HABARI YA KUJIFUNZA YA 14
WIMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Yangu
“Muchague . . . Ni Nani Mutatumikia”
“Mimi na nyumba yangu, tutamutumikia Yehova.”—YOS. 24:15.
WAZO KUBWA
Kutukumbusha sababu zenye zinafanya tuchagule kumutumikia Yehova.
1. Tunapaswa kufanya nini juu tukuwe na furaha ya kweli, na juu ya nini? (Isaya 48:17, 18)
BABA yetu wa mbinguni anatupenda sana, na anapenda tukuwe na maisha ya furaha leo na mu siku zenye ziko nakuya. (Muh. 3:12, 13) Alituumba na uwezo mbalimbali, lakini hakutupatia uwezo wa kujitawala siye wenyewe ao kujiamulia mambo ya muzuri na ya mubaya. (Muh. 8:9; Yer. 10:23) Anajua kama juu tukuwe na furaha ya kweli, tunapaswa kumutumikia na kutumikisha kanuni zake mu maisha yetu.—Soma Isaya 48:17, 18.
2. Shetani anapenda tuwaze nini, na Yehova alifanya nini juu ya kuonyesha kama Shetani alisema bongo?
2 Shetani anapenda tuwaze kama hatuna lazima ya Yehova juu tukuwe na furaha, na anapenda tuamini kama banadamu banaweza kujitawala muzuri. (Mwa. 3:4, 5) Juu ya kuonyesha kama Shetani alisema bongo, Yehova aliacha banadamu benye balimuasi bajitawale kwa wakati fulani. Tuko najionea siye peke namna banadamu bameshindwa kujitawala. Lakini mu Biblia muko mifano ya banaume na banamuke benye balikuwa na furaha juu balimutumikia Yehova. Kwa mufano, Yesu njo mutu mwenye alikuwa na furaha zaidi juu alimutumikia Yehova. Tuone kwanza juu ya nini Yesu alichagula kumutumikia Yehova, kisha tutaona juu ya nini Baba yetu wa mbinguni anastahili ibada yetu. Na ku mwisho, tutaona sababu zenye zinafanya tuchagule kumutumikia Yehova.
JUU YA NINI YESU ALICHAGULA KUMUTUMIKIA YEHOVA
3. Shetani aliambia Yesu nini, na Yesu aliamua nini?
3 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alipaswa kuchagula ni nani atatumikia. Wakati kidogo kisha Yesu kubatizwa, Shetani alisema atamupatia falme zote za mu dunia kama tu anamufanyia tendo moya ya ibada. Yesu alimujibia hivi: “Toka mbele yangu, Shetani! Kwa sababu imeandikwa: ‘Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.’” (Mt. 4:8-10) Juu ya nini Yesu alikamata ile uamuzi? Tuone sababu fulani.
4-5. Juu ya nini Yesu alichagula kumutumikia Yehova?
4 Sababu kubwa yenye ilifanya Yesu achagule kumutumikia Yehova ni upendo. Yesu anamupenda sana Baba yake. (Yoh. 14:31) Zaidi ya ile, Yesu anajua kama kumutumikia Yehova njo jambo ya muzuri ya kufanya. (Yoh. 8:28, 29; Ufu. 4:11) Anajua kama uzima unatoka kwa Yehova na Yehova ni mwenye kutumainika na ni mukarimu. (Zb. 33:4; 36:9; Yak. 1:17) Sikuzote Yehova aliambia Yesu mambo ya kweli, na ni Yehova alimupatia kila kitu yenye alikuwa nayo. (Yoh. 1:14) Lakini, Shetani yeye ni muongo, iko na pupa, na anatafuta tu faida yake. (Yoh. 8:44) Tena ni Shetani njo alileta kifo. Juu Yesu alijua ile mambo yote, hakupenda kumuasi Yehova na kuwa kama Shetani.—Flp. 2:5-8.
5 Sababu ingine yenye ilifanya Yesu achagule kumutumikia Yehova ni hii: alifikiria matokeo ya utumishi wake muaminifu. (Ebr. 12:2) Alijua kama akiendelea kuwa muaminifu, atatakasa jina ya Baba yake, na ile itafanya iwezekane kumaliza mateso yote yenye Shetani ameleta.
JUU YA NINI YEHOVA ANASTAHILI IBADA YETU?
6-7. Juu ya nini batu mingi leo habamutumikie Yehova, lakini juu ya nini Yehova anastahili ibada yetu?
6 Leo batu mingi habamutumikie Yehova juu habamujue; habajue sifa za muzuri zenye iko nazo na habajue mambo yote yenye alishabafanyia. Banafanana na batu benye mutume Paulo alihubiria mu Atene.—Mdo. 17:19, 20, 30, 34.
7 Paulo aliambia batu benye balikuwa namusikiliza kama Mungu wa kweli “anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” Aliongeza hivi: “Kupitia kwake tuko na uzima na tunatembea na tuko.” Mungu njo Muumbaji, na “kutoka kwa mutu mumoja, alifanya kila taifa la watu,” njo maana anastahili ibada yetu.—Mdo. 17:25, 26, 28.
8. Yehova hatafanyaka nini hata siku moya? Fasiria.
8 Yehova ni Muumbaji na iko na mamlaka mu ulimwengu wote. Kwa hiyo, angependa angelazimisha batu bamutumikie. Lakini, Yehova hatafanyaka vile hata siku moya. Anatupatia ushuhuda wenye unaonyesha kama iko na kama anapenda sana kila mumoya wetu. Anapenda batu mingi kadiri inawezekana bakuwe barafiki yake milele. (1 Ti. 2:3, 4) Njo maana Yehova anatuzoeza juu tufundishe bengine kuhusu kusudi yake na kubaonyesha mambo ya muzuri yenye atafanyia banadamu. (Mt. 10:11-13; 28:19, 20) Ametupatia kutaniko kwenye tunamuabudu, na ametupatia bazee benye banatuhangaikia kwa upendo.—Mdo. 20:28.
9. Upendo wa Yehova unaonekana namna gani?
9 Yehova iko na upendo wa ajabu sana, na upendo wake unaonekana hata mu namna anatendea batu benye habaamini kama iko. Waza kidogo: Tangu zamani, batu mingi sana bameamua kujichagulia mambo ya muzuri na ya mubaya. Lakini juu Yehova iko na upendo, anabapatia mambo yenye biko nayo lazima juu baendelee kuishi na bafurahie maisha. (Mt. 5:44, 45; Mdo. 14:16, 17) Kwa mufano, banaweza kuwa na familia na barafiki benye banabapenda, banaweza kuwa na batoto, na banaweza kutumika na kufurahia maisha. (Zb. 127:3; Muh. 2:24) Ile mambo inaonyesha kama Baba yetu wa mbinguni anapenda banadamu bote. (Kut. 34:6) Sasa, tuone juu ya nini tunachagula kumutumikia Yehova na namna anabariki benye banachagula kumutumikia.
JUU YA NINI TUNACHAGULA KUMUTUMIKIA YEHOVA?
10. (a) Ni sababu gani kubwa inafanya tuchagule kumutumikia Yehova? (Matayo 22:37) (b) Uvumilivu wa Yehova umekuletea faida gani? (Zaburi 103:13, 14)
10 Kama Yesu, sababu kubwa yenye inafanya tuchagule kumutumikia Yehova ni juu tunamupenda sana. (Soma Matayo 22:37.) Kujifunza juu ya sifa zake, kunafanya tupende kumukaribia zaidi. Kwa mufano, fikiria namna Yehova anatuvumilia. Wakati Waisraeli walikosa kumutii, aliwaomba hivi: “Mugeuke, tafazali, kutoka kwenye njia zenu za mubaya.” (Yer. 18:11) Yehova anakumbuka kama hatukamilike na tuko mavumbi. (Soma Zaburi 103:13, 14.) Wakati unafikiria uvumilivu wa Yehova na sifa zake zingine, unajisikia namna gani, unapenda kumutumikia milele?
11. Ni sababu gani zingine zenye zinafanya tuchagule kumutumikia Baba yetu wa mbinguni?
11 Sababu ingine yenye inafanya tupende kumutumikia Yehova ni hii: tunajua kama kumutumikia njo jambo ya muzuri ya kufanya. (Mt. 4:10) Zaidi ya ile, tunajua kama kumutumikia Yehova kwa uaminifu kuko na matokeo ya muzuri. Wakati tunamutumikia Yehova kwa uaminifu, tunasaidia kutakasa jina yake, tunafurahisha moyo wake, na tunaonyesha kama Shetani ni muongo. Pia, kama tunachagula kumutumikia Yehova leo, tuko na tumaini ya kumutumikia milele!—Yoh. 17:3.
12-13. Mufano wa Jane na Pam unatufundisha nini?
12 Hata wakati tungali wadogo, tunaweza kuanza kumupenda Yehova sana, na ile upendo inaweza kuendelea kuongezeka wakati tuko nakomala. Ona mufano wa badada bawili ba mu familia moya, Jane na Pam.a Wakati Jane alikuwa na miaka 11 na Pam miaka 10, balianza kujifunza Biblia. Hata kama bazazi yabo habakupenda kujifunza, baliruhusu Jane na Pam bajifunze pamoya na Mashahidi. Lakini Jane na Pam balipaswa kuenda pamoya na familia yote ku kanisa kila mwisho wa juma. Jane anasema hivi: “Mambo yenye Mashahidi walinifundisha, ilinisaidia nikatale, wakati vijana wa miaka yangu walinikaza nitumie dawa za kulewesha na nifanye uasherati.”
13 Kisha miaka fulani, Jane na Pam bakakuwa bahubiri. Na kisha wakati, bakakuwa bapainia, hata kama balikuwa nahangaikia bazazi yabo benye kuzeeka. Wakati Jane anakumbuka ile mambo yote, anasema hivi: “Nilijionea na macho kama Yehova ni muaminifu, anahangaikiaka barafiki yake. Na sawa vile 2 Timoteo 2:19 inasema, ‘Yehova anajua wenye kuwa wake.’” Bila shaka Yehova anahangaikia benye banachagula kumupenda na kumutumikia!
14. Namna gani maneno na matendo yetu inasaidia kutakasa jina ya Yehova? (Ona pia picha.)
14 Juu jina ya Yehova imechafuliwa, tunapenda kusaidia batu bajue kama mambo ya mingi yenye bamesikia juu ya Yehova ni ya bongo. Tuseme uko na rafiki muzuri, mukarimu sana, na mwenye anazoea kusamehe. Kisha siku moya, unasikia mutu iko nasema ule rafiki yako mubaya, aseme hana huruma na anadanganyaka batu. Utafanya nini? Utamutetea. Vilevile, wakati Shetani na benye banamuunga mukono banasema mambo ya bongo juu ya Yehova juu ya kuchafula jina yake, hatubakiake kimya; tunaambia batu kweli juu ya Yehova na tunatetea kwa bidii jina yake. (Zb. 34:1; Isa. 43:10) Tunaonyesha kama tunapenda kumutumikia Yehova kwa nafsi yote kupitia maneno na matendo yetu.
Utasaidia kutetea jina ya Yehova? (Ona fungu ya 14)b
15. Mutume Paulo alipata baraka gani juu alibadilisha miradi yake? (Wafilipi 3:7, 8)
15 Tuko tayari kubadilisha miradi yetu mu maisha juu tuweze kumutumikia Yehova mu njia yenye anakubali na juu tuweze kumutumikia zaidi. Kwa mufano, mutume Paulo alikuwa na cheo mu dini ya Wayahudi, lakini aliamua kuacha ile cheo juu ya kumufuata Yesu na kumutumikia Yehova. (Gal. 1:14) Matokeo ilikuwa nini? Aliishi maisha ya muzuri sana na alipata pendeleo ya kutawala na Kristo mbinguni. Paulo hakuhuzunika hata siku moya juu ya uamuzi wake wa kumutumikia Yehova, na siye hatutahuzunika hata siku moya.—Soma Wafilipi 3:7, 8.
16. Mufano wa Julia unatufundisha nini? (Ona pia picha.)
16 Kama kumutumikia Yehova njo tunatia fasi ya kwanza mu maisha yetu, tutakuwa na maisha ya muzuri leo na wakati wenye kuya. Ona mufano wa dada Julia. Mbele ajifunze kweli, Julia alikuwa muimbaji mu kanisa wakati alikuwa kijana. Muimbaji fulani mwenye uzoefu alitambua kama Julia alikuwa naimba muzuri sana na alimuzoeza. Bila kukawia Julia alijulikana na alianza kuimba fasi zenye kujulikana sana. Wakati alikuwa ku masomo fulani ya muziki yenye kujulikana, mwanafunzi mwenzake alianza kuzungumuza naye juu ya Mungu na alimuambia kama Mungu iko na jina, na jina yake ni Yehova. Bila kukawia, Julia alianza kujifunza Biblia mara mbili mu juma. Ku mwisho, aliamua kutia utumishi wake kwa Yehova fasi ya kwanza mu maisha yake kuliko kufuatilia mambo ya muziki. Haikukuwa mwepesi kukamata ile uamuzi. Julia anasema hivi: “Batu mingi baliniambia kama niko naharibisha zawadi ya kuimba yenye niko nayo. Lakini nilipenda kutumikisha maisha yangu yote juu ya kumutumikia Yehova.” Julia anajisikia namna gani leo kuhusu ule uamuzi wenye alikamata kumepita zaidi ya miaka 30? Anasema hivi: “Niko na amani ya akili, na niko hakika kama Yehova atatimiza tamaa za moyo wangu wakati wenye kuya.”—Zb. 145:16.
