Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Wafalme—Yaliyomo

      • Eliya apelekwa juu katika dhoruba ya upepo (1-18)

        • Elisha apata vazi rasmi la Eliya (13, 14)

      • Elisha ayaponya maji ya Yeriko (19-22)

      • Dubu wawaua wavulana kutoka Betheli (23-25)

2 Wafalme 2:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “angani.”

Marejeo

  • +1Fa 17:1
  • +2Fa 2:11
  • +1Fa 19:16
  • +2Fa 4:38

2 Wafalme 2:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yako inavyoishi.”

Marejeo

  • +Mwa 28:18, 19; 1Fa 12:28, 29; 2Fa 2:23

2 Wafalme 2:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana maneno “wana wa manabii” yanarejelea shule ya kuwafundisha manabii au chama cha manabii.

Marejeo

  • +1Fa 19:16

2 Wafalme 2:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yako inavyoishi.”

Marejeo

  • +Yos 6:26; 1Fa 16:34

2 Wafalme 2:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yako inavyoishi.”

2 Wafalme 2:8

Marejeo

  • +1Fa 19:19
  • +Kut 14:21, 22; Yos 3:17; 2Fa 2:13, 14

2 Wafalme 2:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sehemu mbili za.”

Marejeo

  • +Kum 21:17
  • +Kum 34:9; 1Fa 19:16; Lu 1:17

2 Wafalme 2:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “angani.”

Marejeo

  • +2Fa 6:17; Zb 68:17
  • +2Nya 21:5, 12; Yoh 3:13

2 Wafalme 2:12

Marejeo

  • +2Fa 13:14
  • +2Sa 1:11, 12; Ayu 1:19, 20

2 Wafalme 2:13

Marejeo

  • +1Fa 19:19; 2Fa 1:8; Zek 13:4; Mt 3:4

2 Wafalme 2:14

Marejeo

  • +Yos 3:13; 2Fa 2:8

2 Wafalme 2:15

Marejeo

  • +Hes 11:24, 25; 27:18, 20; 2Fa 2:9

2 Wafalme 2:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upepo wa.”

Marejeo

  • +1Fa 18:11, 12

2 Wafalme 2:18

Marejeo

  • +Yos 6:26; 1Fa 16:34

2 Wafalme 2:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “yanaharibu mimba.”

Marejeo

  • +Kum 34:1-3

2 Wafalme 2:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kuharibu mimba.”

Marejeo

  • +Kut 15:23-25; 2Fa 4:38-41

2 Wafalme 2:23

Marejeo

  • +2Nya 36:15, 16; Lu 10:16

2 Wafalme 2:24

Marejeo

  • +Met 17:12
  • +2Fa 1:10

2 Wafalme 2:25

Marejeo

  • +2Fa 4:25

Jumla

2 Fal. 2:11Fa 17:1
2 Fal. 2:12Fa 2:11
2 Fal. 2:11Fa 19:16
2 Fal. 2:12Fa 4:38
2 Fal. 2:2Mwa 28:18, 19; 1Fa 12:28, 29; 2Fa 2:23
2 Fal. 2:31Fa 19:16
2 Fal. 2:4Yos 6:26; 1Fa 16:34
2 Fal. 2:81Fa 19:19
2 Fal. 2:8Kut 14:21, 22; Yos 3:17; 2Fa 2:13, 14
2 Fal. 2:9Kum 21:17
2 Fal. 2:9Kum 34:9; 1Fa 19:16; Lu 1:17
2 Fal. 2:112Fa 6:17; Zb 68:17
2 Fal. 2:112Nya 21:5, 12; Yoh 3:13
2 Fal. 2:122Fa 13:14
2 Fal. 2:122Sa 1:11, 12; Ayu 1:19, 20
2 Fal. 2:131Fa 19:19; 2Fa 1:8; Zek 13:4; Mt 3:4
2 Fal. 2:14Yos 3:13; 2Fa 2:8
2 Fal. 2:15Hes 11:24, 25; 27:18, 20; 2Fa 2:9
2 Fal. 2:161Fa 18:11, 12
2 Fal. 2:18Yos 6:26; 1Fa 16:34
2 Fal. 2:19Kum 34:1-3
2 Fal. 2:21Kut 15:23-25; 2Fa 4:38-41
2 Fal. 2:232Nya 36:15, 16; Lu 10:16
2 Fal. 2:24Met 17:12
2 Fal. 2:242Fa 1:10
2 Fal. 2:252Fa 4:25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
2 Wafalme 2:1-25

Kitabu cha Pili cha Wafalme

2 Yehova alipokuwa karibu kumchukua Eliya+ kuelekea mbinguni* katika dhoruba ya upepo,+ Eliya na Elisha+ wakaondoka Gilgali.+ 2 Eliya akamwambia Elisha: “Kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wakashuka kwenda Betheli.+ 3 Kisha wana wa manabii* huko Betheli wakaja kwa Elisha na kumuuliza: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kiongozi wako?”+ Ndipo akajibu: “Tayari najua. Nyamazeni.”

4 Sasa Eliya akamwambia: “Elisha, tafadhali kaa hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yeriko.”+ Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wakaenda Yeriko. 5 Kisha wana wa manabii waliokuwa Yeriko wakaenda kwa Elisha na kumuuliza: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kiongozi juu yako?” Ndipo akajibu: “Tayari najua. Nyamazeni.”

6 Sasa Eliya akamwambia: “Kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma Yordani.” Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wote wawili wakaendelea na safari. 7 Na wana 50 wa manabii wakaenda pia, wakasimama na kuwatazama kwa mbali wote wawili wakiwa wamesimama kando ya Mto Yordani. 8 Kisha Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akaliviringa na kuyapiga maji, nayo yakagawanyika kushoto na kulia, basi wote wawili wakavuka ng’ambo kupitia nchi kavu.+

9 Mara tu walipovuka, Eliya akamwambia Elisha: “Omba jambo unalotaka nikutendee kabla sijachukuliwa na kukuacha.” Basi Elisha akamuuliza: “Tafadhali, naweza kupata mafungu mawili+ ya* roho yako?”+ 10 Eliya akajibu: “Umeomba jambo gumu. Ikiwa utaniona nitakapochukuliwa na kukuacha, itakuwa hivyo kwako; lakini usiponiona, jambo hilo halitatokea.”

11 Walipokuwa wakitembea, huku wakizungumza, kwa ghafla gari la moto na farasi wa moto+ wakawatenganisha, na Eliya akapanda kuelekea mbinguni* katika dhoruba ya upepo.+ 12 Elisha alitazama huku akipaza sauti, “Baba yangu, baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!”+ Alipotoweka kabisa machoni pake, akashika mavazi yake mwenyewe na kuyararua vipande viwili.+ 13 Ndipo akaliokota vazi rasmi+ la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, akarudi na kusimama kwenye ukingo wa Yordani. 14 Kisha akachukua vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga maji na kuuliza: “Yuko wapi Yehova, Mungu wa Eliya?” Alipoyapiga maji, yaligawanyika kushoto na kulia, Elisha akavuka ng’ambo.+

15 Wana wa manabii waliokuwa Yeriko walipomwona kwa mbali, wakasema: “Roho ya Eliya imetua juu ya Elisha.”+ Basi wakaenda kukutana naye na kumwinamia mpaka ardhini. 16 Wakamwambia: “Hapa sisi watumishi wako tuna wanaume mashujaa 50. Tafadhali, waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda roho ya* Yehova imemwinua juu na kumtupa juu ya mojawapo ya milima au katika mojawapo ya mabonde.”+ Lakini akawaambia: “Msiwatume.” 17 Hata hivyo, waliendelea kumsihi mpaka akaona aibu, kwa hiyo akasema: “Watumeni.” Wakawatuma wanaume 50, nao wakaendelea kumtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata. 18 Waliporudi kwake, alikuwa anakaa Yeriko.+ Kisha akawauliza: “Je, sikuwaambia msiende?”

19 Baada ya muda watu wa jiji hilo wakamwambia Elisha: “Bwana wetu, unaona kwamba jiji hili liko mahali pazuri;+ lakini maji ni mabaya, na wakaaji wa nchi ni tasa.”* 20 Akawaambia: “Nileteeni bakuli dogo jipya, mweke chumvi ndani yake.” Basi wakamletea. 21 Kisha akatoka na kwenda kwenye chemchemi ya maji hayo, akatupa chumvi ndani yake+ na kusema: “Yehova anasema hivi: ‘Nimeyaponya maji haya. Hayatasababisha tena kifo wala utasa.’”* 22 Na maji hayo yameponywa mpaka leo hii, kulingana na neno alilosema Elisha.

23 Akapanda kutoka huko na kwenda Betheli. Alipokuwa akitembea njiani, wavulana fulani walitoka jijini na kuanza kumdhihaki,+ wakaendelea kumwambia: “Panda juu, wewe mwenye upara! Panda juu, wewe mwenye upara!” 24 Hatimaye akageuka na kuwatazama, akawalaani katika jina la Yehova. Ndipo dubu jike wawili+ wakatoka msituni na kuwararua vipandevipande watoto 42.+ 25 Kutoka huko, akaendelea na safari mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka huko akarudi Samaria.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki