa katika hali yake ya kutokutahiriwa, ili akuwe baba ya wale wote wenye kuwa na imani+ hata kama hawajatahiriwa, kusudi wahesabiwe kuwa wenye haki; 12 na ili akuwe baba ya uzao wenye kutahiriwa, hapana tu kwa wale wenye wanashikamana na kutahiriwa, lakini pia kwa wale wenye wanatembea kwa utaratibu katika hatua za imani yenye baba yetu Abrahamu+ alikuwa nayo katika hali ya kutokutahiriwa.
13 Kwa maana haiko kupitia sheria ndiyo Abrahamu ao uzao wake walipata ahadi kwamba atakuwa* muriti wa ulimwengu fulani,+ lakini ilikuwa kupitia haki kwa njia ya imani.+ 14 Kwa maana kama wale wenye wanashikamana na sheria ni wariti, imani inakuwa bure na ahadi imefutwa. 15 Kwa kweli Sheria inatokeza kasirani kali,+ lakini mahali kwenye hakuna sheria, hakuna pia kosa lolote.+
16 Ndiyo sababu ni kupitia imani, ili ikuwe kulingana na fazili zenye hazistahiliwe,+ kusudi ahadi ikuwe hakika kwa uzao wake wote,*+ haiko kwa wale tu wenye wanashikamana na Sheria, lakini pia kwa wale wenye wanashikamana na imani ya Abrahamu, mwenye kuwa baba yetu sisi wote.+ 17 (Hii ni kama vile imeandikwa: “Nimekuweka kuwa baba ya mataifa mengi.”)+ Hili lilikuwa mbele ya macho ya Mungu, mwenye Abrahamu aliamini, mwenye anafanya wafu kuwa wazima na anaita mambo yenye hayako kama vile yako.* 18 Hata kama hakukuwa na sababu ya kuwa na tumaini, lakini kwa kutegemea tumaini, alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi kulingana na yale yenye yalikuwa yamesemwa: “Ni vile uzao wako utakuwa.”*+ 19 Na hata kama imani yake haikuregea, alifikiria mwili wake mwenyewe, wenye sasa ulikuwa kama umekufa (kwa kuwa alikuwa na miaka karibu mia moja [100]),+ na pia hali ya kufa ya* tumbo la uzazi la Sara.+ 20 Lakini kwa sababu ya ahadi ya Mungu, yeye hakusita-sita kwa kukosa imani; lakini alikuwa mwenye nguvu kwa imani yake, akimupatia Mungu utukufu 21 na akiwa amesadikishwa kabisa kwamba kile chenye Yeye aliahidi, Yeye alikuwa pia na uwezo wa kukifanya.+ 22 Kwa hiyo “ikahesabiwa kwake kuwa haki.”+
23 Hata hivyo, maneno “ikahesabiwa kwake” hayakuandikwa kwa ajili yake tu,+ 24 lakini pia kwa ajili yetu, sisi wenye itahesabiwa kwetu, kwa sababu tunamuamini Yeye mwenye alimufufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu.+ 25 Alitolewa kwa ajili ya makosa yetu+ na alifufuliwa ili tutangazwe kuwa wenye haki.+