Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 29
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu akumbuka maisha mazuri aliyokuwa nayo kabla ya mateso (1-25)

        • Aliheshimiwa kwenye lango la jiji (7-10)

        • Jinsi alivyokuwa akitenda haki awali (11-17)

        • Kila mtu alisikiliza ushauri wake (21-23)

Ayubu 29:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoa methali.”

Ayubu 29:3

Marejeo

  • +Zb 18:28; 119:105

Ayubu 29:4

Marejeo

  • +Zb 25:14; Met 3:32

Ayubu 29:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Watumishi.”

Ayubu 29:6

Marejeo

  • +Kum 32:13; 33:24

Ayubu 29:7

Marejeo

  • +Ru 4:1; Met 31:23
  • +Ne 8:1

Ayubu 29:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “walijificha.”

Marejeo

  • +Law 19:32

Ayubu 29:12

Marejeo

  • +Met 21:13; 24:11
  • +Yak 1:27

Ayubu 29:13

Marejeo

  • +Kum 24:12, 13
  • +Kum 10:17, 18

Ayubu 29:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, joho lisilo na mikono.

Ayubu 29:16

Marejeo

  • +Lu 14:13; Yak 1:27
  • +Met 29:7

Ayubu 29:17

Marejeo

  • +Zb 58:6; Met 30:14

Ayubu 29:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kwenye kiota changu.”

Marejeo

  • +Mwa 25:8; 2Fa 22:20

Ayubu 29:21

Marejeo

  • +Ayu 29:9

Ayubu 29:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “yalitonatona.”

Ayubu 29:23

Marejeo

  • +Zb 72:6; Met 16:15

Ayubu 29:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Hawakuitia giza nuru ya uso wangu.”

Ayubu 29:25

Marejeo

  • +Ayu 1:3
  • +Mhu 7:2

Jumla

Ayu. 29:3Zb 18:28; 119:105
Ayu. 29:4Zb 25:14; Met 3:32
Ayu. 29:6Kum 32:13; 33:24
Ayu. 29:7Ru 4:1; Met 31:23
Ayu. 29:7Ne 8:1
Ayu. 29:8Law 19:32
Ayu. 29:12Met 21:13; 24:11
Ayu. 29:12Yak 1:27
Ayu. 29:13Kum 24:12, 13
Ayu. 29:13Kum 10:17, 18
Ayu. 29:16Lu 14:13; Yak 1:27
Ayu. 29:16Met 29:7
Ayu. 29:17Zb 58:6; Met 30:14
Ayu. 29:18Mwa 25:8; 2Fa 22:20
Ayu. 29:21Ayu 29:9
Ayu. 29:23Zb 72:6; Met 16:15
Ayu. 29:25Ayu 1:3
Ayu. 29:25Mhu 7:2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 29:1-25

Ayubu

29 Ayubu akaendelea kuzungumza:*

 2 “Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa miezi ya zamani,

Siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,

 3 Alipoifanya taa yake iniangazie kichwani,

Nilipotembea gizani kwa nuru yake,+

 4 Nilipokuwa katika kilele cha mafanikio,

Urafiki pamoja na Mungu ulipohisiwa katika hema langu,+

 5 Mweza-Yote alipokuwa bado pamoja nami,

Watoto* wangu wote waliponizunguka,

 6 Nyayo zangu zilipoloweshwa katika siagi,

Na miamba iliponimwagia vijito vya mafuta.+

 7 Nilipokuwa nikienda kwenye lango la jiji+

Na kuketi mahali pangu kwenye uwanja wa jiji,+

 8 Vijana waliponiona walinipisha,*

Na hata wazee waliinuka na kuendelea kusimama.+

 9 Wakuu waliacha kuzungumza;

Walifunika kinywa chao kwa mkono wao.

10 Sauti za watu maarufu zilinyamazishwa;

Ulimi wao ulishikamana na kaakaa lao.

11 Yeyote aliyenisikia alinisifu,

Na wale walioniona walinitetea.

12 Kwa maana nilimwokoa maskini aliyelilia msaada,+

Pamoja na yatima na yeyote ambaye hakuwa na msaidizi.+

13 Mtu aliyekaribia kuangamia alinibariki,+

Nami niliufanya moyo wa mjane ushangilie.+

14 Nilivaa uadilifu kama mavazi yangu;

Haki yangu ilikuwa kama joho* na kilemba.

15 Nilikuwa macho kwa vipofu

Na miguu kwa walemavu.

16 Nilikuwa baba ya maskini;+

Nilichunguza kesi ya watu nisiowajua.+

17 Nilivunja mataya ya mwovu+

Na kuvuta mawindo kutoka katika meno yake.

18 Nilikuwa nikisema, ‘Nitafia nyumbani kwangu,*+

Na siku zangu zitakuwa nyingi kama chembe za mchanga.

19 Mizizi yangu itaenea ndani ya maji,

Na umande utakaa usiku kucha kwenye matawi yangu.

20 Utukufu wangu hufanywa kuwa mpya daima,

Na upinde ulio mkononi mwangu utaendelea kupiga mishale.’

21 Watu walisikiliza kwa hamu,

Walingojea kimyakimya ushauri wangu.+

22 Nilipomaliza kuongea, hawakuwa na la kuongezea;

Maneno yangu yalipenya taratibu* masikioni mwao.

23 Waliningojea kama wanavyongojea mvua;

Walifumbua vinywa vyao wazi kana kwamba wanangojea mvua ya masika.+

24 Nilipotabasamu, hawakuamini;

Nuru ya uso wangu iliwapa ujasiri.*

25 Niliwapa mwelekezo nikiwa kiongozi wao,

Nami niliishi kama mfalme anayezungukwa na majeshi yake,+

Kama mtu anayewafariji waombolezaji.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki