Zaburi
Kuhusu Sulemani.
72 Ee Mungu, umupatie mufalme hukumu zako,
Na umupatie mwana wa mufalme haki yako.+
3 Milima iletee watu amani,
Na vilima vilete haki.
4 Acha atetee* watu wa hali ya chini katika taifa,
Acha aokoe wana wa maskini,
Na acha amuponde mupunjaji.+
6 Atakuwa kama mvua yenye kuanguka juu ya majani yenye yalikatwa,
Kama matone ya mvua yenye kumwangilia dunia maji.+
7 Katika siku zake mwenye haki atasitawi,*+
Na amani itakuwa nyingi+ mupaka wakati mwezi utakuwa hauko tena.
10 Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa watalipa ushuru.+
Wafalme wa Sheba na wa Seba watatoa zawadi.+
11 Wafalme wote watainama mbele yake,
Na mataifa yote yatamutumikia.
12 Kwa maana ataokoa maskini mwenye kulilia musaada,
Pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi.
14 Atawaokoa* katika ukandamizaji na katika jeuri,
Na damu yao itakuwa na samani mbele ya macho yake.
15 Aishi na kupewa zahabu ya Sheba.+
Sala ziendelee kutolewa kwa ajili yake,
Na abarikiwe muchana wote.
Watu wajipatie baraka kupitia yeye;+
Mataifa yote yamutangaze kuwa mwenye furaha.
Amina na Amina.
20 Huu ndio mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.+