HABARI YA KUJIFUNZA YA 21
WIMBO 21 Muendelee Kutafuta Kwanza Ufalme
Tafuta Muji Wenye Utadumu
“Tunatafuta kwa bidii ule [muji] wenye utakuja.”—EBR. 13:14.
WAZO KUBWA
Namna Waebrania sura ya 13 inaweza kutusaidia leo na wakati wenye kuya.
1. Yesu alitabiri nini juu ya Yerusalemu?
MASIKU kidogo mbele Yesu akufe alitoa unabii fulani. Ule unabii ulitimia kwa mara ya kwanza wakati Yerusalemu na hekalu yake viliharibiwa. Yesu alitabiri kama siku moya Yerusalemu ‘itazungukwa na majeshi yenye kupiga kambi.’ (Lu. 21:20) Njo maana aliambia banafunzi yake kama wakati bataona ile majeshi, banapaswa kukimbia bila kukawia. Ile maneno ya Yesu ilitimia wakati majeshi ya Roma ilizunguka Yerusalemu.—Lu. 21:21, 22.
2. Paulo alikumbusha Bakristo Baebrania benye balikuwa naaishi Yudea na Yerusalemu?
2 Miaka kidogo mbele majeshi ya Roma izunguke Yerusalemu, mutume Paulo aliandikia Bakristo ba Yerusalemu na Yudea ujumbe wa maana sana. Ule ujumbe unaitwa leo Barua kwa Waebrania. Mu ile barua Paulo alipatia Bakristo ba Yudea na Yerusalemu mashauri ya maana sana yenye ingebasaidia bajitayarishe juu ya mambo yenye ilikuwa karibu kutokea. Ni mambo gani ilikuwa karibu kutokea? Yerusalemu ilikuwa karibu kuharibiwa. Bale Bakristo balipaswa kuwa tayari kuacha manyumba na makazi juu baokoke. Paulo alisema hivi juu ya muji wa Yerusalemu: “Hapa hatuna muji wenye kudumu.” Kisha aliongeza hivi: “Lakini tunatafuta kwa bidii ule wenye utakuja.”—Ebr. 13:14.
3. “Muji wenye uko na misingi ya kweli” ni nini, na juu ya nini tunaungojea?
3 Wakati Bakristo baliamua kutoka Yerusalemu na Yudea, inawezekana batu mingi balibacheka na baliona kama banakosa akili. Lakini ule uamuzi ulibaokoa. Na siye leo batu banatucheka juu tunaamua kama hatutatumainia banadamu bamalize magumu yetu yote, ao kutumainia kama makuta njo itatuletea furaha mu maisha. Juu ya nini tunakamata ile uamuzi? Ni juu tunajua kama huu ulimwengu utapita. Tunangoya “muji wenye uko na misingi ya kweli,” “wenye utakuja,” ni kusema Ufalme wa Mungu.a (Ebr. 11:10; Mt. 6:33) Mu kila kichwa kidogo ya hii habari tutazungumuzia: (1) namna mashauri ya Paulo yenye iliongozwa na roho ilisaidia Bakristo ba mu karne ya kwanza baendelee kutafuta muji “wenye utakuja,” (2) namna Paulo alibasaidia kujitayarisha juu ya mambo yeye ingetokea, na (3) namna ile mashauri ya Paulo inatusaidia leo.
TUMAINIA ULE MWENYE HAWEZI KUKUACHA
4. Juu ya nini Yerusalemu ilikuwa muji wa maana kwa Bakristo?
4 Ni mu Yerusalemu njo kutaniko ya Kikristo ya kwanza ilianzishwa mu mwaka wa 33 K.K.Y., na ni mule njo mulikuwa baraza yenye kuongoza. Njo maana muji wa Yerusalemu ulikuwa wa maana sana kwa Bakristo. Tena Bakristo ba Yerusalemu balikuwa na manyumba na bitu bingine bya mingi. Lakini, Yesu alionya banafunzi yake kama bangelazimika kutoka mu Yerusalemu na hata mu Yudea.—Mt. 24:16.
5. Paulo alitayarisha namna gani Bakristo juu ya mambo yenye ingetokea?
5 Ili kutayarisha Bakristo juu ya mambo yenye ingetokea, Paulo alibasaidia baelewe mawazo ya Yehova kuhusu Yerusalemu. Alibakumbusha kama Yehova hakukubali tena hekalu, makuhani, na zabihu zenye zilikuwa natolewa Yerusalemu. (Ebr. 8:13) Pia batu mingi mu Yerusalemu balimukatala Masiya. Kwa hiyo, Yerusalemu haikukuwa tena fasi yenye batu balipaswa kuenda juu ya kumuabudu Yehova na karibuni ingeharibiwa.—Lu. 13:34, 35.
