Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Luka 21
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Luka—Yaliyomo

      • Sarafu mbili za mjane maskini (1-4)

      • ISHARA YA MAMBO YATAKAYOKUJA (5-36)

        • Vita, matetemeko makubwa ya ardhi, magonjwa, upungufu wa chakula (10, 11)

        • Yerusalemu lazingirwa na majeshi (20)

        • Nyakati zilizowekwa za mataifa (24)

        • Kuja kwa Mwana wa binadamu (27)

        • Mfano wa mtini (29-33)

        • Endeleeni kukesha (34-36)

      • Yesu afundisha hekaluni (37, 38)

Luka 21:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “makasha.”

Marejeo

  • +Mk 12:41

Luka 21:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “leptoni mbili.” Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Mk 12:42

Luka 21:3

Marejeo

  • +Mk 12:43, 44; 2Ko 8:12

Luka 21:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au, “mwenye uhitaji.”

Marejeo

  • +Mt 22:37

Luka 21:5

Marejeo

  • +Mt 24:1, 2; Mk 13:1, 2

Luka 21:6

Marejeo

  • +Lu 19:44

Luka 21:7

Marejeo

  • +Mt 24:3; Mk 13:4

Luka 21:8

Marejeo

  • +2Ti 3:13; 1Yo 4:1; Ufu 12:9
  • +Mt 24:4, 5; Mk 13:5, 6

Luka 21:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “misukosuko.”

Marejeo

  • +Mt 24:6; Mk 13:7

Luka 21:10

Marejeo

  • +Ufu 6:4
  • +Mt 24:7; Mk 13:8

Luka 21:11

Marejeo

  • +Mdo 11:28; Ufu 6:8

Luka 21:12

Marejeo

  • +Yoh 16:2
  • +Mt 10:17, 18; 24:9; Mk 13:9; Mdo 25:23; Ufu 2:10

Luka 21:14

Marejeo

  • +Lu 12:11, 12

Luka 21:15

Marejeo

  • +Mk 13:11; Mdo 6:8, 10

Luka 21:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtasalitiwa.”

Marejeo

  • +Mik 7:6; Mk 13:12, 13; Mdo 7:59

Luka 21:17

Marejeo

  • +Mt 10:22; 24:9

Luka 21:18

Marejeo

  • +Mt 10:29, 30; Lu 12:6, 7

Luka 21:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtapata nafsi zenu.”

Marejeo

  • +Mt 24:13; Ro 5:3, 4; Ebr 10:36; 2Pe 1:5, 6

Luka 21:20

Marejeo

  • +Lu 19:43
  • +Da 9:26; Mt 23:37, 38; 24:15, 16

Luka 21:21

Marejeo

  • +Mk 13:14

Luka 21:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “siku za kisasi.”

Luka 21:23

Marejeo

  • +Mt 24:19; Mk 13:17; Lu 23:28, 29

Luka 21:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Watu wa mataifa.”

  • *

    Au “Watu wa mataifa.”

Marejeo

  • +Kum 28:64; Da 9:26
  • +Da 4:25

Luka 21:25

Marejeo

  • +Mt 24:29; Mk 13:24, 25

Luka 21:27

Marejeo

  • +Da 7:13
  • +Mt 24:30; Mk 13:26; Ufu 1:7

Luka 21:29

Marejeo

  • +Mt 24:32, 33; Mk 13:28, 29

Luka 21:32

Marejeo

  • +Mt 24:34; Mk 13:30

Luka 21:33

Marejeo

  • +Mt 24:35; Mk 13:31

Luka 21:34

Marejeo

  • +Isa 5:11, 12; Ro 13:13
  • +Met 11:4; Mt 6:25; 1Ti 6:8

Luka 21:35

Marejeo

  • +1Th 5:2, 3; 2Pe 3:10

Luka 21:36

Marejeo

  • +Mt 25:13; Mk 13:33; 1Ko 16:13; 1Pe 5:8
  • +Ro 12:12; Efe 6:18; 1Pe 4:7
  • +Mt 24:42; Mk 13:35; Ufu 6:16, 17; 16:15

