Yobu
37 “Kwa sababu hiyo moyo wangu unapiga-piga
Na kuruka-ruka mahali pake.
2 Musikilize kwa uangalifu mungurumo wa sauti yake
Na mungurumo wenye unatoka katika kinywa chake.
3 Anaeneza mungurumo huo chini ya mbingu yote
Na anatuma umeme wake wa radi+ mupaka kwenye miisho ya dunia.
4 Kisha hilo kuko sauti ya mungurumo;
Ananguruma kwa sauti kubwa sana,+
Na hazuie radi yake wakati sauti yake inasikiwa.
5 Mungu ananguruma kwa sauti yake+ kwa njia ya ajabu;
Anafanya mambo makubwa yenye hatuwezi kuelewa.+
7 Mungu anasimamisha kazi zote za wanadamu*
Ili kila mwanadamu mwenye anaweza kufa atambue kazi Yake.
8 Wanyama wa pori wanaingia katika mapango yao
Na wanabakia ndani ya mashimo yao.
11 Ndiyo, anabebesha mawingu muzigo wa majimaji;
Anasambaza umeme wake wa radi+ katika mawingu;
12 Yanaenda kwa kuzunguka-zunguka mahali kwenye anayaelekeza;
Yanatimiza kila kitu chenye anaamuru+ juu ya uso wa dunia yenye kuikaliwa na watu.*
13 Ikuwe kwa ajili ya azabu*+ ao kwa ajili ya inchi
Ao kwa ajili ya upendo mushikamanifu, anafanya hilo litokee.+
15 Je, unajua namna Mungu anaongoza* mawingu
Na namna anafanya umeme wa radi uangaze kutoka katika wingu lake?
16 Je, unajua namna mawingu yanaelea?+
Hizo ni kazi za ajabu za Ule mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi.+
17 Sababu gani nguo zako zinakuwa na moto
Wakati dunia imetulia kwa sababu ya upepo wa kusini?+
19 Utuambie kile tunapaswa kumuelezea;
Hatuwezi kujibu kwa sababu tuko katika giza.
20 Je, anapaswa kujulishwa kwamba ninataka kusema?
Ao mutu yeyote amesema jambo lenye anapaswa kujulishwa?+
21 Hawawezi hata kuona mwangaza,*
Hata kama unangaa katika anga,
Mupaka upepo upite na kuondoa mawingu.
22 Kungaa kama vile zahabu kunatoka kaskazini;
Utukufu wa Mungu+ ni wenye kuogopesha sana.
23 Hatuwezi kumuelewa kabisa Mweza-Yote;+
Na hawezi hata siku moja kuvunja haki+ na uadilifu* wake mwingi.+
24 Kwa hiyo, watu wanapaswa kumuogopa.+
Kwa sababu yeye hafurahie mutu yeyote kati ya wale wenye wanawaza kwamba wako na hekima.”*+