Wakati kumutumikia Yehova njo jambo ya maana mu maisha yetu, tunakuwa na furaha sana mu maisha (Ona fungu ya 16)c
ENDELEA KUMUTUMIKIA YEHOVA
17. Kujua kama mwisho iko karibu sana kunamaanisha nini kwa benye bamechagula kumutumikia Mungu, na kwa benye habayafanya vile?
17 Mwisho iko karibu sana. Mutume Paulo aliandika hivi: “Kwa maana kunabakia ‘wakati kidogo sana,’ na ‘ule mwenye anakuja atafika na hatakawia.’” (Ebr. 10:37) Ile inamaanisha nini? Inamaanisha kama wakati wenye unabakia juu batu baamue kama batamutumikia Yehova ao hapana, unabakia kidogo. (1 Ko. 7:29) Na kama tulishachagula kumutumikia Mungu, tunajua kama hata tukipata magumu, itakuwa kwa “wakati kidogo sana.”
18. Yehova na Yesu banapenda tufanye nini?
18 Yesu alitia batu moyo bakuwe banafunzi yake, lakini pia baendelee kumufuata. (Mt. 16:24) Kwa hiyo, hata kama kulishapita miaka mingi tangu tuko namutumikia Yehova, tuazimie kuendelea. Tunapaswa kufanya nguvu yetu yote juu tuendelee kuheshimia uamuzi wetu wa kumutumikia Yehova. Pengine haitakuwa mwepesi, lakini tukifanya vile tutakuwa na furaha na tutapata baraka za mingi, leo na wakati wenye kuya!—Zb. 35:27.
19. Mufano wa Gene unakufundisha nini?
19 Batu fulani banaona kama haiko mwepesi kumutumikia Yehova. Kama uko kijana, unaonaka kama kuko byenye unakosa juu uko namutumikia Yehova? Kijana moya mwenye kuitwa Gene anasema hivi: “Niliona kama kuwa Shahidi wa Yehova kunanifunga-funga. Benzangu balionekana kama biko nafurahia maisha; balikuwa nafanya mafete, kila mutu alikuwa na wake, na balikuwa nacheza michezo ya video ya jeuri. Lakini miye nilikuwa napitisha wakati yangu yote ku mikutano na mu mahubiri.” Ile mawazo ilikuwa na matokeo gani juu ya Gene? Anasema hivi: “Nilianza kuishi maisha ya unafiki, na kwa wakati fulani ilinifurahisha. Lakini haikuniletea furaha ya kweli. Nilianza kufikiria faida ya kutii mafundisho ya Biblia na niliamua kumutumikia tena Yehova kwa moyo wangu wote. Tangu pale, imeonekana kama Yehova amejibia sala zangu zote.”
20. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?
20 Muandikaji moya wa zaburi alimuimbia Yehova hivi: “Mwenye furaha ni ule mwenye unachagua na kumuleta karibu ili akae katika viwanja vyako.” (Zb. 65:4) Na siye tuazimie kuendelea kumutumikia Yehova sawa Yoshua mwenye alisema hivi: “Mimi na nyumba yangu, tutamutumikia Yehova.”—Yos. 24:15.
WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?
a Majina fulani ilibadilishwa.
b MAFASIRIO YA PICHA : Mwanamuke fulani anasikia namna wapinzani wetu wako natusema mubaya inje ya fasi ya mukusanyiko, kisha anakaribia prezantware na anasikia maneno ya kweli.
c MAFASIRIO YA PICHA: Picha inaonyesha namna Julia aliamua kama kumutumikia Yehova njo atatia fasi ya kwanza mu maisha yake.