Isaya
46 Beli anainama,+ Nebo anajikunja.
Sanamu zao zimepakizwa juu ya wanyama, juu ya wanyama wa kubeba mizigo,+
Kama mizigo yenye kulemea wanyama wenye kuchoka.
3 “Munisikilize, Ee nyumba ya Yakobo, na ninyi wote wenye kubakia wa nyumba ya Israeli,+
Ninyi wenye nilitegemeza tangu wakati mulizaliwa na kuwabeba tangu tumbo la uzazi.+
4 Mupaka wakati mutazeeka nitakuwa uleule;+
Mupaka wakati kichwa chenu kitakuwa na imvi nitaendelea kuwabeba.
Kama vile nimefanya, nitawachukua na kuwabeba na kuwaokoa.+
5 Mutanifananisha na nani ao kunifanya kuwa sawa na nani ao kunilinganisha na nani,+
Ili tufanane naye?+
Wanalipa fundi wa metali, na anaitengeneza kuwa mungu.+
Kisha wanainamisha uso mupaka chini, ndiyo, wanaiabudu.*+
Haiondoke mahali pake.+
Wanasema nayo kwa sauti kubwa, lakini haijibu;
Haiwezi kuokoa mutu yeyote katika taabu.+
8 Mukumbuke jambo hili, na mujipe moyo.
Muliweke katika moyo, ninyi wakosaji.
9 Mukumbuke mambo ya kwanza ya zamani sana,
Kwamba mimi ni Mungu na hakuna mwingine.
Mimi ni Mungu na hakuna mwenye kuwa kama mimi.+
Nimesema, na nitafanya litokee.
Nimekusudia, na pia nitalitimiza.+
Nitaleta wokovu katika Sayuni, na utukufu wangu kwa Israeli.”+