6. Juu ya nini maneno yenye Paulo alikumbusha Bakristo mu Waebrania 13:5, 6 ingebasaidia sana?
6 Wakati Paulo aliandikia Bakristo Baebrania, Yerusalemu ilikuwa muji yenye kuendelea sana. Muandikaji moya Muroma wa ile wakati alisema kama Yerusalemu njo ilikuwa muji ya kujulikana sana mu ile eneo. Kila mwaka Bayahudi ba kutoka mu maeneo ya mingi balikuwa naenda Yerusalemu juu ya kufanya sikukuu mbalimbali, na ile ilileta makuta mingi mu ule muji. Inawezekana ile ilifanya Bakristo fulani bakuwe pia na makuta mingi. Na pengine njo maana Paulo alibashauria hivi: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.” Kisha alitaya maneno fulani yenye kuwa mu Maandiko. Mu ile maneno Yehova anahakikishia hivi kila mutumishi wake: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” (Soma Waebrania 13:5, 6; Kum. 31:6; Zb. 118:6) Juu ya nini ile maneno ya Yehova ilisaidia sana Bakristo ya Yerusalemu na Yudea? Juu wakati kidogo kisha kupata ile barua ya Paulo, bangelazimika kuacha manyumba, makazi, na bitu yabo yote, na bangeanza maisha ya mupya kwenye bangekimbilia.
7. Juu ya nini tangu leo tunapaswa kumutegemea sana Yehova?
7 Mambo yenye tunajifunza: Karibuni kutatokea “taabu kubwa” na huu ulimwengu wa Shetani utaharibiwa. (Mt. 24:21) Njo maana, sawa Bakristo ba mu karne ya kwanza, tunapaswa kuendelea kuwa baaminifu na kuwa tayari juu ya mambo yenye itatokea. (Lu. 21:34-36) Wakati wa taabu kubwa itaomba tukuwe hakika kabisa kama Yehova hawezi kuacha batu yake. Juu ya nini itaomba tukuwe hakika na ile jambo? Juu pengine tutalazimika kuacha bitu yetu fulani ao bitu yetu yote. Tangu leo, hata mbele taabu kubwa ianze, tujichunguze na tuone ni nani tunategemea. Ujiulize hivi: ‘Matendo yangu na mipango yenye niko nayo inaonyesha kama sitegemee utajiri lakini ninamutegemea Mungu mwenye anaahidi kama atanihangaikia?’ (1 Ti. 6:17) Mufano wa Bakristo ba zamani unaweza kutusaidia tubakie baaminifu wakati wa taabu kubwa. Lakini tusisaabu kama “taabu kubwa” yenye iko nakuya itakuwa ya matata sana. Taabu ya vile haiyatokeaka na haitatokeaka tena. Sasa, tutajua namna gani bya kufanya wakati ile taabu kubwa itaanza?
TII BENYE KUONGOZA
8. Yesu alipatia banafunzi yake maagizo gani?
8 Miaka kidogo kisha Bakristo Baebrania kupokea barua ya Paulo, majeshi ya Roma ilizunguka muji wa Yerusalemu. Wakati Bakristo baliona ile, balitambua kama ile njo wakati wa kukimbia, juu Yerusalemu ilikuwa karibu kuharibiwa. (Mt. 24:3; Lu. 21:20, 24) Lakini bangekimbilia wapi? Yesu alisema tu: “Wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.” (Lu. 21:21) Milima ilikuwa ya mingi mu ile eneo, sasa bangekimbilia ku milima gani?
9. Juu ya nini Bakristo bangejiuliza ni ku milima ya gani njo bangekimbilia? (Ona karte.)
9 Bakristo bangejiuliza ni ku milima gani njo bangekimbilia juu kulikuwa milima ya mingi. Kwa mufano kulikuwa milima ya Samaria, milima ya Galilaya, Mulima Hermoni na milima ya Lebanoni, na pia milima yenye ilikuwa ngambo ingine ya Muto Yordani. (Ona karte.) Miji fulani yenye ilikuwa ku ile milima ilionekana kuwa salama. Kwa mufano muji wa Gamla ulikuwa yulu ku mulima ya murefu na ilikuwa nguvu kufika kule. Bayahudi fulani baliwaza kama ilikuwa fasi ya muzuri ya kukimbilia. Lakini Baroma baliharibu ule muji na batu mingi balikufa.b
Kulikuwa milima mingi kwenye Bakristo bangekimbilia, lakini haiko yote njo ilikuwa salama (Ona fungu ya 9)
10-11. (a) Inawezekana Yehova alipatia batu yake muongozo namna gani? (Waebrania 13:7, 17) (b) Bakristo balipata matokeo gani juu balitii benye balikuwa nabaongoza? (Ona pia picha.)
10 Inaonekana kama Yehova alitumikisha bandugu benye kuongoza mu kutaniko juu ya kupatia Bakristo muongozo. Mwanahistoria Ezebyus aliandika kama Mungu alifunulia bandugu fulani mu Yerusalemu kama Bakristo banapaswa kutoka Yerusalemu na kukimbilia Pela, muji wenye ulikuwa mu eneo ya Perea. Pela ilikuwa kabisa fasi ya muzuri ya kukimbilia. Ilikuwa mwepesi kufika kule juu haikukuwa mbali na Yerusalemu. Zaidi ya ile, batu mingi mu ule muji habakukuwa Bayahudi, njo maana habakukuwa najaribu kupigana na Baroma.—Ona karte.
11 Bakristo benye balikimbilia ku milima balifuata hii shauri ya Paulo: “Mutii wale wenye wanaongoza kati yenu” mu kutaniko. (Soma Waebrania 13:7, 17.) Matokeo ilikuwa nini? Batu ya Mungu baliokoka juu balitii. Mambo yenye ilitokea kisha, inaonyesha kama Mungu hakubaacha juu ‘balingojea muji wenye uko na misingi ya kweli,’ ni kusema Ufalme wa Mungu.—Ebr. 11:10.
Pela ilikuwa fasi ya muzuri ya kukimbilia (Ona fungu ya 10-11)
12-13. Yehova ameongoza namna gani batu yake mu bipindi bya nguvu?
12 Mambo yenye tunajifunza: Yehova anatumikisha benye kuongoza juu ya kupatia batu yake muongozo. Mu Biblia muko mifano ya mingi yenye inaonyesha namna Yehova alitumikisha banaume baaminifu juu ya kuongoza batu yake mu bipindi bya nguvu (Kum. 31:23; Zb. 77:20) Na siye leo tunaona mambo mingi yenye inatuhakikishia kama Yehova anaendelea kutumikisha banaume baaminifu ili kutuongoza.
13 Kwa mufano mu kipindi ya korona, ‘benye kuongoza’ balitupatia maagizo. Bazee balipata maagizo juu ya namna ya kuendelea kufanya mikutano na kusaidia bandugu na badada baendelee kumuabudu Yehova. Miezi kidogo kisha korona kuanza, tulifanya mukusanyiko wa eneo mu maluga zaidi ya 500. Tulifuata ile mukusanyiko kupitia Enternete, televizyo ao radio. Ilikuwa mara ya kwanza tufanye mukusanyiko vile. Korona haikufanya tuache kupata chakula ya kiroho. Njo maana tuliendelea kuwa na umoja. Kwa hiyo hata tupate magumu gani kesho ao kesho yake, tuko hakika kama Yehova ataendelea kusaidia benye kutuongoza bakamate maamuzi ya muzuri. Tumeona kama kutii sheria za Yehova na kumutegemea ni mambo ya maana sana. Lakini tuko na lazima ya sifa zingine juu tuendelee kujitayarisha juu ya taabu kubwa na juu tuweze kutenda kwa hekima mu ile kipindi ya nguvu sana. Ni sifa gani?
TUONYESHANE UPENDO WA KINDUGU NA UKARIBISHAJI WAGENI
14. Vile Waebrania 13:1-3 inaonyesha, Bakristo balipaswa kuonyesha sifa gani mbele Yerusalemu iharibiwe?
14 Ni kweli tunaonyeshanaka upendo, lakini saa taabu kubwa itaanza itaomba tuonyeshane upendo zaidi. Ile wakati itaomba tufuate mufano wa Bakristo ba Yerusalemu na Yudea. (Ebr. 10:32-34) Balikuwaka naonyeshana upendo, lakini mu miaka yenye ilitangulia uharibifu wa Yerusalemu, balipaswa kuonyeshana zaidi ‘upendo wa kindugu’ na “ukaribishaji-wageni.”c (Soma Waebrania 13:1-3.) Vile mwisho ya hii dunia iko nakaribia, na siye tunapaswa kupenda bandugu na badada yetu zaidi.
15. Juu ya nini Bakristo Baebrania balipaswa kuonyeshana upendo na ukaribishaji wageni wakati balikimbilia ku milima?
15 Majeshi ya Roma ilizunguka Yerusalemu, lakini bila kutazamia iliondoka. Ile ilipatia Bakristo nafasi ya kukimbia. Lakini balikimbia na bitu kidogo tu. (Mt. 24:17, 18) Njo maana wakati balikuwa mu njia ya kuenda ku milima balipaswa kusaidiana. Balipaswa pia kusaidiana kuanza maisha ya mupya wakati balifika Pela. Bandugu na badada bamingi balikuwa mu “uhitaji wa haraka,” balikuwa na lazima ya chakula, manguo, na fasi ya kuishi. Wakati Bakristo balisaidiana na kuchangia byenye balikuwa nabyo, balionyesha kama ni bakaribishaji-wageni na kama banapendana sana.—Tit. 3:14.
16. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda bandugu yetu benye biko na lazima ya musaada? (Ona pia picha.)
16 Mambo yenye tunajifunza: Tunapenda bandugu na badada yetu njo maana tunabasaidia wakati biko na lazima ya musaada. Kwa mufano, juu ya vita na misiba ya asili, bandugu mingi bamekimbilia mu maeneo ingine. Na bandugu ba mu ile maeneo bamebakaribisha na kubasaidia kupata bitu byenye biko nabyo lazima. Pia bamebasaidia baendelee kumuabudu Yehova. Dada moya wa Ukraine mwenye alikimbia vita anasema hivi: “Tuliona namna Yehova alitumikisha bandugu yetu juu ya kutusaidia na kutuongoza. Balitukaribisha muzuri na kutusaidia wakati tulikuwa Ukraine, wakati tulikuwa Hongrie, na biko naendelea kutusaidia hapa Alemanye.” Wakati tunahangaikia bandugu na badada yetu na kubakaribisha, tuko natumika pamoya na Yehova.—Mez. 19:17; 2 Ko. 1:3, 4.
Bakristo benye banakimbilia mu maeneo yetu biko na lazima ya musaada wetu (Ona fungu ya 16)
17. Juu ya nini ni jambo ya maana tangu leo tujifunze kuonyesha upendo wa kindugu na ukaribishaji-wageni?
17 Kwa kweli, mu siku zenye zitakuya itaomba tusaidie sana bandugu na badada yetu kupita hata vile tuko nafanya leo. (Ebr. 3:16-18) Njo maana tangu leo Yehova iko natusaidia tujue namna ya kuonyesha upendo wa kindugu na ukaribishaji-wageni juu zile sifa zitakuwa za lazima sana.
MAMBO YENYE ITATOKEA
18. Namna gani tunaweza kuiga Bakristo Baebrania?
18 Bakristo benye balikimbilia ku milima baliokoka wakati Yerusalemu iliharibiwa. Baliacha muji wa Yerusalemu, lakini Yehova hakubaacha. Tuseme nini juu yetu leo? Tunajua mambo yenye Biblia inasema juu ya wakati wenye kuya, lakini hatujue namna kila jambo itapitikana. Njo maana Yesu alitushauria tukuwe tayari kutenda. (Lu. 12:40) Tuko pia na mashauri yenye Paulo aliandikia Bakristo Baebrania. Ile mashauri inaweza kutusaidia leo sawa tu vile ilisaidiaka Bakristo ba zamani. Na Yehova yeye peke ametuhakikishia kama hatatutupa ao kutuacha hata siku moya. (Ebr. 13:5, 6) Njo maana tuendelee kutafuta kwa moyo wote muji wenye utadumu ni kusema Ufalme wa Mungu. Mu ule Ufalme wa Mungu tutapata baraka za mingi na tutaishi milele.—Mt. 25:34.
WIMBO 157 Tutaishi kwa Amani!
a Zamani mara mingi mufalme njo alikuwa natawala muji. Muji wa vile ungeweza kuonwa kuwa ufalme.—Mwa. 14:2.
b Ile ilitokea mu mwaka wa 67 K.K.Y., wakati kidogo tu kisha Bakristo kutoka Yerusalemu na Yudea.
c Maneno yenye inatafsiriwa ‘upendo wa kindugu’ inaweza kumaanisha upendo wenye kuwa kati ya batu ba karibu ba mu familia moya. Lakini Paulo alitumia ile maneno juu ya kuzungumuzia upendo wenye uko kati ya bandugu na badada bote mu kutaniko.