Jumla

Luka 21:1Mk 12:41
Luka 21:2Mk 12:42
Luka 21:3Mk 12:43, 44; 2Ko 8:12
Luka 21:4Mt 22:37
Luka 21:5Mt 24:1, 2; Mk 13:1, 2
Luka 21:6Lu 19:44
Luka 21:7Mt 24:3; Mk 13:4
Luka 21:82Ti 3:13; 1Yo 4:1; Ufu 12:9
Luka 21:8Mt 24:4, 5; Mk 13:5, 6
Luka 21:9Mt 24:6; Mk 13:7
Luka 21:10Ufu 6:4
Luka 21:10Mt 24:7; Mk 13:8
Luka 21:11Mdo 11:28; Ufu 6:8
Luka 21:12Yoh 16:2
Luka 21:12Mt 10:17, 18; 24:9; Mk 13:9; Mdo 25:23; Ufu 2:10
Luka 21:14Lu 12:11, 12
Luka 21:15Mk 13:11; Mdo 6:8, 10
Luka 21:16Mik 7:6; Mk 13:12, 13; Mdo 7:59
Luka 21:17Mt 10:22; 24:9
Luka 21:18Mt 10:29, 30; Lu 12:6, 7
Luka 21:19Mt 24:13; Ro 5:3, 4; Ebr 10:36; 2Pe 1:5, 6
Luka 21:20Lu 19:43
Luka 21:20Da 9:26; Mt 23:37, 38; 24:15, 16
Luka 21:21Mk 13:14
Luka 21:23Mt 24:19; Mk 13:17; Lu 23:28, 29
Luka 21:24Kum 28:64; Da 9:26
Luka 21:24Da 4:25
Luka 21:25Mt 24:29; Mk 13:24, 25
Luka 21:27Da 7:13
Luka 21:27Mt 24:30; Mk 13:26; Ufu 1:7
Luka 21:29Mt 24:32, 33; Mk 13:28, 29
Luka 21:32Mt 24:34; Mk 13:30
Luka 21:33Mt 24:35; Mk 13:31
Luka 21:34Isa 5:11, 12; Ro 13:13
Luka 21:34Met 11:4; Mt 6:25; 1Ti 6:8
Luka 21:351Th 5:2, 3; 2Pe 3:10
Luka 21:36Mt 25:13; Mk 13:33; 1Ko 16:13; 1Pe 5:8
Luka 21:36Ro 12:12; Efe 6:18; 1Pe 4:7
Luka 21:36Mt 24:42; Mk 13:35; Ufu 6:16, 17; 16:15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Luka 21:1-38

Kulingana na Luka

21 Yesu alipotazama, aliwaona matajiri wakitumbukiza zawadi zao katika masanduku* ya hazina.+ 2 Ndipo akamwona mjane mmoja maskini akitumbukiza sarafu mbili ndogo zenye thamani ndogo sana,*+ 3 naye akasema: “Kwa kweli ninawaambia, mjane huyu maskini ametumbukiza zaidi ya wote.+ 4 Kwa maana wote hao walitumbukiza zawadi kutokana na ziada yao, lakini mwanamke huyu ingawa ni maskini* alitumbukiza riziki yake yote.”+

5 Baadaye, watu fulani walipokuwa wakisema jinsi hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na vitu vilivyowekwa wakfu,+ 6 akawaambia: “Vitu hivi mnavyoona, siku zitakuja ambapo hakuna jiwe litakaloachwa juu ya jiwe lingine bila kuangushwa chini.”+ 7 Ndipo wakamuuliza: “Mwalimu, kwa kweli mambo haya yatatukia lini, na ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya yanakaribia kutokea?”+ 8 Akasema: “Jihadharini msipotoshwe,+ kwa maana wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati unaofaa umekaribia.’ Msiwafuate.+ 9 Pia, mtakaposikia kuhusu vita na machafuko* msiogope. Kwa maana lazima mambo hayo yatukie kwanza, lakini ule mwisho hautatokea mara moja.”+

10 Kisha akawaambia: “Taifa litapigana na taifa,+ na ufalme kupigana na ufalme.+ 11 Kutakuwa na matetemeko makubwa ya ardhi, na magonjwa na upungufu wa chakula katika sehemu mbalimbali;+ pia kutakuwa na mambo yenye kuogopesha na ishara kubwa kutoka mbinguni.

12 “Lakini kabla ya mambo hayo yote kutokea, watu watawakamata ninyi na kuwatesa+ na kuwakabidhi kwenye masinagogi na magereza. Mtapelekwa mbele ya wafalme na magavana kwa sababu ya jina langu.+ 13 Hivyo, mtapata nafasi ya kutoa ushahidi. 14 Kwa hiyo, azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema kuhusu jinsi mtakavyojitetea,+ 15 kwa maana nitawapa maneno na hekima, ambayo wapinzani wenu wote kwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+ 16 Zaidi ya hayo, mtakabidhiwa* hata na wazazi, ndugu, watu wa ukoo, na rafiki zenu, nao watawaua baadhi yenu,+ 17 nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ 18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaoangamia.+ 19 Mkivumilia, mtauokoa uhai wenu.*+

20 “Hata hivyo, mtakapoona Yerusalemu limezingirwa na majeshi yaliyopiga kambi,+ jueni kwamba linakaribia kuharibiwa.+ 21 Ndipo wale walio Yudea waanze kukimbilia milimani,+ na wale walio Yerusalemu waondoke, nao wale walio mashambani wasiingie ndani yake, 22 kwa sababu hizi ni siku za kutekeleza haki,* ili mambo yote yaliyoandikwa yatimizwe. 23 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto katika siku hizo!+ Kwa maana kutakuwa na mateso mengi katika nchi na ghadhabu dhidi ya watu hawa. 24 Nao wataangamizwa kwa upanga na watapelekwa utekwani katika mataifa yote;+ na Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa,* mpaka nyakati zilizowekwa za mataifa* zitimie.+

25 “Pia, kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota,+ na duniani mataifa yatakuwa na maumivu makali bila kujua cha kufanya kwa sababu ya mngurumo na msukosuko wa bahari. 26 Watu watazimia kwa woga wakitarajia mambo yatakayotokea juu ya dunia inayokaliwa, kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa. 27 Ndipo watakapomwona Mwana wa binadamu+ akija katika mawingu akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+ 28 Lakini mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.”

29 Ndipo akawaambia mfano huu: “Angalieni mtini na miti mingine yote.+⁠ 30 Inapochipua, mnaona na kujua kwamba kiangazi kinakaribia. 31 Vivyo hivyo, ninyi pia mtakapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia. 32 Kwa kweli ninawaambia, kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote yatukie.+ 33 Mbingu na dunia zitapitilia mbali, lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe.+

34 “Lakini jiangalieni wenyewe ili mioyo yenu isilemewe kamwe na kula na kunywa kupita kiasi+ na mahangaiko ya maisha,+ na siku ile iwakute ghafla 35 kama mtego.+ Kwa maana itakuja juu ya wale wote wanaoishi juu ya uso wa dunia. 36 Basi, endeleeni kukesha+ sikuzote mkiomba dua+ ili mfanikiwe kuponyoka mambo yote hayo ambayo lazima yatukie, na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.”+

37 Yesu alikuwa akifundisha hekaluni mchana, lakini usiku alienda kukaa kwenye Mlima wa Mizeituni.⁠ 38 Watu wote walikuwa wakija hekaluni asubuhi na mapema ili wamsikilize.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki