Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w18 Mwezi wa 2 uku. 28-30
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SHANGWE NI NINI?
  • MIFANO YENYE TUNAPENDA KUIGA
  • SABABU ZA KUWA NA SHANGWE
  • NAMNA YA KUONGEZA SHANGWE YAKO
  • FAIDA ZENYE SHANGWE INALETA
  • “Mwenye Haki Atashangilia Katika Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
w18 Mwezi wa 2 uku. 28-30

Shangwe​—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu

  • UPENDO

  • SHANGWE

  • AMANI

  • USTAHIMILIVU

  • FAZILI

  • WEMA

  • IMANI

  • UPOLE

  • KUJIZUIA

KWA kawaida, watu wanapenda kuwa na maisha yenye shangwe. Lakini katika siku hizi za mwisho, watu wote wanapatwa na matatizo yenye kuwa ‘ngumu kushugulika nayo.’ (2 Tim. 3:1) Ukosefu wa haki, magonjwa, kukosa kazi, huzuni ao mambo mengine yenye kuleta mahangaiko na huzuni, yanaweza kufanya pole kwa pole watu fulani wapoteze shangwe yao. Hata watumishi wa Mungu wanaweza kuvunjika moyo na kupoteza shangwe yao. Ikiwa jambo hilo limekufikia, namna gani unaweza kuwa tena na shangwe?

Ili kujibia ulizo hilo, tunapaswa kwanza kuelewa shangwe ya kweli ni nini na namna wengine wameendelea kuwa na shangwe hata kama wamepatwa na magumu. Kisha, tutajifunza mambo yenye tunaweza kufanya ili kuendelea kuwa na shangwe na hata kuongeza shangwe yetu.

SHANGWE NI NINI?

Shangwe ni tofauti na kuwa tu mwenye kuchangumuka ao mwenye kucheka-cheka. Kwa mufano, kisha kunywa pombe sana, mulevi anaweza kuwa mwenye kucheka-cheka. Lakini, wakati ulevi unaisha, hacheke tena, na anaweza kurudilia maisha yenye huzuni na yenye kujaa magumu. Kuchangamuka kwake kwa wakati fulani haikukuwa shangwe ya kweli.​—Met. 14:13.

Lakini, shangwe ni sifa yenye kuwa ndani ya moyo. Shangwe inafasiriwa kuwa “furaha ya kuwa na kitu kizuri ao ya kutazamia kitu kizuri.” Shangwe ni hali ya furaha yenye tunaendelea kuwa nayo iwe hali zetu ni za muzuri ao hapana. (1 Tes. 1:6) Kwa kweli, mutu anaweza kuhangaishwa na jambo fulani lakini anaendelea kuwa na shangwe katika moyo wake. Kwa mufano, mitume walipigwa kwa sababu ya kuzungumuza juu ya Kristo. Lakini, ‘walitoka mbele ya Sanhedrini, wakishangilia kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake.’ (Mdo. 5:41) Kwa kweli, hawakukuwa wanashangilia kwa sababu ya kupigwa. Lakini, kwa sababu walikuwa watumishi wa Mungu, walipata shangwe ya kweli kwa sababu waliendelea kuwa washikaminifu kwake.

Hatuzaliwe na sifa ya shangwe; na sifa hiyo haijilete yenyewe. Sababu gani? Kwa sababu shangwe ya kweli ni sifa ya tunda la roho takatifu ya Mungu. Kwa musaada wa roho ya Mungu, tunaweza kufikia kuwa na ‘utu mupya,’ wenye kutia ndani shangwe. (Efe. 4:24; Gal. 5:22) Na wakati tunakomalisha sifa ya shangwe, tunakuwa na uwezo zaidi wa kupambana na mahangaiko ya maisha.

MIFANO YENYE TUNAPENDA KUIGA

Yehova alipenda mambo mazuri yajae katika dunia, haiko mambo ya mubaya yenye tunaona mara nyingi leo. Lakini, matendo ya mubaya ya wengine hayamufanye Yehova apoteze shangwe yake. Neno la Mungu linasema hivi: “Nguvu na shangwe zipo mahali pake [ao, katika makao yake].” (1 Nya. 16:27) Zaidi ya hilo, mambo ya muzuri yenye watumishi wa Yehova wanatimiza yanafanya ‘moyo wake ushangilie.’​—Met. 27:11.

Tunaweza kumuiga Yehova kwa kuepuka kuhangaika sana wakati mambo hayatendeke namna tulitazamia. Kuliko kupoteza shangwe yetu, tunaweza kukaza akili yetu juu ya mambo ya muzuri yenye tuko nayo leo, na kungojea kwa ustahimilivu ao kwa uvumilivu mambo ya muzuri zaidi ya wakati wenye kuja.a

Tunaweza pia kupata mifano mingi katika Biblia ya watu wenye waliendelea kuwa na shangwe wakati walipambana na majaribu. Abrahamu alivumilia hali zenye kutia maisha katika hatari na magumu yenye yaliletwa na wengine. (Mwa. 12:10-20; 14:8-16; 16:4, 5; 20:1-18; 21:8, 9) Hata kama alipambana na magumu hayo, Abrahamu aliendelea kuwa na shangwe katika moyo wake. Ni nini ilimusaidia kufanya hivyo? Alikuwa anafikiria sana tumaini lake la kuishi katika ulimwengu mupya katika utawala wa Masiya. (Mwa. 22:15-18; Ebr. 11:10) Yesu alisema hivi: “Baba yenu Abrahamu alishangilia sana katika tazamio la kuona siku yangu.” (Yoh. 8:56) Tunaweza kumuiga Abrahamu kwa kufikiria sana shangwe ya wakati wenye kuja.​—Rom. 8:21.

Kama Abrahamu, mutume Paulo na mwenzake Sila walikaza akili juu ya ahadi za Mungu. Walikuwa na imani yenye nguvu, na waliendelea kuwa na shangwe hata kama walipatwa na mambo yenye kuvunja moyo. Kwa mufano, kisha kupigwa mubaya sana na kutupwa katika gereza, ‘katikati ya usiku . . . walikuwa wanasali na kumusifu Mungu kwa wimbo.’ (Mdo. 16:23-25) Paulo na Sila walipata nguvu kwa sababu ya tumaini lao, lakini walikuwa pia na shangwe kwa sababu walikuwa wanateseka kwa ajili ya jina la Kristo. Tunaweza kuiga mufano wa Paulo na Sila kwa kuendelea kufikiria baraka za kumutumikia Mungu kwa uaminifu.​—Flp. 1:12-14.

Leo, katika familia yetu ya ndugu na dada wa ulimwenguni pote, kuko mifano ya muzuri ya watu wenye waliendelea kuwa na shangwe wakati wa magumu. Kwa mufano, katika Mwezi wa 11, 2013, upepo mukali wenye kuitwa Haiyan ulipiga sehemu ya katikati mwa Ufilipino, na kuharibu nyumba za familia za Mashahidi zaidi ya 1000. George, mwenye nyumba yake iliharibika sana katika muji wa Tacloban, alisema hivi: “Hata kama tulipatwa na magumu hayo, ndugu wako na furaha. Ni vigumu kwangu kueleza shangwe yenye tuko nayo.” Wakati tunapatwa na magumu makubwa, tutaendelea kuwa na shangwe ikiwa tunatafakari juu ya mambo yenye Yehova ametufanyia na kuendelea kuwa na shukrani kwake. Yehova ametutolea mambo gani mengine yenye yanatupatia sababu zingine za kuwa na shangwe?

SABABU ZA KUWA NA SHANGWE

Kwa kweli, sababu kubwa zaidi yenye kutuchochea tukuwe na shangwe ni urafiki wetu pamoja na Yehova. Fikiria jambo hili: tunajua mutu mwenye kuwa na Mamlaka Makubwa Zaidi Katika Ulimwengu. Ni Baba yetu, Mungu wetu, na Rafiki yetu!​—Zab. 71:17, 18.

Tunafurahia sana zawadi ya uzima na uwezo wenye tuko nao wa kufurahia uzima. (Mhu. 3:12, 13) Kwa sababu tuko viumbe wenye akili wenye Yehova amevuta kwake, tunaelewa mapenzi ya Mungu juu yetu. (Kol. 1:9, 10) Kwa hiyo, tuko na kusudi na muongozo katika maisha yetu. Lakini, watu wengi hawajue muzuri kusudi la maisha. Ili kuonyesha tofauti hiyo, mutume Paulo aliandika hivi: “‘Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaomupenda.’ Kwa maana ni kwetu sisi Mungu ameyafunua kupitia roho yake.” (1 Kor. 2:9, 10) Kwa kweli, tunafurahi sana kwa sababu tunaelewa mapenzi ya Yehova na kusudi lake.

Fikiria mambo mengine yenye Yehova amefanyia watu wake. Tunafurahi kwa sababu zambi zetu zinaweza kusamehewa. (1 Yoh. 2:12) Kwa sababu ya rehema ya Mungu, tuko na tumaini lenye kuwa hakika kwamba hivi karibuni ulimwengu mupya utakuja. (Rom. 12:12) Hata leo, Yehova anatupatia marafiki wengi wazuri, na tunaweza kumuabudu pamoja nao. (Zab. 133:1) Neno la Mungu linatuhakikishia pia kwamba Yehova analinda watu wake kutokana na Shetani na mashetani wake. (Zab. 91:11) Ikiwa tunatafakari juu ya baraka hizo zenye kutoka kwa Mungu, shangwe yetu itaongezeka na itakuwa kubwa zaidi.​—Flp. 4:4.

NAMNA YA KUONGEZA SHANGWE YAKO

Mukristo mwenye kuwa tayari na shangwe, anaweza kuongeza shangwe yake? Yesu alisema hivi: “Mambo haya nimewaambia, ili shangwe yangu ipate kuwa ndani yenu na shangwe yenu ipate kujaa.” (Yoh. 15:11) Hilo linaonyesha kabisa kama tunaweza kuongeza shangwe yetu. Unaweza kulinganisha bidii yako ya kuongeza shangwe yako na kufanya moto uendelee kuwaka. Unapaswa kuongeza kuni ili moto uendelee kuwaka. Vilevile, unapaswa kutia nguvu hali yako ya kiroho ili kuongeza shangwe yako. Kumbuka jambo hili: roho ya Mungu ndiyo inatoa shangwe. Kwa hiyo, utaongeza shangwe yako ikiwa unamuomba Yehova kwa ukawaida musaada wa roho yake takatifu na kusali na kutafakari juu ya Neno lake lenye kuongozwa na roho yake.​—Zab. 1:1, 2; Lu. 11:13.

Unaweza pia kuongeza shangwe yako kwa kufanya kwa bidii kazi zenye kumupendeza Yehova. (Zab. 35:27; 112:1) Sababu gani? Kwa sababu tuliumbwa ili ‘kumuogopa Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.’ (Mhu. 12:13) Ni kusema, tuliumbwa ili kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo, wakati tunamutumikia Yehova, kwa ukawaida tunakuwa na shangwe zaidi katika maisha yetu.b

FAIDA ZENYE SHANGWE INALETA

Ikiwa tunakomalisha sifa ya shangwe yenye kutoka kwa Mungu, tutapata faida zingine zaidi ya kujisikia tu kuwa wenye furaha. Kwa mufano, Baba yetu wa mbinguni atatufurahia zaidi wakati tunamutumikia kwa shangwe hata kama tunapambana na magumu ya namna gani. (Kum. 16:15; 1 Tes. 5:16-18) Pia, ikiwa tuko na shangwe ya kweli, tutaepuka maisha ya kufuatia vitu vya kimwili, lakini tutakuwa tayari kujinyima sana kwa ajili ya Ufalme wa Mungu. (Mt. 13:44) Wakati tunaona matokeo ya muzuri ya kujinyima, tutakuwa na shangwe zaidi, tutajisikia muzuri sana, na tutafanya wengine wakuwe na furaha.​—Mdo. 20:35; Flp. 1:3-5.

“Ikiwa uko na furaha na uko mwenye kutosheka leo katika maisha yako, inawezekana kabisa kuwa wakati wenye kuja utakuwa na afya ya muzuri.” Mutu mumoja mwenye kutafuta habari kwenye Masomo ya Juu ya Nebraska katika Amerika aliandika maneno hayo kisha kuchunguza habari mbalimbali juu ya afya. Hilo linapatana na Biblia, yenye kusema hivi: “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri.” (Met. 17:22) Kwa kweli, kadiri unaongeza shangwe yako, inawezekana kabisa kwamba utakuwa na afya ya muzuri.

Kwa hiyo, hata kama tunaishi wakati wenye kujaa mahangaiko, tunaweza kuwa na shangwe yenye kuendelea wakati tunapata roho takatifu kupitia sala, kujifunza, na kutafakari juu ya Neno la Yehova. Tunaweza pia kuongeza shangwe yetu kwa kufikiri juu ya baraka zenye tunapata leo, kwa kuiga imani ya wengine, na kujikaza kufanya mapenzi ya Mungu. Ikiwa tunafanya hivyo, tutajionea ukweli wa maneno yenye kuwa katika Zaburi 64:10 yenye kusema hivi: ‘Muadilifu atashangilia katika Yehova na kwa kweli atamukimbilia.’

a Sifa ya ustahimilivu itazungumuziwa wakati wenye kuja katika habari hizi zenye kuzungumuzia ‘tunda la roho.’

b Ili kujua njia zingine za kuongeza shangwe yako, soma kisanduku “Njia Zingine za Kuongeza Shangwe.”

Njia Zingine za Kuongeza Shangwe

  • Ukuwe na maisha mepesi na yenye hayana mambo mengi.​—Lu. 12:15.

  • Ukuwe mwenye kiasi juu ya mambo yenye unatazamia.​—Mika 6:8.

  • Uhakikishe kuwa programu yako (ya kazi, masomo, kujifurahisha, na mambo mengine) inakuruhusu kufuatia miradi ya kiroho. ​—Efe. 5:15, 16.

  • Ukuwe na usawaziko juu yako mwenyewe na juu ya wengine.​—Flp. 4:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine