Mezali
2 Mutumishi mwenye ufahamu atatawala juu ya mwana mwenye anatenda kwa haya;
Atapokea uriti kama mumoja wa ndugu za mwana huyo.
3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+
Lakini Yehova ndiye anachunguza mioyo.+
4 Mutu muovu anasikiliza maneno yenye kuumiza,
Na mutu mudanganyifu anasikiliza ulimi wenye uovu.+
5 Mutu yeyote mwenye kuchekelea maskini anatukana Mutengenezaji wake,+
Na kila mutu mwenye anafurahia musiba wa mwingine hatakosa kupewa azabu.+
7 Maneno manyoofu* hayamufae mupumbavu.+
Namna gani maneno ya uongo kwa mutawala!*+
8 Zawadi ni kama jiwe lenye samani kwa mwenye kuwa nayo;*+
Kila mahali kwenye anageukia, linamuletea mafanikio.+
9 Kila mutu mwenye anasamehe* kosa anatafuta upendo,+
Lakini ule mwenye anaendelea kuongea juu ya jambo anatenganisha marafiki wa karibu.+
11 Mutu mubaya anatafuta uasi tu,
Lakini mujumbe mwenye hana huruma atatumwa ili kumupatia azabu.+
12 Ni muzuri zaidi kukutana na dubu mwenye amepoteza vitoto vyake
Kuliko kukutana na mujinga katika upumbavu wake.+
13 Kama mutu analipa ubaya kwa wema,
Ubaya hautaondoka katika nyumba yake.+
15 Mutu yeyote mwenye kumuhesabia muovu kuwa hana kosa na mutu yeyote mwenye kumuhukumu mwenye haki kuwa na kosa+
—Wote wawili ni chukizo kwa Yehova.
17 Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote+
Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+
18 Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anapana mukono na kukubali
Kulipia mwingine mukopo mbele ya jirani yake.+
19 Mutu mwenye anapenda ugomvi anapenda kosa.+
Kila mutu mwenye anainua mahali pake pa kuingilia anaalika taabu.+
20 Mutu mwenye kupotoka katika moyo hatapata mafanikio,*+
Na ule mwenye kusema maneno ya udanganyifu ataanguka katika uharibifu.
21 Baba mwenye anazaa mutoto mwenye hana akili atakuwa na huzuni;
Na baba ya mutoto mwenye hana akili hana furaha.+
24 Hekima iko kabisa mbele ya mutu mwenye utambuzi,
Lakini macho ya mujinga yanaenda huku na huku mupaka kwenye miisho ya dunia.+
26 Haiko muzuri kumupatia mwenye haki azabu,*
Na kupiga viboko watu wenye kuheshimiwa ni kinyume na mambo yenye kuwa sawa.
28 Hata mupumbavu mwenye anabakia kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,
Na ule mwenye anafunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.