Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, nabii Nathani alipokuja kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+
51 Ee Mungu, nionyeshe kibali kulingana na upendo wako mshikamanifu.+
Yafute kabisa makosa yangu kulingana na rehema zako nyingi.+
Kwa hiyo, wewe ni mwadilifu unapoongea,
Wewe ni mwenye haki katika hukumu yako.+
6 Tazama! Unapendezwa na ukweli katika utu wa ndani;+
Ufundishe utu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.
7 Nisafishe kutoka katika dhambi yangu kwa hisopo, ili niwe safi;+
Nioshe, ili niwe mweupe kuliko theluji.+
8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,
Ili mifupa uliyoiponda ishangilie.+
11 Usinitupe kutoka mbele zako;*
Wala usiniondolee roho yako takatifu.
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,+
Ili watenda dhambi wakurudie.
14 Niokoe kutoka katika hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+
Ili ulimi wangu utangaze uadilifu wako kwa shangwe.+
15 Ee Yehova, ifungue midomo yangu,
Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+
17 Dhabihu zinazompendeza Mungu ni roho iliyovunjika;
18 Kwa nia yako njema litendee jiji la Sayuni jambo jema;
Zijenge kuta za Yerusalemu.
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,
Dhabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;
Kisha ng’ombe dume watatolewa kwenye madhabahu yako.+